The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 19 June 2013

Is it the beginning of the end of Museveni?






Recent revelations that Ugandan strong man Yoweri Museveni is grooming his son Major Muhoozi to take over after he leave office is a big blow. One of Museveni's inner sanctum army General David Sejusa recently took a shot at Museveni condemning his ploy to create what he called  a Political Monarchy. Sejusa who fled to Britain openly opposed Museveni attempts to clear a way for his son to take power under what Sejusa called National Project. Museveni has been in power illegally since 1986. Many think that Museveni and other dictators fail to learn from what happened recently in Libya and Egypt. Experience shows that for a dictator to pass the mantle to his child must die in power as it happened to Gnassigbe Eyadema and Omar Bongo.  Given that they are hard to learn, time has decided to remind them the right thing to do before being taught a bitter lesson. Will Museven bow to pressure wanting him to abandon his project? Will he soldier on and face the consequences? Is this the beginning of the end of Museveni dynasty and tribal regime? For more info CLICK HERE.

Sunday, 16 June 2013

Huyu Kikwete vipi utadhani waziri wa michezo na si rais!


Wengi tulipopata habari za kutokea shambulizi la kigaidi kwenye mkutano wa kampeni kule Arusha tuliumia na kulaani kitendo hiki. Pia tulidhani taifa kwa wakati huu lingepata faraja angalau kutokana na rais wao kuwahi kwenye tukio na kuonyesha mwelekeo wa taifa. Tumeshuhudia viongozi wengi wakiacha shughuli zao nyingi na kuwahi kwenye matukio kama  haya. Rais Barack Obama anaongoza kwenye umakini huu. Jamaa yetu Vasco da Gama bin Kikwete ndiyo hana habari!
Au kwa vile walioumizwa ni wapinzani? Je Kikwete anafanya madai ya CHADEMA kuwa waliowalipua ni CCM kwa woga wa kuondolewa madarakani? Je yeye ni rais wa CCM au wa mipira na kujilisha upepo kwa kuzurura kila sehemu hata bila sababu? Kwanini Kikwete amekuwa mwepesi na mpenzi wa mambo ya hovyo hata yasiyolingana na cheo chake huku akikwepa majukumu muhimu ya ofisi yake?Je ni kosa kumuita historia ya kisiasa Tanzania? Mko wapi CCM? Yuko wapi Kinana na Mangula? Uko wapi Nape na Mwigulu?
Tujirejea kwa Kikwete,  huwa haishi vituko. Yeye yuko London mkewe Marekani akipokea tuzo ya uongo na ukweli. Nilicheka sana alipopigwa picha akipokea hiyo tuzo. Wapambe wake walirekodi mkanda wa video akipokea hiyo tuzo. Ilipofika zamu ya kuongea kiingereza chake cha mimi ni Maimuna walikata picha ili wasionyeshe kihiyo huyu anavyojikanyaga na kutoa jasho debe kwa vile hajui kimombo.
Je tutaendelea kuwa na mtawala kituko hadi lini? 
Tutafakarini.

Sam Sitta Spot on Politicos Bribing Church Leaders

Dear Sam Sixx,
 Shalom Aleichem wa Assalaam Alaykum,
Jokes aside, man you've become more a cleric than a politico! Ratziti Sheteda (I want you to know). Wonder not.  I know some Hebrew and Arabic. I recently heard you rushing at word-of-God vendors in the tabernacle in Tegeta at the fundraising. You openly told them to avoid being trapped by the sin of greed and money worshiping. However, they’re already swimming in it. You said, “Please, please Christians refuse the monies obtained by means of bribery. For it is like embracing sins.” Well said.  You egged Christians to refuse from being cheaply used by corrupt politicos. How many times should they be used!
Thanks for such wisdom mkuu; however, it fell on deaf ears. Again, can a dog spare a bone really? May be, just maybe! Please never tell sippers to stop swallowing kanywaji; won’t buy it. So too, never tell the power that-be to take on corruption. How if people of cloak charged with duty to admonish rulers to stop blessing corruption and impunity are in the same bed?
Though I’m not a religious creature, the other day I was reading the Bible after finishing the Qur’an and others looking for the authorization of kanywaji. In these books of authority I like the golden rule rightly observed in as thus:  One should not behave towards others in a way which is disagreeable to oneself. This is the essence of morality. All other activities are due to selfish desire, (Hinduism. Mahabharata, Anusasana Parva 113).
Wait. Jesus said, “Take heed that ye be not deceived: for many shall come in my name, saying, I am Christ; and the time draweth near: go ye not therefore after them,” (Luke 21:8).  
Many ‘Judas Iscariot’ of Kerioth are currently vending our souls. These pillagers calling themselves humongous names such as bishop, honorouble, apostle, reverend and whatnot are in bed with thieves of public funds. Instead of shaming thieves, the ‘people of God’ enter unholy alliance with them. This has tarnished their religiosity. Are these swindlers of God or servants of their greed and stomachs? Waongo wakubwa!
 I wonder.  Why what belongs to Caesar is being given to the ‘shepherds’ instead of Caesar? Ufisadi mtupu!  Again, Jesus warned: For many shall come in my name, saying, I am Christ; and shall deceive many (Matthew 25:5). Yeah, the son of man was right. For after his death there followed many interpolations such as the bishop of Roma to become the bishop of the world and many coxed stuff so to speak. Those who remember David Yallop’s masterpiece, “In God’s Name,” will agree with us that the Holy See sank in mud after its Istituto per le Opere di Religione (IOR) was caught in bed with Banco Ambrosiano. This scam came to light after the felling of Pope John Paul II. Again, this shouldn’t be used as an excuse by those money worshipers in the name of God saying: “If the giant can do it why not us?”
Nowadays, the house of God’s become scandalous so much so that tax evaders, money launderers, prostitutes, venal politicians, business magnates, thugs, and jinxes contribute to its construction! Like ikulu, after Mchonga, all venal faces enter and congregate there without raising eyebrows! What a wicked society we've become! Sometimes, I feel like our hunk’s occupied by blind and insane creatures. How come we don’t even see such dirty money like that of Richmonduli penetrating into religions? God’s not that bankrupt and corrupt and doesn't need dirty money from filthy politicians and thieves to run ministries.
 Again, does this dirty money ‘aimed at God’ reach him or her or it is just being swindled in the name of God?  Wezi wakubwa! One bibber called such roadshows theft within theft. It is rip off everywhere. You rip paupers off and offer to God and believe you've done a right thing! What abracadabra!
Why don’t these criminals ask themselves a simple question: If these jinxes donating dirty money love God, why do they rob his or her people? How come they rob the same poor people of God and pretend to donate the loot to the ministries of God? Given that those guys are self-seekers, despite asking themselves the same question, take the money and spend it with their wives in the name of God.  Matthew saw it, He simply wrote, "So you, too, outwardly appear righteous to men, but inwardly you are full of hypocrisy and lawlessness,"(28:23I). I know. They know this verse. Given that they’re using masaburis to think, they pooh pooh everything and receive dirty money. Wealth’s become their religion swallowed hook, line, and sinker so to speak.
 We’re tired of hypocrisy. Let those bribing the temple come out of their shells and tell us how they made their money instead of pretending they can’t hear. Eddie Ewassa, why don’t you tell your colleagues to come clean on this in the first place? Roastamu Aziz, you’re the first one to offer millions to a certain church in Kinondoni. Come clean please. Do you think God is a tart who loves money so much so that when you give money can do whatever you want? Fool yourself not my friends. We know how dirtier your dosh is and how greedy, skinny and small those so-called people of God are. Like dogs, they can lick anything provided they fill their thankless stomachs. Well said Mr. Sam Six. Blessed be.
Off-the-hook cue: I heard presider Jake Kikwete saying that he won’t stop borrowing. For, debts won’t be paid in his life time. He disputed the truth that every Tanzanian owes donors Tshs. 400,000 odd. Again, he didn’t give an actual figure! Uongo mwingine bwana! Who tells lies or truth? Please don’t ask me.
Source: Thisday June 17, 2013.


Hongera Katiba Mpya "kuusuka" Muungano

Baada ya kugundua kuwa rasimu ya katiba mpya inanipa power ya kugombea urais kama mgombea binafsi, leo nawapongeza wananchi walioipendekeza na waliokusanya maoni hata kama walikuwa wanakwamua mabilioni ya njuluku.
Nampongeza jaji Jose Warioba kwa kusimama kidete na kuhakikisha anakuja na kitu ambacho kitaua muungano kistaarabu. Sijui kama jamaa zangu ambao wamekuwa wakilewa na kulalamikia muungano kama wameipata. Mlitchotaka sasa kitakuwa na tutagawana mbao baada ya kuvunja hiyo ndoa ya muungao ambayo kwa ulevi wenu mliiona kama mgongano badala ya muungano. Ila tukubaliane. Ukishavunjika sitaki nisikie vilio tena. Au vipi mkubali tuendelee kuachana taratibu kwa njia ya kuwa na sirikali tatu na marais mia kidogo. Sasa muungano umekuwa mgongano dhahiri.
Japo sipendi utitiri wa sirikali tena kwenye kaya kapuku na ombaomba kama yetu, hili la kuondosha viti vya ubunge wa kashfa rushwa na kila aina ya unyonyaji limenikuna. Huenda hiyo pesa waliyokuwa wakikusanya bila kufanya kazi yoyote ndiyo itaenda kwenye serikali tatu.
Hata hivyo, msiwe na shaka. Nikishashinda urais nitaondosha sirikali tatu na kutangaza moja tu. Atakayetaka matatizo apinge mbinu hii adhimu na takatifu ya kuwaunganisha walevi toka kwenye unafiki na kila kipande kutaka ulaji wa dezo na ujiko. Nasema wazi tena kwa kinywa kipana. Mkinichagua sahau sirikali mbili au tatu. Nitaunganisha kaya hata kwa ntutu wa bunduki. Atakayeona hili halifai basi kila mtu aende kivyake. Wao waende na Zenj yao nasi na Danganyika yetu au vipi? Kwanini kuendelea kunyimana raha bure? Kama wapo walioshiba ulaji wetu au sisi wao basi kila mmoja akale kwake ila aangalie isile kwake. Ngoja nibadili gea.
Hakuna kitu kilikuwa kinanikera kama kuwa na wabunge tena wakiitwa waheshimiwa wasiomwakilisha yeyote isipokuwa matumbo yao. Rafiki yangu Sofia Lion na Anae Andallah mnanipata siyo? Kweli imekula kwenu. Lazima hapa mtafuta kazi ama ya uhausigeli au kuuza nyanya. Hakuna kitu kimenikuna kama kuondoa upuuzi wa spika kuwa muishiwa sorry mheshimiwa tena mwenye kupendelea chata lake huku akiwaburuza waheshimiwa utadhani mjengo mali ya baba yake. Shame on her! Anna Makidamakida unapata?  Umekuwa ukiniudhi kwa kuvurunda kiasi cha kutamani siku moja nikushukie na kukupa kibano kama si kicha... we koma na ishia hapo. Hizi bangi na gongo vitakuja kunilaza lupango siku moja. Jobless Nduguy lazima uwe unalia kama kichanga kwa kunyimwa ulaji ambao ulikuwa ukiutumia kwa nyodo kana kwamba hakuna mwisho wa kila kitu chini ya jua.
 Yawezekana ni Danganyika pekee yenye wabunge watokanao na vitu vyenye kila aina ya kejeli, ubaguzi hata udhalilishaji chini ya dhana ya viti maalumu. Kwa wanavyochuma uchache bila kufanya kazi yoyote, kuna siku walevi watawaita MPigs kama ilivyotokea kule kwa Nyayo ambayo rais wake unachukua jina la nchi na kuongeza ta imetoka hiyo. Kuna mlevi husema eti waishiwa hawa huwa hawana na kazi yoyote mjengoni zaidi ya kungojea posho na sifa ndogo ndogo magazetini.  Jamani naandika kama mlevi asemavyo. Hakuna haya ya wahishimiwa kuanza kunitafuta waninyotoe roho au kunihoji kama vile niko mbele ya pilato. Mjumbe hauawi ati.
Juzi nilikuwa na maongezi na waziri mkubwa wa Ukanada ambaye aliomba nisimtaje jina ili wafisadi wasimjuejue wakati tukipata ulabu kwenye mitaa ya mji mmoja uitwao Arawa. Nilimuuliza anaonaje mfumo wa kuwa nauishimiwa wa msukule. Kwanza, alishangaa inawezekanaje mtu kwenda kwenye mjengo kuwakilisha tumbo lake!. Alisema wazi kuwa hiki nacho ni chanzo kizuri cha umaskini wa kaya. Aliongeza kuwa katika kaya yao hili haliwezekani kwa vile lazima kila mtu apambane kuupata uheshimiwa. Anasema wao wanapambanisha uwezo na si jinsia wala mitandao ya kifisadi ya kivyama kama ilivyo huko kulikoungua shoka ukabaki mpini. Nilishangaa aliposema kuwa uhishimiwa wa namna hii ni matusi ya nguoni. Hata hivyo, nilifurahi kusikia akiongea lugha ya kilevi ya kuliita kulego kulego na si kijiko kikubwa. Acha nitafsiri kwa lugha rahisi.  I call a spade a spade not a big spoon like some hypocrites who can’t tell those hishimiwas that they are screwing our hunk up. Shame on them all!
Walevi kusema ukweli hawajawahi kuona mantiki kwa mfano mtu anapochaguliwa kuwakilisha vijana kwenye mjengo huku vijana hao hao wakiishi kwnye jimbo lenye mbunge. Je huyu mbunge wa kawaida ambaye jimbo lake lina kila aina ya binadamu atawakilisha nani? Je vijana au wanawake wana nini hadi kuwa na wawakilishi zaidi ya mmoja? Hawa hawana tofauti na wale waishiwa toka Zenj wanaowakilisha majimbo yao kwenye muuganiko. Inatisha kuona kijipande cha ardhi sawa na wilaya ya Ushoto kuwa na maulaji kuliko hata mikoa. Japo huwa napenda umoja na kuunganika, nikiangalia ndoa ya sisimizi na tembo huwa uzalendo unanishinda na kusema waache wende zao na kipande chao cha ardhi wakamalizane. Sisemi hivi kwa ubaya wala ulevi.
Jamaa walituzidi akili. Baada ya kugundua kuwa tuna maulaji mengi ya kuwapa hawaachi kudai kila uchao ili tuendelee kupumbaa. Nimekumbuka kikao cha walevi juzi ambapo wengi walikandia muunganiko wakisema eti unawanyonya na kuwakosesha raha.  Hakuna ninachokumbuka kama maneno ya mgosi Machungi pale aliposema, “Ila siku wakiambaa na walevi wabara wakaamua kuwaambia kuwa kila mtu ave na kwao basi watazamisha kila kipande cha ardhi kutokana na wengi wao kuzaliana sana upande wa pili.”
 Baada ya kuona mgosi anavuka mipaka kwa kuanza lugha ya kilevi ambayo wasiopenda ukweli wanaweza kuiita ya kibaguzi, niliamua kuondoka zangu kwenda kusoma kitabu cha yule Mchungaji kidhabu Mtikisa kiitwacho Sera ya Magabacholi na Saa ya Ukombozi.  Hakuna mstari ulinichekesha kama ule usemao, “Wakituita machogo nasi twaita machokoo.”  Sikukisoma sana kutokana na lugha ya jamaa.  Inaoneka huyu jamaa alisoma volume langu la SAA YA UKOMBOZI nililotunga kuonyesha jinsi ya walevi wanavyoweza kuongoza wasiolewa kwa kuwapiga chini kwa njia ya kura ili wakose kula ya dezo kama ilivyo. Hata hivyo, tuache utani. Wazenj wanaopigapiga kelele kila uchao hasa baada ya kusikia kuwa kuna dalili ya kuwa na wese wajiandae kama tutaamua kila mtu aende kivyake baada ya mlevi kutaka kuunganisha pande la kaya na kipande cha kakaya na kutengeneza kaya moja.
Ngoja nikavute kwanza!
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 15, 2013.

Friday, 14 June 2013

Muungano: Tuache ulafi na ubinafsi tuwe na serikali moja


Hali ilivyo ni kwamba Tanzania iko msambweni kutokana na rasimu ya Katiba mpya kupendekeza ziwepo serikali tatu bila kujali mzigo anaoongezewa mlipa kodi maskini. Inashangaza kwenye nchi maskini na ombaomba kufikiri kuwa na serikali tatu. Kwa kumbukumbu yangu ni kwamba Tanganyika ilipoungana na Zanzibar na kuunda Tanzania, rais wa kwanza wa Zanzibar hayati mzee Abeid Aman Karume alitaka kuwepo serikali moja. Jambo hili lilikataliwa na rais wa kwanza wa Tanganyika hayati Mwl Julius Nyerere kwa madai kuwa ingeonekana kama Zanzibar imemezwa.
Ajabu sasa wanaoshupalia kuwapo kwa serikali tatu ni wazanzibari zaidi ya watanganyika. Kwanini imezwe Tanganyika isiwe issue ila iwe issue ikimezwa Zanzibar? Kimsingi kama ni kumezwa zinamezwa nchi zote mbili na kubakia nchi moja Tanzania.
Mie napendekeza tuungane kiukweli kwa kuwa na serikali moja na nchi moja ili kuimarisha muungano na kuwaondolea kero na mzigo wapiga kura.
Ni rahisi watu kupendekeza serikali tatu kwa sababu haziendeshiwa na pesa yao binafsi. Hata hivyo kuna gharama hapa. Kama tutapitisha serikali tatu basi pesa iliyokuwa ikiiendesha serikali ya Mapinduzi Zanzibar itumike kuendesha serikali ya Tanganyika ambayo haikuwepo kwa kitambo kirefu. Au vipi serikali mbili kila moja kwa namna yake bila kujali udogo au ukubwa zitoe pesa za kugharimia serikali ya muungano. Je hili ni rahisi? 
Kuogopa kumezwa ni woga na fikra ya kizamani. Mbona nchi ya Hawaii ambayo ni sawa na Zanzibar hailalamiki kumezwa na Marekani wala PEI  Kanada hailalamiki kumezwa?
Kuna haja ya kuepuka unafiki, ubinafsi na uchoyo na kuungana kwelikweli. Muungano ni kama ndoa ambayo huwaunganisha wawili na kuwa mwili mmoja. Muungano wa sasa ni sawa na mahusiano ya kinyumba ambapo kila mshiriki huwa na maisha yake independent of another.
Naomba kuwasilisha.

Wednesday, 12 June 2013

African must learn from Ghana’s episode

Ghana is currently embroiled in a passive tussle-cum-quandary with China after apprehending at about 100 Chinese nationals allegedly to have been involved in illegal gold mining in Ghana. Such a move irked China so as to start very vivid campaigns against Ghana. We are not aware what is what up till when the court decide otherwise. Again, looking at what transpired in Zambia prior where locals fought with Chinese and killed one a Chinese manager recently, we can comfortably say that Africa needs to be watchful of Chinese presence," Zambian Labor Minister Fackson Shamenda  was quoted by AFP as saying, "I don't know why there is always tension between
Chinese investors and workers at Collum," BBC quoted Yu Jie, spokesman for the Chinese embassy in Ghana saying that they "have cautioned all the Chinese people in Ghana to strictly abide by the related laws and regulations". Again, looking at what was reported by South African based TV ENCA saying that China and Ghana were at loggerhead one wonders why China did not repudiate such story.
Al-Jazeera had this to report, “Their number brings to 181 the total figure of Chinese that the country's immigration office has detained within the past month in this African nation.” If such a humongous number translates to one-month catch, how many are there in Ghana and Africa in general? The Guardian quoted Michael Amoako-Atta, spokesman for the Ghana immigration service as saying.  "We have arrested 168 Chinese nationals, all of whom are being detained and processed for court."  He added, "Most of these illegal miners use very dangerous substances like cyanide and mercury in processing their ore, which are not biodegradable and leach into the water bodies creating serious problems for the communities who use these sources of water as drinking water." If anything, this is a typical replica of what is currently going on in many African countries.
In Dar es Salaam, Chinese petite business persons are seen in the streets even pushing carts. They do all small and odd business poor Tanzanians do. Ironically though, Tanzania expels other suchlike green pasture seekers from neighbouring countries.
Africa was used to seeing a handful of western investors using locals to run their investment. It was used to jackals, wolves and eagles from west sent as explorers, missionaries, military attaches to their embassies and CIA agents. Now that the tiger from Asia is in the house, maybe, the elephant is in the sitting room. Africa needs to put its house in order aiming at securing and saving jobs for its sons and daughters.
Again, what west used to do is not Chinese style of doing things. China exports its people just like India does. These two are among the evolving powers of our world today. To do away from being dumping and breeding grounds for unqualified and jobless people, we need to take a leaf from western and Middle East countries which apply strict rules for investors who abuse this opportunity. Africa needs to tell china even India that what we lack is investment but not manpower.
What transpired in Ghana reminded me what happened in Tanzania recently where it was unearthed that foreign nationals working there are paid ten more times than Tanzanians with the same qualifications.
Another issue that must make African president tread carefully is the fact that China is good at producing and supplying cheap, fake and substandard items. African countries need to strengthen their bureaus of standard to see to it that such cheap and substandard merchandises are not being allowed to infiltrate their territories.
So important too is the whole issue of smuggling in ivory, wood and other products from endangered animals. Currently, China is a very hungry monster that swallows almost everything. We can’t blame the government that has always distanced itself from such conspiracy. Again, as the country benefits from whatever is brought in either legally or illegally sometimes Chinese authorities turn a blind eye and come quickly to deny wrong doing whenever their citizens are caught pant down.
In essence, what happened in Ghana is but a tip of an iceberg. Again, who is to blame? Our leaders have put forth their personal interests at the expense of their citizenry. Though not all, myopic and greedy as they are, if nothing is done; we will soon see the floods of Chinese. This means, the so-called investment will end up becoming another catastrophe just like the one we've been going through under western investment relationship.
Having such aliens that can illegally involve themselves in mining, smuggling and capital flight, Africa stands to lose once again. Essentially, if Africa wants to benefit and prosper from the coming of China, it must see to it that labour and immigration laws are updated to foil such incidents. Without arresting all loopholes allowing aliens to plunder Africa, chances are that we will soon evidence chaos resulting from fighting between locals and those aliens. And indeed, this will be misinterpreted into xenophobia which is not good for our relations. It is better to take measures before the situation worsens and gets out of control. Suffice it to say; what transpired in Ghana should act as eye opener for all African countries.
Source: The African Executive Magazine June 12,2013.

Tuesday, 11 June 2013

Makinda na Ndugai wanaonyesha udhaifu wao


KWA wafuatiliaji wa mitafaruku, ombwe na uongozi mbovu wa Bunge letu, watakubaliana nami kuwa kile kinachosemwa kuhusu kupwaya kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda   na Naibu wake Job Ndugai kunazidi kujidhihiri haraka sana na mara nyingi.
Matukio ya hivi karibuni ya baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuligeuza Bunge kuwa uwanja wa matusi yamewavua nguo wawili hawa ambao uongozi wao umeonyesha wazi ulivyo hatari kwa taifa letu.
Wawili hawa wamethibitisha wasivyojua demokrasia wala mipaka ya uongozi wao, ukiachilia mbali utawala wa sheria na uwajibikaji.
Haiingii akilini mbunge anaamka na kuwatukana wenzake matusi mazito kama ‘f**k you’ na spika hamchukulii hatua. Ajabu, Spika huyu huyu amekuwa hodari wa kuwanyamazisha, kuwaburuza hata kuwasimamisha vikao wabunge wa upinzani kama ilivyotokea hivi karibuni ambapo wabunge watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walifukuzwa bungeni bila sababu za msingi kisheria na kibunge.
Spika wa Bunge na Naibu wake licha ya kuonyesha udhaifu mwingi, wameonyesha upendeleo wa wazi. Wameonyesha wanavyotumikia serikali ya CCM zaidi ya wananchi waliowachagua. Unapofumkuza mbunge au kumsimamisha kuhudhuria vikao, unakuwa umewafukuza na kuwanyima haki wale waliomchagua awawakilishe.
Ukiachia mbali upendeleo, spika na naibu wake wameonyesha wazi walivyo kwenye madaraka kutumikia makundi fulani tofauti na dhana nzima ya kuutumikia umma wa Watanzania bila upendeleo wala uonevu.
Nilishangaa niliposikia Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA) alipopinga kutengwa shilingi bilioni 29 kwa idara mpya ambayo rais anataka kuianzisha eti kufuatilia utekelezaji wa miradi wakati wizara na idara husika zipo.
Mdee aliposema kuwa hili ni chaka la ulaji, spika alikuja juu na kutaka afute kauli yake hata bila kumpa nafasi ya kumaliza hoja yake wala kutoa maelezo.
Lakini Mbunge wa Kigoma Mjini Peter Serukamba alipomwambia mwenzake ‘come on f**k you’ spika alinyamaza kana kwamba hili ni tusi dogo!
Kimsingi, Serukamba alitukana Watanzania wote akiwamo spika, ingawa spika hakuliona hili. Unaposimama bungeni na kurusha matusi unawalenga wenye Bunge ambao ni Watanzania wote.
Kama kulikuwa na fursa ya spika na naibu wake kuonyesha uongozi uliotukuka na siyo uliochafuka kama sasa, ilikuwa ni kwenye kipindi hiki cha kugeuzwa Bunge kuwa uwanja wa matusi bila sababu.
Bahati mbaya wawili hawa waliacha nafasi hii ikapita bila kuitumia kuonyesha ukomavu na uwajibikaji wao kwa wananchi.
Kadhia nyingine kati ya nyingi iliyoonyesha wazi upendeleo wa wawili hawa, ni pale mbunge wa viti maalumu, Christina Mughwai alipougua na ukatolewa ushauri na madaktari apelekwe India kwa matibabu zaidi. Hadi tunaandika Mughwai hajapelekwa India. Badala yake, kwa mujibu wa mdogo wake Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), familia ndiyo inahangaika kumpeleka Mughway baada ya Bunge kuwa linawapiga danadana kana kwamba kumpeleka mbunge huyu India ni hisani na si haki yake.
Lissu amekaririwa hivi karibuni akitoa kauli ya kukata tamaa. Alisema; “Walimshauri akasubirie nyumbani, ingawa hali yake sio nzuri.” Kwanini asuburi nyumbani kana kwamba huko ndiko kuna matibabu. Ni unyama kiasi gani kushindwa kutambua kuwa ugonjwa hausubiri ukiachia mbali mateso anayopata?
Je, Mughway angekuwa mbunge wa CCM wangengoja hivyo na kumshauri bila kufikiri kuwa akasubiri nyumbani? Mbona kwenye kulipana posho za vikao hawasubiri bali kukatiana papo kwa papo? Inakuwaje serikali inapata pesa haraka ya kushughulikia mambo mengine yasiyo muhimu kuliko pesa ya kuokoa uhai wa mbunge?
Si uzushi. Makinda na Ndugai wameshusha uwajibikaji na hadhi ya Bunge kwa kiwango kikubwa. Wamekuwa waanzilishi wa fujo kwa wakati tofauti bila hata kujifunza wala kujirekebisha. Mchezo wa kufukuza wabunge toka kwenye vikao umekuwa ndiyo alama ya Makinda.
Makinda ni spika atakayeingia kwenye historia ya nchi yetu kama spika muonevu na mbabe kuliko waliomtangulia. Imefikia mahali watu wanajiuliza: Makinda anawajibika kwa nani? Je, anafanya yote haya kumridhisha nani? Je, matendo ya Makinda na naibu yake yanaendena na masharti ya nafasi zao ambayo mojawapo ni kutokuwa na ushabiki wa kisiasa? Je, wabunge wataendelea kunyanyaswa na kushikwa mateka na watu hawa wawili hadi lini?
Kwa vile Bunge halina utaratibu wa maana na wa haki wa kumuondoa spika pale anapoonyesha kukosa sifa kama ilivyo kwa Makinda kutokana na chama chake kuwa na wabunge wengi, wabunge wanaoathirika wanapaswa kwenda majimboni mwao na kumshitakia kwa wananchi ili uchaguzi ujao wakiadhibu chama chake kutokana na kazi mbaya ya kada wake.
Ingawa CCM wanaweza kuona anachofanya Makinda ni kuwasaidia, kimsingi, kama wataangalia mbali, anaizika CCM taratibu. Kama wabunge watasimama na kutafsiri na kuelezea aina ya mateso na manyanyaso wanayopata kutoka kwa Makinda na naibu wake, uwezekano wa CCM kuathirika kwenye uchaguzi ujao ni mkubwa.
Maana unapomfukuza mbunge unamnyima fursa ya kuwatetea watu wake. Ni bahati nzuri kuwa si wabunge wote wa CCM wanakubaliana na madudu anayotenda spika na naibu wake. Hawa wakipewa motisha wanaweza kuleta mageuzi ya kweli ndani ya taasisi hii adhimu.
Ni vizuri wabunge wa CCM wakaelewa kuwa anachofanya Makinda kitawaathiri mbele ya safari. Ni vigumu kwao kuona madhara ya uongozi mbovu wa Makinda. Ila wafahamu kuwa kutokana na kuenea kwa mawasiliano na upashanaji wa habari, madudu ya Makinda yanajulikana kwa wananchi. Haiwezekani wananchi hata wapenzi wa CCM washuhudie hoja zinazolenga kuokoa pesa yao zinazimwa eti kwa vile zimeletwa na wabunge wa upinzani.
Watanzania wanajua machungu ya umaskini unaosababishwa na mfumo mbovu wa utawala ulioshindwa kusimamia kodi na rasilimali zao. Wanasikia madudu yote yanayoibuliwa na wakaguzi wa hesabu za seirikali kila mwaka ambayo ni chanzo cha umaskini wao. Watafikia mahali watachoka na hapa ndipo uhovyo wa Makinda utaitafuna CCM.
Tuombe Mungu Makinda na Ndugai waendelee kuonyesha udhaifu wao ili wananchi wautumie kuwaadhibu wao na chama chao.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 11, 2013.