The Chant of Savant

Tuesday 10 July 2012

Waziri Nchimbi aache unafiki


Waziri wa mambo ya ndani  'Dk' Emanuel Nchimba amekaririwa akisema kuwa jeshi lake litawahoja viongozi wa CHADEMA kutokana na kutoa madai kuwa wanatishiwa kuuawa lakini wasiwe tayari kwenda kuripoti mauaji hayo polisi tokana na kutokuwa na imani na jeshi hilo. Wengi wanashangaa anapopata mshipa Nchimbi kuhadaa dunia kuwa usalama wa kila mtanzania si hiari. Je usalama wa Dk Steven Ulimboka nao ni sehemu ya huu anaosema Nchimbi au mikwara kwa vile wahusika ni wapinzani? Nchi inapotawaliwa na watu wanaosema bila kufikiri linageuka kuwa tatizo kubwa tu. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: