The Chant of Savant

Monday 6 April 2020

Je Mwanzo wa Mwisho wa Ndoa ya Seif na Zitto umefika?

Zitto's party stirs up Tanzania, but is the honeymoon about to ...

Kwa wanaojua historia ya Maalim Seif Sharif Hamad na Zitto Kabwe, hata tabia zao, hawashangai haya anayosema huyu Yeremia Kulwa Maganja ambaye aliyekuwa kaimu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, kiongozi wao aliyewachomoka. Kwa wanaojua ajenda binafsi na ithibati ya wahusika, hatashangaa wala kutia shaka maneno anayosema huyu bwana kwenye uzi huu. Je kwa kinachoanza kujifunua hapa ni nini, mwisho wa mwanzo wa ndoa ya Hamad na Kabwe umeanza au ndo siasa? Je nani anatamchuuza mwenzake? Who is using whom? Waingereza huuliza. Kwa uzoefu wa uharibifu, Hamad ana kila sababu ya kuchekelea. Hata hivyo, itategemea. Baada ya kumfukuza na kumpoka chama marehemu James Mapalala––asijue aishie kwa upanga hufa kwa upanga––akaishia kufanyiwa hivyo na profesa Ibrahim Lipumba. Yeye si wa kwanza wala wa mwisho.  Jacob Zuma, rais wa zamani wa Afrika Kusini alimpokonya madaraka Thabo Mbeki na kumfurusha kabla ya kumaliza muda wake. Je Zuma aliondokaje madarakani na yuko wapi kwa sasa? Zitto alijaribu kufanya awezavyo kuipokonya CHADEMA akaishia kuchomolewa mwenyewe. Je nani atamchomoa mwenzake hapa kati ya wanjanja hawa wawili? Je ni nani ataondoka na kicheko au kilio kati ya wasaka madaraka hawa? Hata hivyo, kutokana na historia ya uzoefu wa wawili hawa, ni rahisi kujua nani atacheka na nani atalia. 

No comments: