The Chant of Savant

Thursday 4 August 2011

Mke wa rais anapokuwa rais na kutenda kama rais!




Mke wa Rais Wa Serikali ya Jamhuri ya Tanzania na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake nchini WAMA Mama Salma Kikwete (kulia) akifafanua jambo wakati alipoongea na waandishi wa habari August 3, 2011 katika ofisi ya Taasisi yake jijini baada ya kumkaribisha mke wa Rais wa Burundi Mama Denise Bucumi Nkurunziza (kushoto) ambaye yuko nchini kwa ziara ya siku sita, (Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO)

Kwa wanaojua jinsi blog hii inavyochukia nepotism, watakumbuka tumekuwa tukiandika kulalamikia aina mpya ya ufisadi ambapo wake za marais wa kiafrika nao wamegeuka marais kupitia migongo ya waume zao. Wamegeuka wafanya biashara kupitia migongo ya NGO. Wamekuwa waheshimiwa kupitia waandishi habari nyemelezi wanaojipendekeza ima kwao au waume zao. Sasa naona wameongeza kasi kiasi cha kuanza kuwa na ziara za kiserikali kama waume zao. Je jinai hii ya matumizi ya urais kifamilia itaisha lini? Je wananchi wa kawaida wanaliona hili? Eti mke wa rais yumo nchi kwa ziara ya siku sita ili kufanya nini na kwa kugharimiwa na nani? Kesho utasikia ziara ya mtoto wa rais kabla ya kufuatiwa na ya mama yake, dada yake baba yake na upuuzi mwingine. Hata kama kuna wanaopenda na kushabikia mchezo huu, bado ni mchafu unaopaswa kupigwa vita kwa nguvu zote. Maana kinachochezewa ni ofisi na pesa vya umma. Kwa utajiri gani tunaruhusu israfu hii?

No comments: