The Chant of Savant

Tuesday 29 September 2015

Kumbe Rugemalira ameiweka serikali ya Kikwete mfukoni!


Makama wa rais Dk Gharib Bilal akimpa tuzo mkurugenzi wa Mabibo Spirits James Rugemalira mtuhumiw amkuu wa ufisadi wa escrow. Huu ni ushahidi kuwa kumbe jamaa bado anao ubavu wa kupewa tuzo kwa biashara chafu iliyotokana na fedha za wizi wa mabilioni ya shilingi ya umma. Ndoa hii ya serikali na fisadi ni hatari na ya kukatisha tamaa ukiachia mbali kupaswa kulaaniwa. Badala ya mhalifu huyu kuwa gerezani sasa yuko majukwaani akichangia hata miradi ya serikali hiyo hiyo aliyoifilisi! Ni ujinga au upumbavukuendelea kuwa na serikali inayolala kitanda kimoja na mafisadi?

No comments: