The Chant of Savant

Wednesday 14 December 2016

Akina baba tusiwe kama baba Kamakl

Huu muziki ni wa kikuyu. Umetungwa na John Njagi na kuimbwa na binti ambaye jina lake halikutajwa. Muziki huu una somo kubwa kwa wanaume -tena watu wazima -wanaopenda kuharibu watoto wa wenzao.
Binti ameamua kumshitaki mzee mwenzie kwa baba yake ambaye ni rafiki yake. Anamwambia baba yake aende akamuonye mzee mwenzake kuacha kutaka kumharibu binti wa mwenzie.
Anamwambia baba yake
Baba Kamaki ni rafiki yako
Nilikutanaye juzi pale Kanunga
Nilikuwa nikitokea kanisani
Aliniita na kuomba namba yangu ya simu
Niliuliza ya nini wakati anaiona
Alijibu ana jambo moja anataka kuniambia.

Aliniita kwenye baa na kutaka tupendane
Alisema akiniona hujihisi vyema
Nilishangaa sana

Mbona mke wa baba Kamaki ni mama mwema?
Mbona rafiki yake mama toka shuleni?
Baba Kamaki ni baba choyo
Kichwa kimejaa mvi
Lakini anataka kuhangaika na vitoto

Baba nenda kamuonye
Kwani si rafiki yake
Nilikutana naye akiendesha gari nzuri ya toto
Aliahidi angeninunulia moja
Hata anunue meli hanipta
Ashindwe kabisa.

Siwezi kutafisri wimbo mzima. Hiyo ndiyo faida niliyoipata kuishi Kenya kwa miaka mitatu ambako nilitia bidii na kuondoka na lugha ya Kikuyu.

Hata kama hujui lugha, unaweza kusikiliza na kuburudika angalau baada ya kukupa kwa ufupi ujumbe mkuu na mahsusi wa wimbo husika.

No comments: