The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Sunday, 15 November 2015

Open notelet to president Magufuli


            Honourable President John Pombe Magufuli,
            I must admit from the outset. I didn’t like your party before appointing you its presidential flagbearer. Guess what. I predicted you’d become fifth president two years before. Had the opposition brought another person other than Eddy Lowassa, my love wouldn’t have waned. Again, after Lowassa was crowned opposition’s flagbearer, my love shifted to you but not to your party. I still dislike your party up till you overhaul it. Yet, I’ve a lot of veneration and faith in you as a hard worker.
            Sir, I humbly seek you leave to communicate with you for the first time. I hope –before you became president –you used to read this column. I’m sure you liked it so much and you still do. Take note that – after becoming president –you may find yourself being probed or clinically examined if not dissected here. Today I’m touching base with without anything in my head or blood. I’m as sober as a judge.
            I pray that I address the following:
Firstly, Boozers have sent me to tell you the following that they want you to fulfill. They want you to declare your wife’s and your wealth and thereby ask all of your officials and who’s who in your government to follow suit.
            Secondly, you must mercilessly deal with drug dealers that your predecessor spared for reasons only known to himself failure to which boozers will believe –as they did with him –that you’re benefiting from this crime.  So, too, you must mercilessly take on corrupt officials. It is easy. Form an underground task force to probe all that cheat in declaring their wealth. Make sure you hit the nail on the head so that the message sent can daunt and put sense into others still at large. Boozers still believe that you can retrieve the dosh these corrupt putas stashed in Swiss Banks and other Western capitals.
            Mr. brand new President, you’re in the past government. You saw and heard everything. Thus, you know everything. Do you remember the promises your predecessor offered on stamping thugs out of the hunk to no avail? Please, spear nobody. Boozers say that your job’s still bigger. Make sure that all thugs are deposited behind bars. So, too, avoid thuggish behaviour of allowing your wife to form an NGO aimed at minting and printing dosh on the back of the state house.  For boozers, forming a bogus NGO is as good as thuggery. After you’re done with thugs take on thuggish investment contracts that need to be reviewed, annulled and whatnot.
            I heard one rookie saying he is another Sokoine. Had he known that you’ll become bigger than his Sokoine, he’d not waste time. I hope you remember what Sokoine did vis-à-vis saboteurs that we still have in the upper echelons of power. Play your cards secretly and wisely otherwise you’re playing with fire. You know what I mean. Before I forget, taking on bogus contracts won’t be enough without hauling up all those involved in past scams such as EPA, Escrow, IPTL, Richmond, Merementa, Mwananchi Gold, UDA, SUKITA, Kiwira, Loliondo, Presidential jet and radar and many more you obviously know.
            Everybody is waiting to see the type of people you’re going to appoint to be your ministers. Boozers say is openly and loudly that you’d not appoint forgers, corrupt, inept and indolent mortals. All those who butchered our education shouldn’t be considered.  Think about revivifying our education system. Being a teacher yourself, I know you know the importance of education especially as it was fine-tuned by mzee Mchonga.
            Another problem that denies boozer sleeps is none other than ghost workers, illegal immigrants mostly from Asia and tax evaders. Boozers know too well as you do that our country has become shamba la bibi under chizi. To do away with this anathema, make sure, you put a stop on all such criminality. Go further. Probe your predecessors and their family members. We know of young kids who became rich just because their parents were biggies. Descend on them like a hawk descending on chicks.
            There are other areas to reconsider. Increase the budgets of education and health for the development of the country.  No sick and ignorant nation can develop in a meaningful manner.  I heard you putting a stop on globetrotting that your predecessor was famous of. Make this habitus-cum-continuum instead of being an action. Probe the swelling of our external debt. There must be culprits waiting to be nabbed and jailed hither so to speak.           
            Finally, boozers are waiting for you to fulfill your promises you made during the campaigns so as to convince them to vote for you knowingly you’re seconded by a corrupt party. Overhaul it and make sure no stone is left unturned. In doing so, you need to be proactive instead of being reactive.

Next time you’ll the series of poetic Hello Mr President.
Source: Guardian November 15, 2015.

Friday, 13 November 2015

Mlevi akumbuka Kiquete kuingiana EPA kuondoka na Escrow

            














Utawala wa rahis mtaafiska Njaa Kaya Kiquette ulisifika kwa mambo mengi ya hovyo mojawapo ikiwa ni kukumbwa na kashfa mara kwa mara. Kwani lilikuumbwa na kashfa hata kabla ya kuundwa huku jamaa akituhumiwa kushiriana na rais Mstaafika Ben Makapi kuchota njuluku Banki kuu kwenye fuko la madeni ya nje almaaruf EPA. Wote wawili hawa kukiri au kukanusha. Hata hivyo, ushahidi wa kimazingira unaonyesha ukweli hasa pale Kiquette alipowataka waliochota fedha hizo kurejesha badala ya kuwafungulia mashtaka.  Hata ukimya wake na kukwepa kukiri au kukanusha unaweza kuwa ushahidi mzuri tu unaoelekeza kwenye ukweli wa mambo.
            Jamaa alipowambia wenzake kurejesha njuluku na si kuwashughulikia, wenye akili walijiuliza; Je ni waarabu wa Pemba? Je kuamuru kurejeshwa chumo la wizi si kushiriki wizi ule ule kwa mlango wa nyuma? Je si motisha kwa wezi wengine –hata ambao hawakuwa na mpango wa kuiba –kuiba wakijua hakuna adhabu wala maumivu?
            Bahati mbaya, jamaa hakuwahi kueleza mantiki na sababu za kupinda sheria kuwanusuru wezi kama hanao ushirika. Wengi walitaka kusika utetezi wake.  Jamaa ameondoka na EPA kama alivyoingia navyo. Ameondoka amechafuka zaidi kwa kashfa nyingine ya Escrow. Hapa ndipo usemi kuwa aliingia kwa EPA na kuondoka na Escrow unapata maana.
            Jamaa anaingia kwenye vitabu vya historia kama rahis aliyewaonea huruma wezi kiasi cha serikali yake kusifika kwa ufisadi zaidi ya mema. Atakumbukwa kwa matumizi na matanuzi yake yaliyoongezea uchungu kwa walipa kodi walioibiwa haya mabilioni ya EPA na Escrow. Nani anaweza kusamehe au kusahau kashfa ya Richmond ambayo ilimhusisha mshirika na rafiki yake mkuu waziri wake mkuu Eddie Lowassa ambaye hadi kesho anasema alitolewa kafara. Je waliozoea kuuibia umma kwa maslahi binafsi na kisiasa walikuwa nyuma ya wizi huu, ni juu ya msomaji kuamua mwenyewe.
            Licha ya kuzidi wizi wa mabilioni, utawala wa jamaa ulishuhudia deni la taifa likifumka kupita viwango tokana na matumizi ya hovyo na ukwapuaji ambapo wahusika hawakuchuliwa hatua. Nani mara hii atasahau utamaduni mpya wa kuficha majina ya walaji aliokuwa akiandamana kwenye mamia ya safari zake ughaibuni?
            Pia, utawala wa jamaa unasifika kwa kuvumilia mafisadi wengi walikingiwa kifua bila kujua sababu za msingi za kufanya hivyo. Rejea, mfano, mamlaka za Uswisi zilipolalamika kutopata ushirikiano toka lisirikali kurejesha mabilioni yaliyofichwa huk, bada Badala ya kushangilia kitendo hiki cha utu, tulishuhudia balozi wa Uswisi nchini Olivier Chave akitishiwa na mwanasharia mkuu wa wa wakati ule Freddie Werema aliyejizolea sifa ya kutetea uoza kuliko uadilifu. Ni huyu huyu aliyetishia kumkata kichwa mheshimiwa mbunge aliponyooshea kidole ujambazi wa Escrow ambapo matapeli wa kitanzania na kimataifa waliweza kutumika kuwaibia watanzania jumla ya shilingi zipatazo bilioni nyingi.
            Wakati baadhi ya washirika wa jamaa wakikerwa na kufichuliwa madhambi yake, yeye alikuwa kimya akitabasamu kama kawaida kana kwamba hakuna kilichotokea! Wengi walianza kuuliza. Ndiyo haya Maisha Bora kwa Wote au kwa baadhi tena wateule, wake na watoto, waramba viatu na marafiki zao?
            Mtangulizi wa jamaa aliondoka akinuka kwa kashfa ya kufanyia biashara ikulu na kujitwalia mali za umma, jamaa amempiku. Kwani ameondoka akinuka wizi kwa kutoshughulikia waliovunja Benki kuu na kuiba mabilioni.
            Wapo wanaodhani wizi wa Escrow –sawa na wa EPA –una mkono wa chata twawala. Kwanini wizi huu wote ulifanyika karibu na uchaguzi ambapo chama kilikuwa kinataka kushinda kwa udi na uvumba? Hapa ndipo ulipo mkanganyiko ambao ulimhusisha wore waliopo na waliotimka.

            Hata hivyo, kilichowazi ni ukweli usiopingika kuwa Kikwete anaondoka madarakani akiwa ameweka rekodi ya kuingia na kuondoka madarakani kwa kashfa za wizi wa mabilioni ya watanzania maskini ambao serikali yao licha ya kuruhusu wizi inaendeshwa kwa fedha za kukopa na kuomba. Hapa hujaongelea ni namna gani ofisi yake imetumika kuanzishia NGO za bi mkubwa kwa ajili ya kutunisha fuko la baada ya kuondoka ofisini. Hapa hujagusia kashfa zilizowahusisha watu wake wa karibu na hata yeye mwenyewe.
Chanzo: Nipashe Nov., 14, 2015.

Tuesday, 10 November 2015

Kijiwe chahoji baadhi ya mambo kwenye uapishaji


            Baada ya wazee wa Kijiwe kujialika kwenye sherehe za kuapishwa kwa rahis mpya Dk Kanywaji Makufuli na makamu wake Samie Sululu, kimekaa kama kamati kuhoji baadhi ya mambo ili kujua maisha ya viongozi wake wapya
            Tukiwa tunapata kahawa na kashata anaingia Mgosi Machungi akiwa na gazeti la leo. Anaamkua na kusema, “Vipi wazee na uchovu wa jana kushuhudia kuapishwa kwa waaji wenu wapya?”
            Mpemba anamjibu, “Hata nawe hawa walaji wako sawa nasi.”
            Mgosi anajibu huku akijiweka vizuri kwenye fomu, “Mpemba tiheshimiane. Unaona mimi ni mtu wa kuiwa kama wadanganyika?”
            Mpemba anajibu, “Yakhe kwani we Nzanzibari au Ntanganyika?”
            Mgosi anajibu, “Mimi mtanzania sawa nawe. Anyway, haya tiyaache.”
            Baada ya Kapende maongezi yanakwenda tenge, anaamua kuwanyang’anya mic na kusema, “Mwenzenu yote tisa, sikuona mantiki ya kumualika mchunaji wa Kinigeria Temitope Jushwa ambaye najua mhoteli wake uliua makumi ya watu kutokana utapeli na tamaa zake. Je huyu naye alialikwa kama nani au ni yale yale ya babu wa Loliondo?”
            “Usikumbushe huyu habithi wa Liloyondo aliyewatapeli na kuwaua wengi kwa miwaya?  Huoni walikuwa wakimsifia wanavyoanza kunyonyoka kama kuku aliyenyeshewa mvua?” anajibu Mipawa.
            Anakohoa na kuendelea, “Nadhani kuna kitu nyie hamkukipata. Hamjui wanasiasa, wachunaji na waganga wa kienyeji lao moja? Sikushangaa kumuona huyu mchunaji wa kinigeria akishiriki sherehe zetu. Nikikumbuka alivyondangaya Joisi Banda kuwa angechaguliwa rahis wa Malawi sina hamu na tapeli huyu.”
            Mzee Maneno anauliza, “Je huyu mnigeria alikuja kama nani wakati si mwanasiasa?  Au tunataka kuungana na Nigeria? Maana Njaa Kaya na Nkapa walikuwa mfukoni mwa Dongote na Kanywaji sasa na Jushwa!  Sijui huyu naye kama uwekezaji wake una tija au ni uchukuaji ule ule. Dongote amewekeza kwenye saruji. Huyu nadhani atawekeza kwenye kondoo wa Bwana.”
 Mijjinga anakula mic, “Usishangae kesho ukaambiwa huyu msanii mchunaji wa kinigeria kesho anawekeza kwa kufungua bonge ya kanisa au uwanja wa kutendea miujiza. Umesahau kuwa Danganyika ni shamba la bibi? Kwanini hwajiamini au kumwamimi Mungu? Kwanini kama ni kuomba wasijiombee wakati wana akili sauti na mawazo? Aibu tena yam waka!”
            Kapende anachomekea, “Wenzangu sijui macho yangu, maana kwenye kuapishwa Makufuli akina Luwassa na wenzake wa UKAUA sikuwaona au waligwaya baada ya kujidanganya kuwa tungewaamini pamoja na usanii na ufisadi wao?
Mbwamwitu anajibu, “Wawepo kufanya nini wakati walitulazimisha kuchagua chata la mafisadi wale wale tokana na upogo uroho na ujinga wao? Wangeweka wapi nyuso zao wakati ni wasaliti watupu? Mie naona lao na CcM ni moja tu wanatufanyia usanii huku wakipeana mishiko nyuma ya pazia.”
            Kabla ya kuendelea Mgosi anapoka mic, “Hebu Mpemba tisaidiene. Hivi hawa CcM kualika madikteta wengi kiasi hiki walimaanisha nini au nao wanapaga kutifanyie hivyo?”
             Mpemba anajibu “Yakhe mie wallahi sioni tofauti baina ya uimla wa chama na watu binafsi.”
Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “Hao mnaowaita madikteta si kazi yenu bali wanakaya wao. Kwanini mnapenda kuingilia mambo ya wengine wakati yenu yanawashinda?”Awe na mume au asiwe naye yakuhusu nini wewe au umbea tu? Mbona nyinyi hamji na wake zenu hapa?”
            Mbwa mwitu anakula mic, “Da Sofi acha nikuchomekee. Hujui kuwa mambo mengine kuyafikiria achia mbali kuyasema yanahitaji kichaa cha aina yake?”
            Mheshimiwa Bwege anakula mic, “Kwani nani anaweza kuwa rahis Afrika bila kuwa dikteta hata kwa mlango wa nyuma? Unapokuwa juu ya katiba unategeme uwe nani kama si dikteta? Unapotawala miaka karne hata kama ni chama unategemea uwe nini kama si dikteta? Warabu wa Pemba ati.”
            Mijjinga anarejea “Mwenzenu naona kama tumetua mzigo huu uliokuwepo ingawa hata huyu anayekuja hatujui kama atakuwa nyenzo au mzigo ule kama huu ulioondoka na walaji wenzake. Nangoja kusikia atakavyofumia mikataba ya uchukuaji aliyoinga Tunituni na huyu msanii aliyekitoa. Nenda mwana kwenda na utokomee na ahadi zako za uongo. Mambo kwa Makufuli, halo halo!” anapiga ung’ende Mheshimiwa Bwege huku akinyoosha kidole juu kama wacheza mdundiko.
            Mwenzenu mie huenda mshamba. Huu uchafuaji wa mazingira wa kulipua mizinga mliuonaje?”
            Msomi anajibu, “Unashangaa kulipua mizinga? Huu ni urithi na muigizo toka kwa wakoloni waliotutawala na kutuachia makando kando ya ukoloni. Huoni hata hawa wetu hukaa kwenye nyumba ile ile yaliyokuwa makao makuu ya mkoloni mwenyewe? Unategemea nini kuwa na viongozi wanaotoa ahadi wazitekeleze au kushiriki ufisadi wazi wazi tukaendelea kuwagwaya na kuwapa kiburi badala ya kuwafikisha mahakamani? Mie namngojea bwana Kanywaji kuona hawa waliomtangulia atawatia adabu namna gani. hapa lazima wote kuanzia awamu pili hadi hii iliyokwisha lazima wawe na appointment na pilato tu kama kweli jamaa anataka kung’oa mzizi wa fitina na ufisadi.”
            Kanji aliyekuwa akiongea na mkewe kule Bombei anaamua kutia guu, “Veve Somi ongea kama toto dogo siyo. Veve nazani vatu ya chama moja naweza fungana? Hii Kufuli na ile nasema veve yote koo moja. Kama nafunga hii natangulia naye tafungwa na ile nafuata. Yote hii siasa dugu yangu. Najua vengi goja timiza promise natoa. Ohoo! Nenda lia sana sana dugu yangu. Hapana jua samaki yote iko na surubu?”
Chanzo: Tanzania Daima Nov., 11, 2015.

Sunday, 8 November 2015

Habith Salva Rweyemamu ang'atuka ikulu




























Taarifa zilizotufikia ni kwamba yule mwandishi kidhabu na mchumitumbo Salva Rweyemamu hatimaye ameondolewa ikulu na utawala mpya wa awamu ya tano. Kwa tunaomjua kwa kufanya naye kazi kwa karibu, tunamjua kama alama ya uoza wa serikali ya hovyo na fisadi iliyomaliza muda wake. Rweyemamu na waandishi wenzake wengine nyemelezi walitumiwa na Jakaya Kikwete kuosha nepi zake na kuweza kuwazuga watanzania na kumchagua rais wao jambo ambalo watalijuita milele. Kidhabi na habithi inasemekana haziivi na Dk Kanywaji Makufuli. Kwa tunaomjua, ni mtu wa hovyo mnafiki na hasidi ambaye kuwa kwake ikulu ni machukizo kwa Mungu na watanzania. Hayawi hayawi. Tunangoja na wengine wote waliopewa vyeo kwa kulipana fadhila kuanzia za ngono hadi kufua nepi watimliwe mara moja ili kurejesha heshima ya ofisi za umma. Hongera Magufuli kuanza kuonyesha ndia. Nenda mwanakwenda Salva. Nenda katokomee kusikojulikana. Nenda utuondelee mbu kiza na aibu.Nenda mwanakwenda na ukatokomee. Nenda usiangalie nyuma. Nenda kama kibwengo na moto wake kichwani. Nenda mwanakwenda usigeuke nyuma. Nenda ukaishie uishiako. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

Bongo suffers from PPD malady


            In my last two weeks’ piece I extolled the hunk for conducting very placatory elections. However, they’re some issues I didn’t touch on due to the space limit. Today, I’m going to allude on those issues that our hunk is facing currently. I know. This won’t augur well with a section of our bin-Adams especially the high and the mighty. Bear with me. I like to do things in the way that pleases others even if it sometimes –accidentally –hurts others.  First of all, as a Psychedelician I must say it loudly and clearly that our hunk needs some remedies to do away with the current paranoia she suffers that we technically call Paranoid Personality Disorder (PPD).
Everybody knows –including insects and birds –that our hunk suffers from petty nationalism whereby people gang along ideological line while they suffer the same magnitude of disservice equally. Do landlords and landladies discriminate when they mess paupers’ lives demanding this and that simply because they’re living in their mabavu za mbwa? Another vice we suffer is superficiality whereby we want to make those who don’t know our true state of affairs believe we’re a peaceful hunk. Can a hunk puffing with reeking corruption be truly peaceful? Where do you put googly grafts such as EPA, Escrow, Richmond, Meremeta, UDA, SUKITA and others that sunk poor taxpayer’s billions of dosh? Can a hunk that loses revenues thanks to having a sitting-duck-like govt be truly peaceable? Do we really know the meaning of peace?
 Let me touch on another disease that has eaten us big time. We’re suffering from paranoia from which we fear “our enemies” real, unreal, manmade, womanmade [unspecified]). Before the general elections I heard some brain-dead specimens intimidating boozers claiming that if they vote for the opposition our hunk would become another Rwanda of 1994 or the recent Burundi if not Central African Republic (CAR). Truly, and unfortunately for the boozers, some bought in this fallacy for fear of the unknown.
Methinks. If we’re to truly fear, we’d have feared those who robbed us and spent the same dosh bribing us so that we can give them more yum-yum for more five years after ruining our lives big time. Again, whenever they feed us with their lies, we take them without a grain of salt! How many fisadis that Jimmy Rugemalayer gave the cuts returned to the house? Who voted for them if not pauperized boozers?  Let me say it clearly and loudly. Is it an insult to say that we are a sick hunk that believes in hoo-has as we fear torturing our brains to seek Truth that’d free us? Tell me. Is there any peace in Zenj now after Zenj Evading Commission (ZEC) annulled results without giving logical reasons?  This makes our so-called peace hypocritical hypothetically.
Well, some loudmouthed politicos used to say ours is a peaceable hunk. How if at all thugs and fisadis have held our hunk at ransom? Who’s bamboozling who here?  I don’t know if our brethren with albinism do enjoy this abunwas freedom at all? What of the elderly that are butchered every day and nothing is done to address this Satanism? I don’t think our farmers do enjoy the said peace by being loaned of their produces. What of the low-rank civil servants that are apprehended for receiving some peanuts while sharks steal billions and get away with murder? Do they think we’ve forgotten the bigwigs who forged their academic credentials?
 Ask our poor pregnant women who can be tortured by nurses and caregivers like the one Rhoda Bujiku whom Constancia John in Simiyu beat when she went to deliver. Do such Rhodas enjoy this make-believe peace? I don’t think students who sit on the floor are indeed enjoying this peace. What of the passengers that are oft-butchered due to traveling on substandard roads many swindlers construct poorly. Don’t the powers that be know this really? Where is this illusive peace really?
Going back to PPD, I found that our paupers fear the unknown unbeknownst that the enemies are within. Take this from me. During the campaigns our paupers were fed with many meal-mouthed promises. Will they stay put to see to it that those who offered such promises are living up to their words? Where is Maisha Bora kwa Wote Apechealolo (MBWA)? Didn’t they guy cheat them for ten years and leave without fulfilling any of them? Yet again, you’ll hear them praising such a cheater as a good person while he actually is a big liar. Maybe, big liars don’t lie and when they lie their lies become truth. Yes, for boozers suffering from PPD such is a rationale. How do they touch on an untouchable even if it is their right and they’ve what it takes?
Given that I’m now waiting to see what this new fella, Kanywaji, will do to deliver on his promise, let me go and grab some kanywaji as I wait.
After looking at our peaceability, let’s gage if what we boast of is real peace and how. Can peace and injustice go hand in hand really or sleep in the same bed really? What an unjust hunk that is!
Source; Guardian Nov.,8, 2015.

Saturday, 7 November 2015

Wapiga kura waliikataa CCM UKAWA wakairejesha















            Uchaguzi mkuu umekwisha. Walioshinda wameshinda na walioshindwa wameshindwa.  Hata hivi haina maana kuwa wale wanaodhani hawakutendewa haki wasiende mahakamani. Kwa umma wa watanzania, wamemaliza kazi yao kwa kutekeleza haki yao ya kikatiba. Kilichobaki ni kusonga mbele katika ujenzi wa taifa. Pamoja na kuwepo kasoro za hapa na pale –ambazo, kimsingi, haziepukiki –tunaweza kusema uchaguzi ulikwenda vizuri kwa amani na utulivu.
            Kama kichwa cha habari kisemacho, ni kwamba wapiga kura walidhamiria kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM). Hata hivyo, Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) –ambao umeachana na katiba ya wananchi –umeirejesha CCM madarakani ima kwa bahati mbaya au kwa maksudi. Makala hii inalenga kueleza sababu za kudai kuwa UKAWA wameirejesha madarakani CCM baada ya wapiga kura kuitosa. Nazo ni kama ifuatavyo:
Mosi, UKAWA walifanya kosa kubwa kwa kushindwa kusoma kile ambacho waingereza huiita Realpolitik yaani siasa za msimu au za wakati fulani za Tanzania. Tunaweza kusema kuwa walichoshindwa kuelewa UKAWA ni kwamba hapakuwa na jambo lolote au mtikisiko ambavyo vingebadili misimamo ya wapiga kura au kufanya waichukie CCM sana kiasi cha kuweza kumchagua yeyote aliyesimama kuipinga. Ni kwamba hapakuwa na vitu kama vile kuzorota sana kwa uchumi, ukame, baada la njaa au balaa lolote ambalo lingeonyesha kushindwa kwa CCM.
Waliishaichoka CCM ila hawakuwa na chaguo.
            Kwa walio wengi tofauti baina ya rais John Maguli na waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa ni majina lakini ni makada wale wale wa chama kile kile sema mmoja hakuwa na mawaa wala historia yenye kughubikwa na wingu la uchafu na ufisadi.
            Kosa la pili ni ile hali ya kumleta Lowassa na kumfanya mgombea wa UKAWA. Lowassa hakuwa akiuzika kutokana na historia yake.  CCM walitumia fursa hii kuwazidi UKAWA kwa kumwita kapi na asiyefaa ukiachia mbali kudai kuwa alihonga mabilioni kwenye mchakato na ana majumba nje.
 Tatu, ilikuwa ni UKAWA kutokuwa na hoja za kuweza kuwashawishi wapiga kura’ kimsingi, UKAWA hawakuwa na hoja baada ya kuizika hoja ile iliyowafanya maarufu ya kufichua na kupambana na rushwa. Hii ilionekana kama kujipiga mtama, ugeugeu, kutoaminika, uchumiatumbo na hata ubabaishaji wa kawaida. Nani angewaamini watu wasioaminika madaraka makubwa ya kuongoza nchi huku wakiwa na watuhumiwa wakubwa wa ufisadi. Wasingefanya kosa kuwaachia amali za taifa watu kama hawa. Sijui kwanini wasomi kama maprofesa Safari na Baregu au mchumi mkongwe Edwin Mtei hawakuliona hili?
            Sababu ya tatu ni ile hali ya Lowassa kuwa bubu akionyesha wazi kushindwa kujenga hoja wala kumilki jukwaa. Mara nyingi alikuwa akiongea kwa muda mfupi huku akiwaachia akina Fredrick Sumaye na Freeman Mbowe waongee kwa muda mrefu utadhani wao ndiyo walikuwa wagombea. Ilifikia mahali hadi watu wakaanza kushuku afya yake kutokana na hali hii. Wapo waliodhani ima Lowassa ni mgonjwa au aliogopa kuongea sana ili asiwakumbushe wapiga kura madhambi yake ambayo kimsingi, yaliibuliw ana UKAWA hawa hawa hasa walipotoa orodha ya mafisadi papa pale Mwembe Yanga mwaka 2007. Laiti Lowassa angetumia fursa hii kupangua na kukana tuhuma nyingi za ufisadi na wizi wa mabilioni mojawapo ikiwemo kashfa ya Richmond, huenda angeweza kuwapata wapiga kura wengi. Ni bahati mbaya kuwa –kwa sababu azijuazo binafsi –Lowassa hakufanya hivyo jambo ambalo lilizidi kupoteza uwezekano wake kuchaguliwa kuwa rais.
            Sababu ya nne ni ile hali ya CCM kumteua Magufuli ambaye anasifika kwa uchapakazi wake akilinganishwa na mawaziri wa serikali liyopita. Pia Magufuli hakuwa na kashfa nyingi ikilinganishwa na Lowassa ukiacha ile hali ya kusakamwa kuwa ni mwana CCM na pia alihusika kwenye utwaliwaji wa nyumba za umma chini ya utawala wa awamu ya tatu jambo ambalo, kimsingi, linapaswa kuelekezwa kwa Benjamin Mkapa.
            Hata kwa upande wa visiwani hali ni ile ile hasa pale chama kilichotegemewa sana cha Civic United Front (CUF) kilipoteza umaarufu, imani na ushawishi kilipofunga ndoa , kwanza, na CCM kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) na pili na vyama vingine kuunda UKAWA. Nadhani wapiga kura wa visiwani wanazijua vizuri siasa za bara hasa ujio wa Lowassa na mizigo yake ya tuhuma. Hivyo, athari za Lowassa zimeweza kuathiri sehemu mbili za muungano ukiachia mbali kuwa hata namba ya CUF kushinda visiwani ni suala la mjadala hasa tukiangalia wafuasi, wanachama na mashabiki wake kwenye visiwa viwili vya Pemba na Zanzibar na historia zao. Kwa waliotegemea kufanya mabadiliko kujikuta wana wagombea wale wala na siasa zile ni vigumu kuwashawishi. Mfano ni kuondoka kwa Profesa Ibrahim Lipumba ambaye –si haba –ana wafuasi wengi visiwani. Sababu nyingine ni kuchoshwa kwa mgombea Seif Sharrif Hamad. Alipaswa kupisha nguvu na sura mpya kama vile Haji Duni ambaye alimtuma CHADEMA asifue dafu.
            Kwa ujumla ni kwamba UKAWA walishindwa kupambana na nguvu za ushawishi na umakini kimkakati wa CCM hasa kwa kuondoka kwenye kile walichokisimamia kwa miaka yote. Hivyo, hawana haja ya kulaumu wala kulalamika bali wajilaumu wenyewe kwa kushindwa kuona mapungufu yao wenywe na ya wapinzani wao. Hata hivyo, tunawez a kusema kuwa, kama kutakuwa na upinzani wenye visheni, miaka kumi ijayo inatosha kuitupa nje CCM. Nalo hili linategemea na utendaji wa Magufuli.
Tanzania Daima Nov.. 8, 2015.

If Africa were a one united country!


King Kinya got it right here

Thursday, 5 November 2015

Samia Suluhu Hassan ni nani?



Pamoja na kujua kuwa Bi Samia Suluhu Hassan ndiye makamu wetu wa rais na mwanamke wa kwanza nchini kushika wadhifa huu, wengi hatujamfahamu vizuri. Kwa mfano, katika sherehe za kuapishwa kwake na rais John Magufuli tulionyeshwa wana familia ya Magufuli. Ajabu, tangu ateuliwe kuwa mgombea mwenza hadi kuwa makamu wa rais, habari za familia zake ni kama hazipo. Unapokuwa kiongozi wa umma lazima mambo yako mengi yawekwe wazi. Kwa mfano, tunamjua mke wa rais Magufuli kuwa anaitwa Janet. Sambamba naye hatumjui mume wa bi mkubwa huyu. Je ni single, ameachika au vipi? 



Hii kitu wakati ikiwika ulikuwa wapi?


Tuesday, 3 November 2015

Kijiwe champongeza Dk Kanywaji kwa urahis


 














            

Baada ya wapingaji kufanya kosa la mwaka kwa kumkumbatia adui yao waliyembomoa hadi akabwaga uwaziri mkubwa kiasi cha kuiwezesha Chama Cha Maulaji (CCM) kushinda kirahisi, Kijiwe kimeamua –kwa makusudi na roho safi –kumpogeza Dk Kanywaji Makufuli.
             Mpemba anaingia akiwa na bashasha kidogo. Anakula mic, “Yakhe mmesikia jinsi wapingaji walivokiwezesha chama twawala kuendelea kutula?”
            Mgosi Machungi anachomekea, “Utaiwa wewe au kuana wao kwa wao haiwi mtu hapa.”
            Kapende anakamua mic,”Kama mkikumbuka, nilikuwa mpenzi wa upingaji kabla haujaingia kitanda kimoja na Luwasa. Kwa vile wapingaji walituona sisi mabwege na wasio na kumbukumbu kwa kumkumbatia yule yule waliyetuaminisha ni fisadi, kura yangu niliharibu.”
            Mijjinga anakamua mic, “Ni kweli usemayo ndugu yangu. Hata mimi nilitaka hata kugombea uishiwa. Lakini baada ya kuona chata nililotaka kutumia limemkumbatia huyu jamaa, niliamua kuachana na ndoto za ubunge na kuharibu kura yangu. Utadhani tuliambiana.”
            Mipawa naye hajivungi. Anakula mic,”Kusema ukweli jamaa wametunyima fursa ya kuleta mageuzi kwa ajili yetu na vizazi vijavyo. Inasikitisha na kukatisha tamaa ukiachia mbali kuudhhi. Sijui tutafanyaje baada ya jamaa kuondoka na vyama vinne kwa mpigo?”
            Sofia Lion aka Kanungaembe aliyeingia punde akiwa ametinga kwenye mavazi ya CCM huku akishangilia kwa sana anakula mic,”Yako wapi? Tuliwaambia hashindwi mtu hapa piga ua. Sasa mtasemaje zaidi ya kuufyata.” Anasimama na kuangalia huku na kule na kuendelea, “Jamani, hamna haja ya kusikitika. Amkeni tushangilie ushindi wa ndugu yetu mwenzetu Dk Kanywaji Makufuli ambaye –kama alivyoahidi kwenye kampeni –lazima awafunge mafisadi akiwamo mtu wenu aliyemgalagaza chari.”
            Msomi Mkatatamaa anakwanyua mic, “Japo sikubaliani na da Sofi kwa yote aliyosema, nakubaliana naye kuwa tunachopaswa kufanya hapa ni kumzonga Makufuli atimize ahadi zake. Hakuna kitu kimenivunja moyo kama kuona watu wanavyoshindwa kuisoma na kuelewa historia kiasi cha kujifunza toka kwake. Nimehuzunishwa sana na kushangaa sana kuona kuwa wanasiasa wetu walishindwa kujifunza toka kwa Mremavu aliyeua NCCR-Mageuko mwaka 1995. Kwa upande mwingine naweza kusema kuwa upogo wa kumkubali Luwasa azike vyama vinne kwa mpigo ulitokana na ruiya ya kudhani kuwa kuondoka kwa Luwasa CCM kungesababisha vigogo wengine wamfuate kama ilivyo kuwa kwa rafiki yake Dk Kanywaji, Raira Odinga alivyofanya kule kwenye kaya ya nyayo wasijue siasa za Bongo ni tofauti na za kule. Kama walivyesema wasemaji waliotangulia, sijui hawa jamaa wataweka wapi sura zao baada ya kutuletea balaa hili?”
            Kanji anaamua kutia guu, “Somi veve iko sema zuri. Hapa napaswa laumu pingaji. Imepiga tama yenyeve sasa talia na nani dugu yangu. Mimi furahi san asana ona chaguzi nakwisha salama ili vatu iendelee na biashara yake.”
            “Pamoja na kumkubali Dk Kanywaji ambaye tulisoma wote seminari tukitaka kuwa makasisi kabla ya kushindwa kwa uchapakazi wake, sitegemei jipya toka kwake. Utakuwa ubwege kutegemea mtu mmoja aubadili mfumo uliomlea na kumkuza. Sana sana mfumo wa ulaji utambadili naye awe kama wenzake. Mmesahau kuwa kambale wote wana sharubu siyo?” anajibu mheshimiwa Bwege huku akikuna kidevu chake chenye mvi kama Dk Kanywaji anayedai walisoma wote seminari kabla ya miili yao kushinda roho zao.
            Msomi anarejea tena, “Sina haya ya kupingana nawe. Ila ukimlinganisha Dk Kanywaji ambaye mimi nilimfundisha kemia pale chuo kikuu cha Manzese, bado ana udhu. Kubadili au kubadiliwa na mfumo itategemea na shinikizo letu katika kumtaka atimize na kutekeleza ahadi zake lukuki alizotoa kwenye kampeni. Nadhani pia inabidi tumponge Luwasa kwa ushindi mnono hasa kufanikiwa kulipiza kisasi kwa waliomshitaki akautema uwaziri mkubwa na kuweza kuua vyama vinne kwa mpigo kama inzi. Pia nashauri tuanze kuangalia namna ya kubadili kijiwe chetu kuwa chama mbadala baada ya vyama vyote vya siasa vilivyopo –ima kugeuka CCM B au kusambaratishwa na upogo na uroho wa kutaka kutumiana vikaisha kutumiwa na kuuawa mchana kweupe.” Anakohoa kidogo na kuendelea, “Tukubali tumeingizwa mkenge na wale tuliodhani ni wenzetu wakati ni wenzao.”
            Kabla ya kuendelea, Mbwamwitu anachomekea, “Mnashangaa nini wakati wenzenu waliuza mechi? Hamkuona akina prof Pumba na Dk Slaa walivyostukia dili? Kumbe hamkujua hili?”
            Msomi anamtazama Mpemba na kuendelea, “Nadhani sasa tuelekeze macho na masikio yetu kule Zenj ambapo jamaa wa madevu anang’ang’ana angalau aendelee kuwa kwenye serikali ya umoja wa ulaji kitaifa. Tuombe Mungu wasinyotoeane roho kwa sababu ya ngurumbili wawili wanaogombea ulaji. Hapa lazima busara itumike ili kuendelea kutanua kama walivyozoea. Hata hivyo, naweza kusema kuwa ufa mkubwa umeishatokea.”
            Mijjinga naye anarejea, “Nakuunga mkono msomi mwenzangu. Tunachopaswa kufanya hapa ni kuunda kikosi mbadala ya kukomboa kaya hii. Najua Dk Kanywaji atakwamishwa na wenzake vinginevyo afanya kile alichofanya Mutharika wa Malawi, aunde chata lake akiwa humo humo ili kuwasulubu wale mafisadi aliotwambia anawajue ili asiishie kuwa kama njaa Kaya aliyesema anawajua mafisadi na wauza bwimbwi akaishia kula nao.”

            Kijiwe kikiwa kinanoga si likaja kundi la wakota wa CCM likinengua na kushangilia!
Chanzo: Tanzania Daima Nov., 4, 2015.

Kwa vijana wa zamani tu


Sunday, 1 November 2015

When Bongo politics became nastily bongo-bongo

Bongo politics had saneness before the Chama Cha Maulaji (CCM) appointed its presidential candidate Dr Joni Kanywaji Makufuli. Before this exercise that saw many bigwigs left out in the cold, voters had a variety of choices. Everything was divided right in the middle between a ruling rotten lot and anti-graft opposition. Again, soon after CCM got their man, one creature Eddie Luwasha altered the map of the politics of the hunk. Two visible sides the hoi polloi used to see and assumed they’d vote from vanished. Those we used to view as adversaries went together in bed so as to leave voters with no choice at all.
            Looking at the whole stuff through my booze eyes I can restfully argue that our politics has become bongo-bongo stuff whereby voters –apart from having no choice –had to choose from the same meme and kit and caboodle of swindlers. I say this with many good reasons among which are:
            Firstly, I must admit that our politics are becoming as useless as everywhere in Africa that burns billions of dosh to get the same stuff.
Secondly, I must say it clearly and loudly that we’d the same party to vote from. What do you call choosing between two CCM’s cadres namely Makufuli and Luwasha? Their differences are in their names and the parties they used to seek ulaji. I can use Gaia hypothesis of connectivity of beings to argue that Makufuli and Lowassa constitute a political single entity, and they stymied change for the hunk.  When it comes to their integrity, vision, myopia, hopelessness and whatnot they’re but identical twins from the same mother CCM.
Thirdly, what do you call this situation whereby those who made you believe they’re against graft end up in the same bed doing the same simian biz? I think my UKAUA brethren get me well that their myopic, greed and arrogance denied voters the choice. Now it is obvious that they’ve lost it big. What will they tell us? How come that our politicians are too scatter-brained this way? Aren’t they the same dudes who unearthed Richmonduli scandal that saw Luwasha packing? Again, did they think Luwasha forgave and forgot them to end up being their man? Interestingly, the same dudes we used to wrongly think were smart and meant business have proved how unscrupulous and ticklish they are.
Fourth, you can take this to the bank. Why didn’t they learn from the 1995 fall from grace for the NCCR-Ma-change? I tend to concur with Desmond Tutu, retired Archbishop of Pretoria who said, and “We learn from history that we don't learn from history.” Our opposition politicos seem to have done exactly the same.  For nifty politicians, even politicos, a blow August Lyato-nga Mremavu dealt NCCR would have opened their eyes not to be in bed with CCM’s cadre. I’m trying to imagine. If UKAUA had stuck to their guns –fighting for the New Constitution and accountability –how would Bongo’s political map would look like today? Take it from me. Had Dr Willy Silaha stood this time around, CCM would have been expeditiously heading for the purgatory.
I know after being defeated squarely, UKAUA will come with all sorts of hoo-has to calm down the situation. Again, what befell them is titanic by magnitude. Luwasha won his battles and wars against his nemeses by making them lick their own vomits. He goes home a happy man whose name will always appear along CCM’s landslide victory. So, too, he goes down as the man who sunk four used-to-be reliable parties.
I know for sure. All those noise makers we used to hear and believe from the media and opposition who were voted in will have nothing to say in the parliament. They became famous just because they were able to bark at CCM accusing it of the same sin they’ve now committed by words and acts. We now know that they’re preaching water and drinking wine, hypocrisy at its best. Such dudes won’t have any moral ground to attack their opponent on what they actually did openly as opposed to their opponents.  
Why did CCM win easily? First of all, it did not deny the fact that it is corrupt through and through. Instead, it turned tables against its indicters by showing how double faced they are. And this worked well. For, it appealed to the voters who wanted to punish those who used to dupe them claiming they’re against graft while they’re themselves corrupt through and through. CCM may be corrupt. But it is not two-faced like those who used to accuse it.
Before the general elections I made a goof thinking that Bongo will show other African hunks what democracy means. Poor me, I ended up pissed off after learning that our politics has become just as useless and hopeless as other African hunks whose presidents meddle with the constitutions to remain in power forever. Can we now laugh at our neighbours ruled by individual dictators while we’re ruled by a dictatorial party? Indeed, when Bongo politics becomes bongo-bongo and googly, it tends to become as useless as other African hunks.
Source: Guardian Nov., 1, 2015.

Magufuli: Kupambana na ufisadi anza na Kikwete

  • Tanzania ruling party names candidate for Oct. elections - Breitbart
Wahenga walinena: Jasiri haachi asili. Hapa jasiri ninayemuongelea si mwingine bali rais Jakaya Kikwete ambaye kuingia kwake madarakani kunasemekana kuwezeshwa na fedha ya wizi wa mabilioni ya Mfuko wa Madeni ya nje (EPA). Tokana na wizi kuasisiwa na kuhusishwa na wakubwa, hakuna aliyewajibishwa wala kulazimika kutoa maelezo hasa wakubwa husika walipotajwa wazi wazi. Rejea kukiri kwa mwanasheria Michael Bhindika aliyesimamia uhamishaji wa fedha husika ambaye aliwataja Benjamin Mkapa rais mstaafu, Philip Mangula (Makamu mwenyekiti wa CCM), Jakaya Kikwete rais anayeondoka na wengine wengi akiwemo kada maarufu wa CCM Rostam Aziz ambaye kampuni yake ya Kagoda ilitumika kuchotea fedha husika.
            Punde alipoingia madarakani, Kikwete hakuacha asili. Aliasisi kashfa nyingine ya mabilioni ya Richmond ambayo iliondoka na mabilioni ya wananchi huku ikijirudufu na kuzaa kampuni nyingine ya Dowan ambayo inaendelea kuwakamua watanzania mabilioni. Kwa mara nyingine, Kikwete na Aziz walihusishwa moja kwa moja kabla ya kumtoa sadaka swahiba na waziri wake mkuu, Edward Lowassa hapo mwaka 2008.
            Funga mzigo ya Kikwete ni kashfa ambayo anaondoka huku akiiacha ikiwa mbichi. Hii si nyingine ni kashfa ya Escrow ambapo maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Kikwete wakiwamo mawaziri wakishirikiana na  matapeli na majizi makubwa waliweza kuiibia serikali kwa kile walichosema ni kulipa kampuni iliyoingia nchini kinyemela chini ya uangalizi wa Kikwete ambaye anahusika moja kwa moja kwa vile ndiye alikuwa waziri wa wizara husika.
            Kama siyo kulindana na kuogopana, rais John Pombe Magufuli –aliyeahidi umma wakati wa kampeni zake za kugombea urais kuwa angewashughulikia mafisadi ambao alisema ni kikundi kidogo cha watu –basi angeanza na Jakaya Mrisho Kikwete na wenzake wanaojulikana. Na Magufuli hawezi kusema hawajui. Anawajua vizuri sana kwa sura na majina hata miradi yao ya kijambazi. Kama Magufuli atamgwaya mtangulizi wake ataishia kuonekana muongo na msanii kama wasanii wengine walioahidi wananchi Maisha Bora kwa Wote wakaishia kuwaibia na kuwasababishia maisha mabovu.
            Kikwete anapaswa kushughulikiwa vilivyo kwenye vita ya kupambana na ufisadi kutokana na kuhusishwa na ufisadi wa kutishwa katika kashfa tatu zilionyeshwa hapo juu. Pia Kikwete ana ushahidi mwingi kuhusiana na ujambazi, ufisadi na biashara haramu ya mihadarati. Rejea kukiri kwake kuwa ana orodha za majambazi, mafisadi na wauza mihadarati lakini asiwashughulikie kutokana na sababu anazojua mwenyewe.
            Ukiachia mbali Kikwete, kama Magufuli atatimiza ahadi zake –hasa hii ya kupambana na ufisadi –hata akina Mkapa na Ali Hassan Mwinyi hawatapona hasa ikizingatiwa kuna kashfa nyingi waliasisi na kushiriki kama vile kashfa ya kuuza mbuga yetu na kuua wanyama wetu kule Loliondo chini ya Mwinyi. Mkapa –ukiachia mbali EPA –anahusika na kashfa ya uuzaji wa kifisadi wa iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), na ubinafsishaji mwingine uliogeuka kuwa mzigo kwa taifa na wizi wa mali ya umma hasa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira ambao Mkapa alijitwalia yeye na familia yake. Pia mke wa Mkapa Anna, hatanusurika hasa kama kampuni yake ya Fursa Sawa kwa Wote ilivyotumia mgongo wa Ikulu kuliibia taifa. Sambamba na Anna ni Salma Kikwete ambaye naye kampuni yake ya Wanawake na Maendeleo imetumia mgongo wa ikulu kuliibia taifa na kulitia aibu.
            Hata zile nyumba za umma anazotuhumiwa kusimamia kuziuza Magufuli, anaweza kumtwisha Mkapa mzigo wake na kumchunguza ili kujitenga na uchafu huu na kutooenekana kama anawaogoopa wahusika kwa vile alishirikiana nao. Hapa bila shaka Edward Lowassa aliyekuwa mpinzani wa Magufuli hatanusurika hasa ikizingatiwa kuwa anajua mengi kuhusiana na Richmond ukiachia mbali kuwahi kuweka hatiani na Kamati Teule ya Bunge kwa kashfa hii naye akakiri na kuachia uwaziri mkuu.
            Japo ni mapema kuhukumu, wahenga husema: Kusema ni jambo moja na kutenda ni jambo jingine. Je Magufuli ambaye alimlaumu Kikwete wazi wazi jukwaani huku Kikwete mwenyewe akiwapo atakubali kuwa rais wa aina ya Kikwete ambaye wengi walimjua kama msanii na mtu anayeahidi bila kutimiza? Je Magufuli atawashangaza wengi hata wale waliomuunga mkono wakitegemea awalinde? Je Magufuli atawaangusha hawa wachache na kutowaangusha umma aliouahidi mara nyingi kuwa hatauangusha? Je Magufuli atajipiga mtama? Je Magufuli ataibadili CCM au CCM itambadili? Je Magufuli atausafisha mfumo au mfumo utamchafua? Maswali ni mengi kuliko majibu.
            Kitakachompa changamoto Magufuli ni ukweli kuwa kashfa hizi si mpya. Karibu watanzania walio wengi –hasa wafuatiliaji wa mambo –wanazijua kwa undani hata saa nyingine kuliko tulivyozieleza tokana na jinsi zilivyowaathiri na wengine walivyoona zikisukwa na kutekelezwa kiasi cha kuiba siri zake na kuzivujisha kwa upinzani na vyombo vya habari.
            Kwa vile Magufuli ameahidi mambo mengi yanayohitaji fedha nyingi, ni wakati muafaka kumkumbusha kuwa bila kuwashughulikia mafisadi papa na kuwafilisi ili kuwazuia kuendelea kuliibia taifa na kupata mtaji wa kukamilisha ahadi zake, atajikuta muda ukimpita kiasi cha kujikuta akiwa mwanachama wa kundi aliloahidi kupambana nalo ili kuwakwamua watanzania. Wakati wa kupambana na ufisadi ni sasa.
Chanzo: Tanzania Daima Nov. 1, 2015.