The Curse for Salvation
Wednesday, 19 June 2013
Is it the beginning of the end of Museveni?
Sunday, 16 June 2013
Huyu Kikwete vipi utadhani waziri wa michezo na si rais!
.jpg)
Wengi tulipopata habari za kutokea shambulizi la kigaidi kwenye mkutano wa kampeni kule Arusha tuliumia na kulaani kitendo hiki. Pia tulidhani taifa kwa wakati huu lingepata faraja angalau kutokana na rais wao kuwahi kwenye tukio na kuonyesha mwelekeo wa taifa. Tumeshuhudia viongozi wengi wakiacha shughuli zao nyingi na kuwahi kwenye matukio kama haya. Rais Barack Obama anaongoza kwenye umakini huu. Jamaa yetu Vasco da Gama bin Kikwete ndiyo hana habari!
Au kwa vile walioumizwa ni wapinzani? Je Kikwete anafanya madai ya CHADEMA kuwa waliowalipua ni CCM kwa woga wa kuondolewa madarakani? Je yeye ni rais wa CCM au wa mipira na kujilisha upepo kwa kuzurura kila sehemu hata bila sababu? Kwanini Kikwete amekuwa mwepesi na mpenzi wa mambo ya hovyo hata yasiyolingana na cheo chake huku akikwepa majukumu muhimu ya ofisi yake?Je ni kosa kumuita historia ya kisiasa Tanzania? Mko wapi CCM? Yuko wapi Kinana na Mangula? Uko wapi Nape na Mwigulu?
Tujirejea kwa Kikwete, huwa haishi vituko. Yeye yuko London mkewe Marekani akipokea tuzo ya uongo na ukweli. Nilicheka sana alipopigwa picha akipokea hiyo tuzo. Wapambe wake walirekodi mkanda wa video akipokea hiyo tuzo. Ilipofika zamu ya kuongea kiingereza chake cha mimi ni Maimuna walikata picha ili wasionyeshe kihiyo huyu anavyojikanyaga na kutoa jasho debe kwa vile hajui kimombo.
Je tutaendelea kuwa na mtawala kituko hadi lini?
Tutafakarini.
Sam Sitta Spot on Politicos Bribing Church Leaders
Shalom
Aleichem wa Assalaam Alaykum,
Jokes aside,
man you've become more a cleric than a politico! Ratziti Sheteda
(I want you to know). Wonder not. I know some Hebrew and Arabic. I
recently heard you rushing at word-of-God vendors in the tabernacle in Tegeta at
the fundraising. You openly told them to avoid being trapped by the sin of greed
and money worshiping. However, they’re already swimming in it. You said,
“Please, please Christians refuse the monies obtained by means of bribery. For
it is like embracing sins.”
Well said. You egged Christians to
refuse from being cheaply used by corrupt politicos. How many times should they
be used!
Thanks for such
wisdom mkuu; however, it fell on deaf ears. Again, can a dog spare a bone
really? May be, just maybe! Please never tell sippers to stop swallowing
kanywaji; won’t buy it. So too, never tell the power that-be to take on
corruption. How if people of cloak charged with duty to admonish rulers to stop
blessing corruption and impunity are in the same bed?
Though I’m not
a religious creature, the other day I was reading the Bible after finishing the
Qur’an and others looking for the authorization of kanywaji. In these books of
authority I like the golden rule rightly observed in as thus: One
should not behave towards others in a way which is disagreeable to oneself. This
is the essence of morality. All other activities are due to selfish desire,
(Hinduism. Mahabharata, Anusasana Parva 113).
Wait. Jesus
said, “Take heed that ye be not deceived: for many shall come in my name,
saying, I am Christ; and the time draweth near: go ye not therefore after them,”
(Luke 21:8).
Many ‘Judas
Iscariot’ of Kerioth are currently vending our souls. These pillagers calling
themselves humongous names such as bishop, honorouble, apostle, reverend and
whatnot are in bed with thieves of public funds. Instead of shaming thieves, the
‘people of God’ enter unholy alliance with them. This has tarnished their
religiosity. Are these swindlers of God or servants of their greed and stomachs?
Waongo wakubwa!
I
wonder. Why what belongs to Caesar is being given to the
‘shepherds’ instead of Caesar? Ufisadi mtupu! Again, Jesus warned:
For many shall come in my name, saying, I am Christ; and shall deceive many
(Matthew 25:5). Yeah, the son of man was right. For after his death there
followed many interpolations such as the bishop of Roma to become the bishop of
the world and many coxed stuff so to speak. Those who remember David Yallop’s
masterpiece, “In God’s Name,” will agree with us that the Holy See sank in mud
after its Istituto per le Opere di Religione (IOR) was caught in bed with Banco
Ambrosiano. This scam came to light after the felling of Pope John Paul II.
Again, this shouldn’t be used as an excuse by those money worshipers in the
name of God saying: “If the giant can do it why not us?”
Nowadays, the
house of God’s become scandalous so much so that tax evaders, money launderers,
prostitutes, venal politicians, business magnates, thugs, and jinxes contribute
to its construction! Like ikulu, after Mchonga, all venal faces enter and
congregate there without raising eyebrows! What a wicked society we've become!
Sometimes, I feel like our hunk’s occupied by blind and insane creatures. How
come we don’t even see such dirty money like that of Richmonduli penetrating
into religions? God’s not that bankrupt and corrupt and doesn't need dirty money
from filthy politicians and thieves to run ministries.
Again,
does this dirty money ‘aimed at God’ reach him or her or it is just being
swindled in the name of God? Wezi wakubwa! One bibber called such
roadshows theft within theft. It is rip off everywhere. You rip paupers off and
offer to God and believe you've done a right thing! What abracadabra!
Why don’t these
criminals ask themselves a simple question: If these jinxes donating dirty money
love God, why do they rob his or her people? How come they rob the same poor
people of God and pretend to donate the loot to the ministries of God? Given
that those guys are self-seekers, despite asking themselves the same question,
take the money and spend it with their wives in the name of God.
Matthew saw it, He simply wrote, "So you, too,
outwardly appear righteous to men, but inwardly you are full of hypocrisy and
lawlessness,"(28:23I). I know. They know this verse. Given that they’re using
masaburis to think, they pooh pooh everything and receive dirty money. Wealth’s
become their religion swallowed hook, line, and sinker so to speak.
We’re
tired of hypocrisy. Let those bribing the temple come out of their shells and
tell us how they made their money instead of pretending they can’t hear. Eddie
Ewassa, why don’t you tell your colleagues to come clean on this in the first
place? Roastamu Aziz, you’re the first one to offer millions to a certain church
in Kinondoni. Come clean please. Do you think God is a tart who loves money so
much so that when you give money can do whatever you want? Fool yourself not my
friends. We know how dirtier your dosh is and how greedy, skinny and small those
so-called people of God are. Like dogs, they can lick anything provided they
fill their thankless stomachs. Well said Mr. Sam Six. Blessed be.
Off-the-hook
cue: I heard presider Jake Kikwete saying that he won’t stop borrowing. For,
debts won’t be paid in his life time. He disputed the truth that every Tanzanian
owes donors Tshs. 400,000 odd. Again, he didn’t give an actual figure! Uongo
mwingine bwana! Who tells lies or truth? Please don’t ask me.
Source: Thisday June 17, 2013.
Source: Thisday June 17, 2013.
Hongera Katiba Mpya "kuusuka" Muungano

Baada ya
kugundua kuwa rasimu ya katiba mpya inanipa power ya kugombea urais kama mgombea
binafsi, leo nawapongeza wananchi walioipendekeza na waliokusanya maoni hata
kama walikuwa wanakwamua mabilioni ya njuluku.
Nampongeza jaji
Jose Warioba kwa kusimama kidete na kuhakikisha anakuja na kitu ambacho kitaua
muungano kistaarabu. Sijui kama jamaa zangu ambao wamekuwa wakilewa na
kulalamikia muungano kama wameipata. Mlitchotaka sasa kitakuwa na tutagawana
mbao baada ya kuvunja hiyo ndoa ya muungao ambayo kwa ulevi wenu mliiona kama
mgongano badala ya muungano. Ila tukubaliane. Ukishavunjika sitaki nisikie vilio
tena. Au vipi mkubali tuendelee kuachana taratibu kwa njia ya kuwa na sirikali
tatu na marais mia kidogo. Sasa muungano umekuwa mgongano dhahiri.
Japo sipendi
utitiri wa sirikali tena kwenye kaya kapuku na ombaomba kama yetu, hili la
kuondosha viti vya ubunge wa kashfa rushwa na kila aina ya unyonyaji limenikuna.
Huenda hiyo pesa waliyokuwa wakikusanya bila kufanya kazi yoyote ndiyo itaenda
kwenye serikali tatu.
Hata hivyo,
msiwe na shaka. Nikishashinda urais nitaondosha sirikali tatu na kutangaza moja
tu. Atakayetaka matatizo apinge mbinu hii adhimu na takatifu ya kuwaunganisha
walevi toka kwenye unafiki na kila kipande kutaka ulaji wa dezo na ujiko. Nasema
wazi tena kwa kinywa kipana. Mkinichagua sahau sirikali mbili au tatu.
Nitaunganisha kaya hata kwa ntutu wa bunduki. Atakayeona hili halifai basi kila
mtu aende kivyake. Wao waende na Zenj yao nasi na Danganyika yetu au vipi?
Kwanini kuendelea kunyimana raha bure? Kama wapo walioshiba ulaji wetu au sisi
wao basi kila mmoja akale kwake ila aangalie isile kwake. Ngoja nibadili
gea.
Hakuna kitu
kilikuwa kinanikera kama kuwa na wabunge tena wakiitwa waheshimiwa
wasiomwakilisha yeyote isipokuwa matumbo yao. Rafiki yangu Sofia Lion na Anae
Andallah mnanipata siyo? Kweli imekula kwenu. Lazima hapa mtafuta kazi ama ya
uhausigeli au kuuza nyanya. Hakuna kitu kimenikuna kama kuondoa upuuzi wa spika
kuwa muishiwa sorry mheshimiwa tena mwenye kupendelea chata lake huku
akiwaburuza waheshimiwa utadhani mjengo mali ya baba yake. Shame on her! Anna
Makidamakida unapata? Umekuwa ukiniudhi kwa kuvurunda kiasi cha
kutamani siku moja nikushukie na kukupa kibano kama si kicha... we koma na ishia
hapo. Hizi bangi na gongo vitakuja kunilaza lupango siku moja. Jobless Nduguy
lazima uwe unalia kama kichanga kwa kunyimwa ulaji ambao ulikuwa ukiutumia kwa
nyodo kana kwamba hakuna mwisho wa kila kitu chini ya jua.
Yawezekana
ni Danganyika pekee yenye wabunge watokanao na vitu vyenye kila aina ya kejeli,
ubaguzi hata udhalilishaji chini ya dhana ya viti maalumu. Kwa wanavyochuma
uchache bila kufanya kazi yoyote, kuna siku walevi watawaita MPigs kama
ilivyotokea kule kwa Nyayo ambayo rais wake unachukua jina la nchi na kuongeza
ta imetoka hiyo. Kuna mlevi husema eti waishiwa hawa huwa hawana na kazi yoyote
mjengoni zaidi ya kungojea posho na sifa ndogo ndogo magazetini.
Jamani naandika kama mlevi asemavyo. Hakuna haya ya wahishimiwa kuanza
kunitafuta waninyotoe roho au kunihoji kama vile niko mbele ya pilato. Mjumbe
hauawi ati.
Juzi nilikuwa
na maongezi na waziri mkubwa wa Ukanada ambaye aliomba nisimtaje jina ili
wafisadi wasimjuejue wakati tukipata ulabu kwenye mitaa ya mji mmoja uitwao
Arawa. Nilimuuliza anaonaje mfumo wa kuwa nauishimiwa wa msukule. Kwanza,
alishangaa inawezekanaje mtu kwenda kwenye mjengo kuwakilisha tumbo lake!.
Alisema wazi kuwa hiki nacho ni chanzo kizuri cha umaskini wa kaya. Aliongeza
kuwa katika kaya yao hili haliwezekani kwa vile lazima kila mtu apambane kuupata
uheshimiwa. Anasema wao wanapambanisha uwezo na si jinsia wala mitandao ya
kifisadi ya kivyama kama ilivyo huko kulikoungua shoka ukabaki mpini.
Nilishangaa aliposema kuwa uhishimiwa wa namna hii ni matusi ya nguoni. Hata
hivyo, nilifurahi kusikia akiongea lugha ya kilevi ya kuliita kulego kulego na
si kijiko kikubwa. Acha nitafsiri kwa lugha rahisi. I call a spade
a spade not a big spoon like some hypocrites who can’t tell those hishimiwas
that they are screwing our hunk up. Shame on them all!
Walevi kusema
ukweli hawajawahi kuona mantiki kwa mfano mtu anapochaguliwa kuwakilisha vijana
kwenye mjengo huku vijana hao hao wakiishi kwnye jimbo lenye mbunge. Je huyu
mbunge wa kawaida ambaye jimbo lake lina kila aina ya binadamu atawakilisha
nani? Je vijana au wanawake wana nini hadi kuwa na wawakilishi zaidi ya mmoja?
Hawa hawana tofauti na wale waishiwa toka Zenj wanaowakilisha majimbo yao kwenye
muuganiko. Inatisha kuona kijipande cha ardhi sawa na wilaya ya Ushoto kuwa na
maulaji kuliko hata mikoa. Japo huwa napenda umoja na kuunganika, nikiangalia
ndoa ya sisimizi na tembo huwa uzalendo unanishinda na kusema waache wende zao
na kipande chao cha ardhi wakamalizane. Sisemi hivi kwa ubaya wala ulevi.
Jamaa
walituzidi akili. Baada ya kugundua kuwa tuna maulaji mengi ya kuwapa hawaachi
kudai kila uchao ili tuendelee kupumbaa. Nimekumbuka kikao cha walevi juzi
ambapo wengi walikandia muunganiko wakisema eti unawanyonya na kuwakosesha
raha. Hakuna ninachokumbuka kama maneno ya mgosi Machungi pale
aliposema, “Ila siku wakiambaa na walevi wabara wakaamua kuwaambia kuwa kila mtu
ave na kwao basi watazamisha kila kipande cha ardhi kutokana na wengi wao
kuzaliana sana upande wa pili.”
Baada
ya kuona mgosi anavuka mipaka kwa kuanza lugha ya kilevi ambayo wasiopenda
ukweli wanaweza kuiita ya kibaguzi, niliamua kuondoka zangu kwenda kusoma kitabu
cha yule Mchungaji kidhabu Mtikisa kiitwacho Sera ya Magabacholi na Saa ya
Ukombozi. Hakuna mstari ulinichekesha kama ule usemao, “Wakituita
machogo nasi twaita machokoo.” Sikukisoma sana kutokana na lugha
ya jamaa. Inaoneka huyu jamaa alisoma volume langu la SAA YA
UKOMBOZI nililotunga kuonyesha jinsi ya walevi wanavyoweza kuongoza wasiolewa
kwa kuwapiga chini kwa njia ya kura ili wakose kula ya dezo kama ilivyo. Hata
hivyo, tuache utani. Wazenj wanaopigapiga kelele kila uchao hasa baada ya
kusikia kuwa kuna dalili ya kuwa na wese wajiandae kama tutaamua kila mtu aende
kivyake baada ya mlevi kutaka kuunganisha pande la kaya na kipande cha kakaya na
kutengeneza kaya moja.
Ngoja nikavute
kwanza!
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 15, 2013.
Friday, 14 June 2013
Muungano: Tuache ulafi na ubinafsi tuwe na serikali moja

Hali ilivyo ni kwamba Tanzania iko msambweni kutokana na rasimu ya Katiba mpya kupendekeza ziwepo serikali tatu bila kujali mzigo anaoongezewa mlipa kodi maskini. Inashangaza kwenye nchi maskini na ombaomba kufikiri kuwa na serikali tatu. Kwa kumbukumbu yangu ni kwamba Tanganyika ilipoungana na Zanzibar na kuunda Tanzania, rais wa kwanza wa Zanzibar hayati mzee Abeid Aman Karume alitaka kuwepo serikali moja. Jambo hili lilikataliwa na rais wa kwanza wa Tanganyika hayati Mwl Julius Nyerere kwa madai kuwa ingeonekana kama Zanzibar imemezwa.
Ajabu sasa wanaoshupalia kuwapo kwa serikali tatu ni wazanzibari zaidi ya watanganyika. Kwanini imezwe Tanganyika isiwe issue ila iwe issue ikimezwa Zanzibar? Kimsingi kama ni kumezwa zinamezwa nchi zote mbili na kubakia nchi moja Tanzania.
Mie napendekeza tuungane kiukweli kwa kuwa na serikali moja na nchi moja ili kuimarisha muungano na kuwaondolea kero na mzigo wapiga kura.
Ni rahisi watu kupendekeza serikali tatu kwa sababu haziendeshiwa na pesa yao binafsi. Hata hivyo kuna gharama hapa. Kama tutapitisha serikali tatu basi pesa iliyokuwa ikiiendesha serikali ya Mapinduzi Zanzibar itumike kuendesha serikali ya Tanganyika ambayo haikuwepo kwa kitambo kirefu. Au vipi serikali mbili kila moja kwa namna yake bila kujali udogo au ukubwa zitoe pesa za kugharimia serikali ya muungano. Je hili ni rahisi?
Kuogopa kumezwa ni woga na fikra ya kizamani. Mbona nchi ya Hawaii ambayo ni sawa na Zanzibar hailalamiki kumezwa na Marekani wala PEI Kanada hailalamiki kumezwa?
Kuna haja ya kuepuka unafiki, ubinafsi na uchoyo na kuungana kwelikweli. Muungano ni kama ndoa ambayo huwaunganisha wawili na kuwa mwili mmoja. Muungano wa sasa ni sawa na mahusiano ya kinyumba ambapo kila mshiriki huwa na maisha yake independent of another.
Naomba kuwasilisha.
Wednesday, 12 June 2013
African must learn from Ghana’s episode
Ghana is
currently embroiled in a passive tussle-cum-quandary with China after
apprehending at about 100 Chinese nationals allegedly to have been involved in
illegal gold mining in Ghana. Such a move irked China so as to start very vivid
campaigns against Ghana. We are not aware what is what up till when the court
decide otherwise. Again, looking at what transpired in Zambia prior where locals
fought with Chinese and killed one a Chinese manager recently, we can
comfortably say that Africa needs to be watchful of Chinese presence," Zambian
Labor Minister Fackson Shamenda was quoted by AFP as saying, "I don't know why
there is always tension between
Chinese
investors and workers at Collum," BBC quoted Yu
Jie, spokesman for the Chinese embassy in Ghana saying that they "have cautioned
all the Chinese people in Ghana to strictly abide by the related laws and
regulations". Again, looking at what was reported by South African based TV ENCA
saying that China and Ghana were at loggerhead one wonders why China did not
repudiate such story.
Al-Jazeera had
this to report, “Their number
brings to 181 the total figure of Chinese that the country's immigration office
has detained within the past month in this African nation.” If such a humongous
number translates to one-month catch, how many are there in Ghana and Africa in
general? The Guardian quoted Michael Amoako-Atta, spokesman for the Ghana
immigration service as saying. "We have arrested 168 Chinese
nationals, all of whom are being detained and processed for court."
He added, "Most of these
illegal miners use very dangerous substances like cyanide and mercury in
processing their ore, which are not biodegradable and leach into the water
bodies creating serious problems for the communities who use these sources of
water as drinking water." If anything, this is a typical replica of what is
currently going on in many African countries.
In Dar es
Salaam, Chinese petite business persons are seen in the streets even pushing
carts. They do all small and odd business poor Tanzanians do. Ironically though,
Tanzania expels other suchlike green pasture seekers from neighbouring
countries.
Africa was used
to seeing a handful of western investors using locals to run their investment.
It was used to jackals, wolves and eagles from west sent as explorers,
missionaries, military attaches to their embassies and CIA agents. Now that the
tiger from Asia is in the house, maybe, the elephant is in the sitting room.
Africa needs to put its house in order aiming at securing and saving jobs for
its sons and daughters.
Again, what
west used to do is not Chinese style of doing things. China exports its people
just like India does. These two are among the evolving powers of our world
today. To do away from being dumping and breeding grounds for unqualified and
jobless people, we need to take a leaf from western and Middle East countries
which apply strict rules for investors who abuse this opportunity. Africa needs
to tell china even India that what we lack is investment but not
manpower.
What transpired
in Ghana reminded me what happened in Tanzania recently where it was unearthed
that foreign nationals working there are paid ten more times than Tanzanians
with the same qualifications.
Another issue
that must make African president tread carefully is the fact that China is good
at producing and supplying cheap, fake and substandard items. African countries
need to strengthen their bureaus of standard to see to it that such cheap and
substandard merchandises are not being allowed to infiltrate their
territories.
So important
too is the whole issue of smuggling in ivory, wood and other products from
endangered animals. Currently, China is a very hungry monster that swallows
almost everything. We can’t blame the government that has always distanced
itself from such conspiracy. Again, as the country benefits from whatever is
brought in either legally or illegally sometimes Chinese authorities turn a
blind eye and come quickly to deny wrong doing whenever their citizens are
caught pant down.
In essence,
what happened in Ghana is but a tip of an iceberg. Again, who is to blame? Our
leaders have put forth their personal interests at the expense of their
citizenry. Though not all, myopic and greedy as they are, if nothing is done; we
will soon see the floods of Chinese. This means, the so-called investment will
end up becoming another catastrophe just like the one we've been going through
under western investment relationship.
Having such
aliens that can illegally involve themselves in mining, smuggling and capital
flight, Africa stands to lose once again. Essentially, if Africa wants to
benefit and prosper from the coming of China, it must see to it that labour and
immigration laws are updated to foil such incidents. Without arresting all
loopholes allowing aliens to plunder Africa, chances are that we will soon
evidence chaos resulting from fighting between locals and those aliens. And
indeed, this will be misinterpreted into xenophobia which is not good for our
relations. It is better to take measures before the situation worsens and gets
out of control. Suffice it to say; what transpired in Ghana should act as eye
opener for all African countries.
Source: The African Executive Magazine June 12,2013.
Tuesday, 11 June 2013
Makinda na Ndugai wanaonyesha udhaifu wao
KWA wafuatiliaji wa mitafaruku, ombwe na uongozi mbovu wa Bunge letu, watakubaliana nami kuwa kile kinachosemwa kuhusu kupwaya kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai kunazidi kujidhihiri haraka sana na mara nyingi.
Matukio ya hivi karibuni ya baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuligeuza Bunge kuwa uwanja wa matusi yamewavua nguo wawili hawa ambao uongozi wao umeonyesha wazi ulivyo hatari kwa taifa letu.
Wawili hawa wamethibitisha wasivyojua demokrasia wala mipaka ya uongozi wao, ukiachilia mbali utawala wa sheria na uwajibikaji.
Haiingii akilini mbunge anaamka na kuwatukana wenzake matusi mazito kama ‘f**k you’ na spika hamchukulii hatua. Ajabu, Spika huyu huyu amekuwa hodari wa kuwanyamazisha, kuwaburuza hata kuwasimamisha vikao wabunge wa upinzani kama ilivyotokea hivi karibuni ambapo wabunge watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walifukuzwa bungeni bila sababu za msingi kisheria na kibunge.
Spika wa Bunge na Naibu wake licha ya kuonyesha udhaifu mwingi, wameonyesha upendeleo wa wazi. Wameonyesha wanavyotumikia serikali ya CCM zaidi ya wananchi waliowachagua. Unapofumkuza mbunge au kumsimamisha kuhudhuria vikao, unakuwa umewafukuza na kuwanyima haki wale waliomchagua awawakilishe.
Ukiachia mbali upendeleo, spika na naibu wake wameonyesha wazi walivyo kwenye madaraka kutumikia makundi fulani tofauti na dhana nzima ya kuutumikia umma wa Watanzania bila upendeleo wala uonevu.
Nilishangaa niliposikia Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA) alipopinga kutengwa shilingi bilioni 29 kwa idara mpya ambayo rais anataka kuianzisha eti kufuatilia utekelezaji wa miradi wakati wizara na idara husika zipo.
Mdee aliposema kuwa hili ni chaka la ulaji, spika alikuja juu na kutaka afute kauli yake hata bila kumpa nafasi ya kumaliza hoja yake wala kutoa maelezo.
Lakini Mbunge wa Kigoma Mjini Peter Serukamba alipomwambia mwenzake ‘come on f**k you’ spika alinyamaza kana kwamba hili ni tusi dogo!
Kimsingi, Serukamba alitukana Watanzania wote akiwamo spika, ingawa spika hakuliona hili. Unaposimama bungeni na kurusha matusi unawalenga wenye Bunge ambao ni Watanzania wote.
Kama kulikuwa na fursa ya spika na naibu wake kuonyesha uongozi uliotukuka na siyo uliochafuka kama sasa, ilikuwa ni kwenye kipindi hiki cha kugeuzwa Bunge kuwa uwanja wa matusi bila sababu.
Bahati mbaya wawili hawa waliacha nafasi hii ikapita bila kuitumia kuonyesha ukomavu na uwajibikaji wao kwa wananchi.
Kadhia nyingine kati ya nyingi iliyoonyesha wazi upendeleo wa wawili hawa, ni pale mbunge wa viti maalumu, Christina Mughwai alipougua na ukatolewa ushauri na madaktari apelekwe India kwa matibabu zaidi. Hadi tunaandika Mughwai hajapelekwa India. Badala yake, kwa mujibu wa mdogo wake Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), familia ndiyo inahangaika kumpeleka Mughway baada ya Bunge kuwa linawapiga danadana kana kwamba kumpeleka mbunge huyu India ni hisani na si haki yake.
Lissu amekaririwa hivi karibuni akitoa kauli ya kukata tamaa. Alisema; “Walimshauri akasubirie nyumbani, ingawa hali yake sio nzuri.” Kwanini asuburi nyumbani kana kwamba huko ndiko kuna matibabu. Ni unyama kiasi gani kushindwa kutambua kuwa ugonjwa hausubiri ukiachia mbali mateso anayopata?
Je, Mughway angekuwa mbunge wa CCM wangengoja hivyo na kumshauri bila kufikiri kuwa akasubiri nyumbani? Mbona kwenye kulipana posho za vikao hawasubiri bali kukatiana papo kwa papo? Inakuwaje serikali inapata pesa haraka ya kushughulikia mambo mengine yasiyo muhimu kuliko pesa ya kuokoa uhai wa mbunge?
Si uzushi. Makinda na Ndugai wameshusha uwajibikaji na hadhi ya Bunge kwa kiwango kikubwa. Wamekuwa waanzilishi wa fujo kwa wakati tofauti bila hata kujifunza wala kujirekebisha. Mchezo wa kufukuza wabunge toka kwenye vikao umekuwa ndiyo alama ya Makinda.
Makinda ni spika atakayeingia kwenye historia ya nchi yetu kama spika muonevu na mbabe kuliko waliomtangulia. Imefikia mahali watu wanajiuliza: Makinda anawajibika kwa nani? Je, anafanya yote haya kumridhisha nani? Je, matendo ya Makinda na naibu yake yanaendena na masharti ya nafasi zao ambayo mojawapo ni kutokuwa na ushabiki wa kisiasa? Je, wabunge wataendelea kunyanyaswa na kushikwa mateka na watu hawa wawili hadi lini?
Kwa vile Bunge halina utaratibu wa maana na wa haki wa kumuondoa spika pale anapoonyesha kukosa sifa kama ilivyo kwa Makinda kutokana na chama chake kuwa na wabunge wengi, wabunge wanaoathirika wanapaswa kwenda majimboni mwao na kumshitakia kwa wananchi ili uchaguzi ujao wakiadhibu chama chake kutokana na kazi mbaya ya kada wake.
Ingawa CCM wanaweza kuona anachofanya Makinda ni kuwasaidia, kimsingi, kama wataangalia mbali, anaizika CCM taratibu. Kama wabunge watasimama na kutafsiri na kuelezea aina ya mateso na manyanyaso wanayopata kutoka kwa Makinda na naibu wake, uwezekano wa CCM kuathirika kwenye uchaguzi ujao ni mkubwa.
Maana unapomfukuza mbunge unamnyima fursa ya kuwatetea watu wake. Ni bahati nzuri kuwa si wabunge wote wa CCM wanakubaliana na madudu anayotenda spika na naibu wake. Hawa wakipewa motisha wanaweza kuleta mageuzi ya kweli ndani ya taasisi hii adhimu.
Ni vizuri wabunge wa CCM wakaelewa kuwa anachofanya Makinda kitawaathiri mbele ya safari. Ni vigumu kwao kuona madhara ya uongozi mbovu wa Makinda. Ila wafahamu kuwa kutokana na kuenea kwa mawasiliano na upashanaji wa habari, madudu ya Makinda yanajulikana kwa wananchi. Haiwezekani wananchi hata wapenzi wa CCM washuhudie hoja zinazolenga kuokoa pesa yao zinazimwa eti kwa vile zimeletwa na wabunge wa upinzani.
Watanzania wanajua machungu ya umaskini unaosababishwa na mfumo mbovu wa utawala ulioshindwa kusimamia kodi na rasilimali zao. Wanasikia madudu yote yanayoibuliwa na wakaguzi wa hesabu za seirikali kila mwaka ambayo ni chanzo cha umaskini wao. Watafikia mahali watachoka na hapa ndipo uhovyo wa Makinda utaitafuna CCM.
Tuombe Mungu Makinda na Ndugai waendelee kuonyesha udhaifu wao ili wananchi wautumie kuwaadhibu wao na chama chao.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 11, 2013.
Subscribe to:
Posts (Atom)