The Chant of Savant

Thursday 16 April 2020

MASHABIKI WA UZAZI WA MPANGO ANGALIA MAANGAMIZI HAYA TOKA NCHI ZA MAGHARIBI


Tumekuwa tukiaminishwa kuwa uzazi wa mpapngo ni njia bora ya kuendelea kama nchi. Ukweli ni kwamba wabaguzi wa magharibi wanatafuta namna ya kupunguza maskini na wale wanaowaona hawafai. Tafadhali fuatilia kisa hiki ujue lipi la kushika na lipi la kuacha. Waafrika wanapaswa kuchukua tahadhari kuliko wengine kwa sababu kuu mbili:
Kwanza, hawatakiwi tokana na rangi yao. Hii si kwa wazungu tu bali hata waarabu, wahindi, wachina na kila anayejiona kuwa mweupe na hata wenzetu waafrika katika baadhi ya nchi wanaojiona kuwa si waafrika bali waarabu au vyovyote vile wanaojihisi kuwa bora.
Pili, wanataka tuishe ili wachukue bara letu na kufaidi mali asili yetu tuliyojaliwa. Hizi ndizo sababu kuu japo kuna nyingine nyingi kama vile kututumia kufanyia majairibio ya madawa kwa ajili ya kutibu wale wanaojiona wako bora kuliko sisi. Kwa wenye akili na kuona mbali, hawakubali mauaji haya ya kishenzi. Kwanini tuambiwe tuzae wangapi wakati tuna uwezo wa kujilisha na kujiendesha kama hatutaendelea kujidanganya kwa kuwa tegemezi, ombaomba, kopa kopa na wafisadi? Hapa ndipo hoja ya rais Magufuli kuwa akina mama wazae ina mashiko ikilinganishwa na watu kama Bill Gates hapa chini.


No comments: