Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Thursday 29 August 2024

TUKUMBUKE ZAMA ZILE NA MAMA MIA YA SAHLOMON



Ni CcM policy au geshi la polishi?


Katiba ya mafyatu inatoa haki na uhuru kwa kila fyatu kukutana na fyatu yeyote unayemtaka kutembea au kuandamana na unayemtaka kwenda unakotaka kusema unalotaka imradi usivunje sheria ya kaya ambayo nayo siyo maagizo au mapenzi ya ndata na wanaowatumia tena vibaya. Unapozuiwa kufanya hayo hapo juu na mengine kama au kukaribiana nayo, anayefanya hivyo havunji sharia tu bali katiba yetu virakaviraka ya mwaka 47. Kisharia, bila kujali cheo au sura ya yeyote, anayezuia uhuru wa kikatiba ni mhalifu sawa na wahalifu wowote.

 Kikatiba, haki na uhuru tajwa hapo juu siyo utashi wala hisani toka kwa yeyote hata awe mnene kiasi gani. Kaya ya mafyatu hutawaliwa kikatiba na siyo kichata wala kichawa. Uhuru ni haki ya kila fyatua. Msigeuze uhuru kuwa udhuru. Mbona mkipiga njuluku au kuzitumia vibaya Hamshikwi na kuswekwa lupango? Mbona mkipiga mnada kaya hamshikani, kufungana, hata kuswekana lupango?
            Mbona mafisi na mafisadi walioingia mikataba inayoanza kututokea puani hawakamatwi au ndata hawawaoni au wanawaogopa kwa vile wengi ni wanene au makuadi na washirika wao? Mbona tunawaona wakipeta na wengine hata kupewa ulaji zaidi ili wavimbiwe wafe, au kuna namna?

Wako wapi waliouza bandari, maji, na hata hewa? Wako wapi walioingiza madudu kama Buzwagy, Mwanakaya, IpTL, Kagoda, Eskorow, waliochoma banki yetu kuu na wengine wengi waliokwisharejesha namba? Kwani mtaishi milele kumbaff nyie?

Leo, tena kwa hasira na kifyatu, nitafyatua sakata la kuwadaka na kuwatia adabu viongozi wa upingaji. Japo mimi si wakili wao wala sitaki kujifanya kuwa, kwani wapo kisheria au kihiari? Je siasa ni haki au hisani? Hamjui kuwa maulaji yana mwisho? Wako wapi waliowabia kura za kula, wengine kuwapoteza mbali na walionusurika mitutu? Si wameyaacha maulaji na kutokomea kwenye kaburi na sahau? Hamuoni maulaji yaliyowahangaisha sasa yanaliwa na wengine tena ambao hawakuwa na nchango wowote zaidi ya unafiki na ufichi?

 Nashauri maulaji yasituchoganishe na kutufanya kunyatuana roho, kudhalilishana, na kutesana bure. Duniani tunapita. Kwanza, maulaji yenyewe ni ya mafyatu ukiachia kuwa ni ya muda. Kuepuka udhalilishaji, ukandamizaji hata uonevu, basi futeni vyata vya kisiasa na kusajili geshi la polishi kama chata cha siasa muone, maana limekosa kazi mbali na kufanya kazi za kisiasa na siasa za visasi na kutumika hovyo. Japo sipendi wala si mwanasiasa, napanga kuingia kwenye siasa ili nikomeshe siasa za visasi. Kwa nilivyo gwiji na nguli mwenye ushawishi, naamini nitabadili upepo wa kaya kisawasawa na kufanya kiumane nchana kweupe. Nashangaa. Tunaambwa vyata vipo kikatiba, vinapiga ruzuku mbali na kelele halafu vinakandamizwa. Basi, tangazeni kaya ya chata kimoja tujuwe na muone watasha watakavyowawashia moto na kuwanyima misaada japo Uchumi mnao lakini mnaukalia kama alivyowahi kusema mzee Nchonga (RIP sana tu).

Kila uchao mafyatu wanatekwa na kuibiwa. Ajabu hakuna ndata wa kuwalinda au kuwashukia wezi. Ajabu ya maajabu, magari ya wagonjwa na madawa hakuna wala njuluku ya kuajiri matibabu ila ipo ya kununua mibomu ya kutoa machozi, risasi, virungu, na zana nyingine za ghasia! Vitegemezi vya makapuku vinakaa chini na kukosa maticha ilhali ndata wanatesa! Hata nao hawajitambui. Hawa wanaowadhalilisha na kuwatesa ni ndugu zao hata kama hawawataki wala kuwaheshimu na kuwajali. Msitupeleke Bangla--- ambako mama alitemeshwa ulaji baada ya kulewa maulaji na kujisahau akayafanya kuwa urathi wa kifalme asijue hajui kuwa hajui.

Nani aliwachagua nyinyi na kuwapa power na utashi ya kukandamiza wenzenu wanaofanya usanii kama nyinyi? Tangu tunyake udhuru, sorry, uhuru, mmefanya nini cha maana zaidi ya kujihudumia kwa migongo yetu? Leo hii bei ya kila kitu imepaa huku wanene wachache wakitanua na kutapanya kama hawana akili nzuri. Mnataka tunyamaze au kupongeza wakati tunaumizwa na kudhalilishwa?  Kwani mafyatu hawajui wala kuona?

Zamani nikirejea toka kuutwika, lau, nilikuwa na jeuri ya kuwaletea vitegemezi pipi. Siku hizi, narejea home kwa kujificha kama mwizi ili vitegemezi visinione na kutaka zawadi. Ni maisha gani usawa huu wa karne ya sayansi na tekelinalokujia? Wanene wachache wasiojali mafyatu wanazidi kuongeza nafasi za ulaji hata zisizo kwenye katiba kama ule wa Dot p’Bitek, waziri mkubwa mdogo. Kwani hatujui wala kuona? Nawashangaa hata wanasharia wetu. Kwanini msiende kwa pilato na kuzuia israfu hii ya wazi au hamuoni? Lo! Nimepayukaje? Nimesema eti cheo cha p’Bitek ni unconstitutional au? Hayo tuyaache. Wajinga ndio waliwao. Mwalimu wangu usinibaini. Nikipata kumi tano zako. Hiv ndata wanaoatwanga wapinganji wanakumbuka viapo vyao? Ikitokea wanaowachapa wakaukwaa unene watakuwa wageni wa nani? laiti wangejua kuwa kazi ngumu ni kupanda na siyo kushuka! Wangejua hili, wangefanya wafanyayo kwa haki na tahadhari. Ngoja nikapate kanywaji nipate usingizi na kuepuka makelele ya yule kiumbe ajifanyaye ananipenda. Nimesemaje?

Chanzo: Mwananchi Jumatano iliyopita.

Unapochagua Mchumba Jua na Zingatia Yafuatayo

Kuoa au kuolewa, au kuoana kama wasemavyo siku hizi, si suala la kukurupuka au siku moja kama kununua tiketi ya bahati nasibu au kukodisha taxi. Katika kuchagua mwenza wako (wa maisha au vinginevyo kama hamtafanikiwa), unapaswa uwe makini tena sana. Usikurupuke kuamua kuingia uhusiano ambao una mwanzo lakini hauna mwisho isipokuwa kifo hasa kwa wale wanaofunga ndoa za kikristo (hata walio kwenye ndoa tofauti wangetamani iwe ni ‘kufa na kuzikana). Hivyo, ni muhimu kumjua mwenzako kwa madhaifu na ubora wake. Lazima uwe na orodha ya vitu ambavyo ungependa mwenze wako awe navyo kama vile umri, atokako, tabia, urefu, uwezo wa kufikiri, mvuto, mengine mengi kulingana na utakavyo bila kusahau kama nawe unavyo au unapimwa hivyo. Kama ilivyo kwenye kujenga nyumba au kununua gari, lazima ujue ukubwa hata muundo wa nyumba. Kama ni gari, ungependa kujua aina, ulaji wake mafuta, nguvu (horsepower), rangi, mwaka wa kutengenezwa na hata ubora na udhaifu wake.

            Kwa vile ndoa ni taasisi unaoingia kwa sababu za upendo na uhuru wa kuchagua, siyo sawa na kuzaa watoto au kuzaliwa. Wazazi hawachagui watoto wala watoto hawachagui wazazi kwa sababu hawana uwezo wa kufanya hivyo. Kwa upande wa ndoa, una chaguo huru ambalo likishafanyika, huodoa uhuru huo. Hivyo, unapaswa kuwa makini, mvumilivu, na mwelevu kufikia kusema I do.

            Tofauti na gari na nyumba, ndoa siyo mali yako binafsi. Ni mali ya jamii hasa kwa jamii za Kiafrika ambapo familia za pande mbili huanza machakato na hatua mpya ya uhusiano wa karibu usio na mwisho vinginevyo ivunjike japo si lengo lake. Hivyo, tofautisha kumchagua rafiki mnayeweza kufarakana na kuamua kuvunja urafiki. Ndoa ni zaidi ya urafiki maana, rafiki hana haki kisheria kumrithi au kumrithisha rafiki yake mali zake pale inapotokea kufariki. Tofauti, mwanandoa anakuwa na haki hata zaidi ya wazazi na ndugu kwenye kukumilki wewe na mali zako. Hivyo, huyu si mtu wa mchezo au wa kukwapukia. Siyo mchezo wa pata potea wala kamari bali jitihada makusudi zinazolenga kujenga uhusiano wa karibu katika maisha yenu yote. Hakuna anayefunga ndoa anayeomba au kutegemea ivunjike japo nyingi zinavunjika.

            Katika mila za Kiafrika, ndoa huwahusisha wazazi, ndugu, na jamaa katika kuanza kuijenga, hata wakati mwingine kuimboa na hufanya familia mbili tofauti kuwa moja. Familia mbili uhusisha familia nyingine nyingi ambazo hazikuhusiana kabla kuingia katika uhusiano usio na mwisho japo una mwanzo. Ndiyo maana tuna washenga, makuwadi, na wengine wengi tunawaowahusisha kwenye kuanza msingi wa ndoa ambao, kimsingi, ni watu wa karibu na wanaoaminika walio karibu nawe kwa uhusiano wa damu ambao, mara nyingi, huteuliwa na wazazi wetu tokana na ukaribu na imani yao kwao. Hii ni kutokana na wahusika kuwa na uzoefu wa muda mrefu mbali na ujuzi ambao huchukua miaka mingi kuupata.

Tunadhani utaratibu huu ndiyo uliowawezesha wazazi na mababu na mabibi zetu kutokuwa na talaka kwani ulikuwa siyo shirikishi tu bali wenye umakini zaidi katika kutafuta wahusika wanaofaa na kufaana tokana na walivyowajua. Kwa Waafrika hata neno talaka ni la kigeni litokanalo na lugha ya kiarabu iliyoleta Uislam. Kabla ya hapo, hatujui dhana hii ilivyotafsiriwa. Japo talaka zinatolewa, huwa si jambo la kufurahisha wala kutamani liwepo ukiachia mbali kwenye zile ndoa ambazo ni rahisi kuoa na kuacha kulingana na misingi na taratibu zilizojiwekea.

Kumalizia, bila kuzama zaidi kwenye mada tokana ufinyu wa nafasi. Wanyama hawana send offs, vyeti vya ndoa wala mikataba yanayojulikana kwa binadamu, wana dalili zinazoashiria thamani ya ndoa ikizingatiwa na maarifa ambayo binadamu ameyachota kwao, lina mashiko au ghorofa bila kuangalia kichuguu? Hii ni elimu mwanadamu aliyoipata toka kwa mwalimu mchwa. Kama tukubalivyo kupata ujuzi huu toka kwa mwalimu huyu, kadhalika tukubali na ukweli juu ya taasisi hii ya ndoa toka kwa viumbe mbali mbali waliotuzunguka.

Chanzo: Mwananchi Jumapili iliyopita.


Wednesday 21 August 2024

Hongereni Mafytu Kumpenda Mama

Mwanafalsafa’ maarufu wa Uganda, alhaj, Doktari, field Marshall, profedheha Idi Amin Kaidada  Oumee aliyepata elimu yake mtaani aliwahi kusema kuwa lazima watawaliwa wawapende watawala bila kujali lolote au wanawatenza vipi. Lazima wawasifie hata wakikosea. Wawachekee hata kama wanapaswa kulia. Wawaabudu ikibidi hata kama wao si Mungu. Kwani, kufanya hivyo, huleta ‘amani na maendeleo’ hata kama kuna kero. Kwa kuzingatia ushauri huu wa kitaalamu wa fyatu aliyewafyutua waganda akataka hata kutufyatua kabla ya JWTZ kumfyatua na kumg’oa, mafyatu juzi walionyesha upendo usio kifani. Si walimnunulia maza chopa kwa ajili ya kuivinjali kaya yake tukufu. Ni jambo la kupigiwa mfano na kumshukuru Mungu aliyewapa moyo wa upendo.
            Dunia hii we acha tu. Si walijitokezea wenye wivu tena wa ki-female wakaanza kusema eti ni hongo na kielelezo kuwa kutakuwa na uchakachuaji. Maana, wanasema tena bila aibu kuwa mafyatu waliomnunua chopa, kwanza, wamepataje njuluku na wanategemea kuzirejesha vipi. Wanasema. Akishafyatua ulaji, nao watamfyatua kwa kutaka alipe fadhila. 
        Wanahoji kwanini wasinunune ambulances za kubebea wagonjwa. Au ni yale ya ndata kuwa na ndiga wakati wagonjwa hawana? Hayo si yangu.
        Wafyatuane au la, hayanihusu. Muhimu wasinifyatue na mafyatu wenzangu. Je kama ni kweli kuwa huku ni kufyatuana kunakolenga kulipana fadhila, mafyatu tutanusurika wakati kaya itakayofyatuliwa ni yetu? Je tutakubali kufyatuliwa na hawa wanaofyatuana ili watufyatue? Je tutawafyatua kwa kutowapa kura ya kula ili wasitufyatue au tutafyatuliwa mkenge? Niliwahi kuwadokezea mafyatu wa upingaji walivyowahi kuhoji tukutuku zilizosambazwa nkoani wakisema kuwa bi Nkubwa anawahonga watendaji. Walihoji alikopata hii njuluku tena mabilioni, ananunua, nani, nini, na anategemea kupata nini. 
        Kwa vile mie siyo mpingaji wala muungaji au msifiaji bali mfyatua, natimiza wajibu wangu wa kufyatua bila kuwaudhi wanene ambao hata nikiwaudhi hawana grounds au locus standi kwa lugha ya kisharia, kunifikisha kwa pilato. Hii jamani nayo ni sanaa. Ukiona umefyatuliwa, huna haja ya kunichukia au kulalamika bali kujirekebisha au kufyatua kijanja. Hayo tuyaache. Mibangi hii! Sasa naanza kufichua siri!
            Turejee kwenye ununuzi wa chopa na umuhimu wa watawala kuwapenda watawaliwa hata kama wanawaponda au kuwafyatua.             Kwanza, ni jambo bora kumchangia mama kipenzi kuliko kuwapa njuluku matapeli wa kidini wanaotoza njuluku eti kutoa maombi aka huduma wakati ni huduma. 
        Juzi nilimsikia jembuz mmoja toka kaya ya jirani anayejiita kiboko ya wanga wakati naye ni tapeli wa kawaida. Hivi inakuwaje kaya yetu inageuzwa shamba la bibi tena mwenye kipofu? Kwanini mnaruhusu matapeli tena wenye mtindio wa mawazo na wavivu wa ubunifu kuja na kuwafyatua mafyatu wenu mliowasikinisha na kuwajaza ujinga na kukata tamaa hadi wakaamini kila upuuzi? Au hao nao wanawasaidia kuwafyatua kwa sababu wanawaaminisha mafyatu wachovu na wavivu wa kufikiri kuwa ukapuku wao ima ni kazi ya muumba au wachawi?
         Sijawahi kujua kwanini mafyatu wetu wamekuwa wa hovyo hivi. Hivi, kweli kwa anayejua umaskini waliotegeneza akina Mobutu, kuna la maana unaweza kupata kwa jamaa hawa mabingwa wa utapeli sawa na wale kutoka kwa akina Buhari ambao ujanja wao ni utapeli tu na siyo ubunifu wa maana? Nasikia siku hizi kila tapeli anatumia gea ya kuwowa mabinti wa kidanganyika wasiojua hili wala lile ili kuishi kwenye kanani ya Afrika chini ya mama kipenzi.             Mtaachwa Solemba. Hawa jamaa wakishapata wanawaacha na vitegemezi vyenu kiasi cha kugeuka wajane bila kufiwa. Kuna haya ya kuanzisha safu ya kuwaelimisha mabinti zetu waache kushobokea wageni wasijue hakuna la maana zaidi ya kuwa visa za kuishia kayani. Huku Ulaya ni jambo la kawaida. Wanachotuzidi watasha ni kwamba waswahili wanaotaka kuishi hapa kwa gea ya kuoa, lazima watimize matakwa ya wadada wa huku na kugeuzwa mashine ya kunonihino. We! Koma. 
        Wapo wengi wananyonywa sawa na mabinti zetu wanaonyonywa na hawa matapeli uchwara. Hali ni hiyohiyo bondeni. Nakumbuka mwanamuziki wa kwaya aitwaye Debbie Fraiser aliyeingizwa mjini na tapeli toka kwa akina Buhari na kumharibia maisha hadi kunyotoka roho.  
        Mna habari kuwa hata Brenda Fassie aliponzwa na matapeli haya? Fumbueni macho ya mabinti zenu waache kutumika kama ilivyokuwa zamani ambapo vijana wengi wa kibongo walibebeshwa miunga na kuishia kufungwa na kugeuzwa mashoga kwa tamaa na ukumbaff wao.
        Kimsingi, kumnunulia mama kifaa ni ushahidi kuwa mafyatu wanampenda kama siyo kufyatuliwa na baadhi wenye ukwasi ili wamtumie. Pia, inaonyesha kuwa si mafyatu wote ni mataahira wa kuibiwa na kila tapeli kama yule jambazi toka kwa akina pedejee wanaokuja na kuwaibia au waganga wa kienyeji wanaowaibia wakidai wanawasaidia kutengeneza utajiri wakati wao ni maskini wa kunuka.
        Tumalizie tukiwapongeza mafyatu na kuwashauri wawe macho kuona huu mchezo utaisha vipi nani atamfyatua nani na nani atazembea akafyatuliwa. Hivi nimesemaje? We koma.
Chanzo: Mwananchi leo.

Thursday 15 August 2024

Nashauri Kununua Majenereta Kuendeshea SgR


Baada ya kuwafyatua kwa SgR kufanya majaribio, nilionya kuwa safari zingeanza pindipo mwana wa Adam­­­––––yule fyatu wa kiyahudi anayeabudiwa na mafyatu wengi duniani hadi wenzake mafyatu wanasema kwanini tusiwaabudie wote wakati hawana lolote zaidi ya mikwara na kuiona bora kuliko wengine wakati ni hovyo–––akirudi si waliamua kunifyatua na kujifyatua na kuanza majaribio. Nikiri. Nilikosea. Juzi mtukufu mpendeka, msikivu, mwenye maone, Doktari rahis Mama alizindua safari za mwanzo. Je hizi safari zinazopigigiwa upatu ni endelevu na fyatu au danganyifu? Wale wanaoelewa nilichofyatua, wako wanafyatua maandalizi ya kuja kwa njemba hii iliyopumbaza wengi kuwa iliwaokoa wakati iliwatonya kuwa kila fyatu atabeba furushi lake mwenyewe siku ile ikifika. Chonde chonde, wale makanjanja wenye uroho wa kiroho msianze kuwafyatua na kuwachuna mafyatu zoba yanayoamini kila kitu hadi wanaitwa kondoo na kuchungwa na wachunaji wanaoishia kuwachuna na kuwasikinisha wakijiona kama mataahira. Yangu mato.
        Gwaijimmy, Katortoise, Gamanyie, Mwakasegie, Lusekelelo, Godavie, Muingirer, Mwamposer, Mutalemewa, na matapeli wachunaji, sorry, wachungaji mnanipata? Yaani hamuoni ni dhambi kuwafyatua mafyatu wasio na hatia bali ukumbaff na kukata tamaa? Je mnajua yaliyoibuliwa kuhusiana na mwenzenu Tii Bii Joshuer, beberu fyatu aliyefyatua watumishi wake njuluku hata uroda? Mnamfyatua nani wakati soon mtafyatuliwa na God mnayemtumia kuwafyatuliwa na kuwatapeli mafyatu majuha? Mshajiuliza, mkizeeka na kukaribia kufyatuliwa mtafyatua nini lau kuepuka kuingizwa motoni hata kama hamuamini kuwa moto upo?
        Kwanza, sijui kama hawa walioamua kunizodoa kwa kufyatua kiini macho wana umeme, uaminifu, utaalamu, uwajibikaji, na uzalendo vya kutosha kunifyatua kwa kufanya kweli kabla sijaja na fyatuafyatua na zomeazomea zaidi hadi kuwafyatua mafyatu wakawafyatua tofauti na mlivyotegemea wala kuotea. Basi, ngoja niwafyatulie kweli. Mnaweza kujimwabafy kuwa bwawa la Mzee Mchonga limeanza kufyatua umeme msijue watendaji wetu uchwara wanaweza kulihujumu au kuzembea kikaumana tena. Jikumbusheni jinsi bundi na ngedere walivyoifyatua SgR juzijuzi.
            Hivi tunakosa umeme tokana na kukosekana umeme au ubunifu na uzalendo wa kutunza miundumbinu yetu mbali na lisrikal kupenda kutumia umeme tena hovyo bila kulipa ukiachia mbali kuwa linapigwa njuluku kila siku na linabaki kutoa mimacho kama panya aliyefyatuliwa na ntego? Huwezi kutegemea mambo yaende kisayansi na vyedi wakati wahusika wanaishi kwa kujikomba, kusifiana, hata utopolo bila kuchapa mzigo. Huwaoni? Kila anayeongea utamsikia “napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu yada yada yada… na ukumbaff kibao.’ 
            Anaendelea “pia, napenda kumshukuru mno na sana bila kukoma wala kukomaa mtukufu, mpendwa, mpenzi, mwenye mapenzi yasiyomithalika kwetu hata kuliko mshirika wake wa bedroom, mwenye masikio makubwa na asiye na mdomo, asiyejivuna hata akijivuna, doktari, profesa emeritus, al- hajat, ustaadha, sheikha,  sayidat rahis yada yada yada na pumb’a kibao.” Unategemea mafyatu kama hawa wasiojiamini, wanaodanganya, wanaodanganyana, na kusifiana badala ya kufyatuliana ukweli wanaweza kupambana na tatizo kama hili linalohitaji umahiri, ukweli, na weledi bila kusahau ufyatu?
            Hapa tunachoona ni kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kufyatuana kwa kusifiana kwa sababu tunapenda kusifiwa na kuabudiwa. Mie mafyatu wangu, pamoja na kujua ni daktari wa kweli na siyo hawa madoktari wa heshima, niliwapiga marufuku kuniita daktari. Ndiyo maana hata kwenye uga huu huoni udaktari wangu tena usiofeki kama wa akina au wa kuzawadiana au wa kununua kama wa akina Gwaijimmy na matapeli wenzake. 
            Kesho mtasikia na waganga wa kienyeji wakiitwa doktari hata maprofesa! Hata hivyo, kama maprofesa wenyewe ni akina wa jalalani, tutegemeeni? Tokana na uzoefu wetu, kufyatuliwa, kuanza safari na kufanikiwa ni vitu tofauti. Kwa vile kaya yetu ni ya majaribio, wanaweza kufanya majaribio hata milioni. Je lengo la kuzamisha matrilioni ya madafu kwenye mradi huu ni kufanya majaribio au kufanya kweli? Je hizo njia zilizojengwa na makandarasi wa kutia shaka, zinaaminika na zina thamani sawa na njuluku tunayopigwa baada ya wanene wachache kula dili? Je tatizo hapa kama ambavyo imekuwa, ni nini kama siyo wanene wetu?  Kesho umeme ukigoma, tutapigwa kwa kisingizio cha kununua portable jenereta za kuzalisha umeme wa SGR. Unacheza na kaya hii sanii siyo?
        Najua mafyatu wengi hawakuambua. Niliposema majaribio nilimaanisha majaribio ya kufanya kweli siyo kutuonyesha vichwa viwili vitatu vya treni na kuminya. Narudia, hili halifanyiki na kufanikiwa hadi mwana wa Adam arudi. Atarudi lini? Msiniulize. Kawaulize wao. Pia, hakuna haja ya kuchukiana maana mie si wa kwanza kutoa ahadi hii. Atarudi kweli au la? Nani anajua wakati wote mtakuwa mmeishafyatuliwa na kulala milele bila kujua ukweli mchungu yote ilikuwa fumbo la imani la kuwafyatulia mafyatua wasifyatuane kinyama. 
        Naona yule anatikisa kichwa na kufyatua midomo kwa hasira. Huna haja ya kunichukia. Simpo, anapofyatuka fyatu na kurudi kwa mfyatuaji wake huwa si mnasema uilaze pema roho yake milele baada ya kumuweka kwenye makazi yake ya milele. Unajua maana ya milele? Hivi safari za majaribio zimefikia wapi na zimefanikiwa au kukwama kiasi gani? Je usafiri wa kweli utaanza lini, maana kwenye mitandao sioni kitu tena? Basi, jiandaeni kununua majenereta kuendeshea SgR. Vipi mafuriko Bwala la Mwl Mchonga? Du! Kumbe napanga kuwasaka bundi na ngedere niwatie adabu!
Chanzo: Mwananchi jana.


Thursday 8 August 2024

FYATU MFYATUZI: Ukweli nchungu kuhusu uchaguzi wa mwaka 2025


Nikiwa kwa akina Nshomile, wapo wachionjiua wala lengo langu. Nilipochema ukweli walidhani namwaga ntama kwenye kuku wengi baada ya kuchoshwa na dhuluma wanaona kama ulijifanya nshomile. Kuna mmbea mmoja kanitonya eti nilikuwa nimepewa ka-nshomile nilikolala nako kakanizingua nikafyatuka na kufyatua niliyofyatua nikasahau kuwa ningewaudhi wengi hacha wanene wa chata wanaotaka chacha nifyatuliwe wachijue chi vizuri.                                     Kilichowakosha mafyatu ni kufyatuka na kufyatua ukweli, sorry, upupu ulioacha Chama cha Mafyatu (CcM) hoi japo hai. Wapo wanaozusha eti nilikuwa amefyatua lubichi, kimpumu, gongo, na waragi toka UG. Wapo waliochema eti nilivuta chigara kubwa chiku hiyo ikanifyatua nifyatuka hadi kufyatuliwa. Wangejua kuwa hata juichi huwa chinywi kwa kuogopa inaweza ku-ferment ikanifyatua, wachingefyatua wanayofyatua. Hata kama nilipata kanywaji wao yawahuchu nini? 
Hata kama nimefyatuliwa, najivunia nilivyopayuka, chorry, kufyatuka wachijue mie ni Fyatu Mfyatuzi aka Mpayukaji Mchemahovyo zamani kabla sijabadili dini na kuwa na dini ya Mwananchi hadi nikapewa chafu hii. Nimechemaje? 
            Chiogopi wala kuchononeka. Hii kwa kimakonde huitwa collateral demage. Chijali. Ukifyatuka ukafyatua lazima ufyatuliwe. Kamuulize mhariri wangu. Chamtaim, hutaka kunifyatua. Huwa tunayamaliza kichikaji. Hivo, pliji, don’t take me chiriyachili. Hayo tuyaache njomba.
             Eti wanashangaa Nilivyochema eti kwenye uchakachauaji ujao, kama kawa, kutakuwa na upigaji halafu wahuchika watatubu na kuomba Chir God awachamehe. Kwani chili? Hawajali mafyatu watafanya nini? Wanadai eti ninawaona mafyatu kama hamnazo kama mie wanayedhani eti china akili na ujachiri mkubwa chana wakati nimeonyesha wazi nilivyosheheni kwangu. Nilimchikia mmoja akiniita mkumbaff achijue ukumbaff mwingine unalipa njomba. Kama unafanya ukumbaff unachinda, shida iko wapi? Kwanini nao wachifanye ukumbaff huo huo kuwazuia na wakachinda?
Nawachangaa wanaonichangaa na kunitukana. Mbona yupo waziri aliyechema eti chichi tunakopa kwa vile tu matajiri wakati raichi anachema anadhalilishwa kwa kukopa na hakuchukuliwa hatua? Mbona yupo aliyetengeneza uhaba wa chukari na bado anatecha? Mbona hata aliyetuhumiwa upigaji Mirerani amepandishwa cheo?
Zifuatazo ni chababu kuntu za kujipongeza:
        Fechiti, najua wengi hawanijui. Hii ni chiri uchiwambie hawajui nimerithi ujachiri wa dingi wangu? Mara nyingi wengi wakiniona humwaga chozi. Maana ni kama huwa wanamuona njomba kanali Mucha mwenyewe baba yangu mzazi.
        Chekandi, napenda ukweli na uwazi kama njomba Ben Nkapa. Hii ni achili yetu. Kuchema ukweli njomba. Nadhani huko Njomba Nkapa alipo atakuwa anafurahia kaburini mwake.
        Three, japo mimi chiyo chehe, nimetabiri vizuri kuwa Chichiemu itashinda hata kama ni kwa goli la mkono kama ilivyotokea 2015 nilivyotabiri bila kukochea au kupitia nje ya chanduku la kula kama ambavyo itatokea mwakani. Nani hajui hili japo wengi tena wanene wanaficha? Hawajui kuwa mie chiyo ntu wa utani utani!
        Nne, nimethibitisha kuwa ni gwiji la hichitoria. Rejea zilivyokuwa zikifyatuliwa kula za kura kama nilivyowahi kuchema kuwa ni goli la nkono. Naamini hii itarudiwa uchawa huu ambapo mnachema mitano tena kwa maza. Kwa wachio kujua nawachauri warejee hichitoria. Nakumbuka kicha cha kule Ntama ambako mshindani alipotea kabla ya kurejesha fomu nawe tukapeta? Nani hakumbuki kuwa hata aliponyatuka Mwendaze nilichema eti Mungu kaamua ugomvi? Hawa nazani wamechahau au wanijui au wanajifanya kutonijua. Wanachahau kuwa niliwahi kuchema kuwa huwezi kuchonga kinyago halafu kikakutisha. Chijui kinyago ni nani hapa.
        Tano, kama ushauri wangu utazingatiwa, tunaweza kuokoa njuluku ambazo zimekuwa zikipotezwa kwenye uchakachauaji ambao matokeo yake hujulikana hata kabla ya kufanyika kama ilivyo kwa majirani zetu wa Rwanda na Uganda. Kwanini kupoteza njuluku wakati tunacholipia ni kujitia hachara na kinachotakiwa kinaweza kupatikana bila kutumia njuluku. Bahati mbaya, wanaokulaumu hawalioni, kulijua, wala kulikubali.
        Kabla ya kumaliza, ngoja nimguchie pia rafiki na mshirika wetu Mgoshi wa Bumbui. Naye alifyatua maulaji hadi yakamfyatua akafyatuka kabla ya kufyatuliwa. Chijui mzee wake anajichikiaje chacha. Maana, aliwahi kututambia kuwa vitegemezi vyake vina akili chana na lazima kuteuliwa uwaziri achijue kuna na kutumbua aka kufyatua. 
Chijui huyu naye chiku hiyo alikunywa kanywaji gani hadi kuchema eti hawampendi mtukufu raichi doktari mpendeka. Tate nane tate nane.                         Niliwaonya kuwa kuchifia kupita kiachi chaa nyingi hupitiliza na kuchababisha kukufuru kama huyu aliyemponda maza wakati alikuwa akijionyesha kuwa anampenda. Nadhani mlichahau mlilvyotumbuliwa na Mwendazake akawachamehe na akafyatuka mkaendelea kumchengenya. Hayo tuyaacha. Nangoja kuona wengine kama wale wa walitengeneza uhaba wa chuga, wenye kachifa za mirerani japo naona wengine wamepandishwa, na wale wote wachiomchaidia mtukufu raichi daktari. Hivi leo ni chiku gani?
    Chanzo: Mwananchi jana.

Monday 5 August 2024

Epuka au Usiwe, Kuoa au Kuolewa na RST

Tumeumbwa watu kila aina wabaya hata wazuri. Kwa vile ndoa hufungwa na wanadamu, tunaomba tugusie suala nyeti bila kuonekana kama tunabagua au kuwawekea utu ubaya. Hivyo, siyo uzushi kusema dunia ina watu wazuri na wabaya. Leo tutaongelea tutakachokiita RST bi maana ya Roho mbaya, Sura mbaya na Tabia mbaya. Kwanza, tukubaliane. Kuna watu wenye sifa hizi.
Tutaanza na kisa cha kijana mmoja wa kiume mtanashati na handsome (hatuna Kiswahili chake). Kijana huyu alijaliwa elimu na kazi nzuri vilivyompatia kipato mbali na biashara zake. Pamoja na yote, tokana na makuzi yake ya kizazi cha zamani, hakuwahi kuwa kwenye mahusiano tokana na sababu zifuatazo:
        Mosi, malezi yake yalikataza uhuni au uhuria unaoanza kujitokeza kwa kuigiza wazungu ambapo watu wasiooa au kuolewa huanza mambo ya wanandoa. 
        Pili, alichelea kuzaa kabla ya kuoa jambo ambalo hakutaka liwe kikwazo katika ndoa yake. 
        Tatu, hakutaka watoto wenye mama tofauti aka rangi mbili.
        Nne, alikuwe mwenye aibu na mwenye kujitunza vitu viliviyomtenga na mambo ya starehe. 
        Tano, alitunza fedha ili baadaye awe na familia yenye maisha mazuri. Mfano, alijenga nyumba na kununua gari kwa ajili ya shughuli zake za kikazi na kibiashara kabla ya kuoa. 
    Sita, aliogopa kuwakwaza wazazi wake kwa kujiingiza kwenye mambo ambayo, kimila lazima yapate ridhaa yao. Hivyo, alingoja kupata mwenza atakapoamua kuoa.
        Pamoja na kijana yule kutotaka kuoa kabla ya kukamilisha malengo yake na kuheshimu taratibu, hakukosa akina dada waliompenda ima kwa sababu ya u-handsome wake, elimu yake, au fedha. Mwenyewe aliendelea kujijenga ili awe tayari kuanzisha familia yake. Siku ya kutafuta mchumba, alipata taabu sana. Kwanza, alikuwa mwenye aibu na ambaye hakuwa na uzoefu wa kuwa na mawasiliano na akina dada hasa akichelea wangemuingiza majaribuni.
        Kadri siku zilivyokwenda, dada wengi jirani waliomjua walimuona mdenguaji au mwenye tatizo. Hivyo, waliacha kumsumbua na kukosa imani naye. Hapa ndipo tatizo lilipoanza. Akiwa yuko tayari kutafuta mchumba, alijikuta hajui pa kuanzia. Akiwa katika mchakato, aliajiriwa dada mmoja kazini kwake ambaye, licha ya umri kwenda, alikuwa si mwenye sura nzuri na wala hakuwa mechi ya yule kijana si kwa tabia wala sura. Hivyo, tutamuita jimama.
        Tokana na muda kwenda, jimama lilipogundua kuwa yule kijana mtanashati hakuwa na mke wala rafiki wa kike, lilianza kumzoeazoea kiasi cha kuanzisha urafiki wa kawaida. Jimama lilikuwa lilishafanya kila aina ya ufuska, utoaji mimba, uhuni wa kila aina kuchumbiwa hata kuvunjika uchumba kutokana na tabia mbaya. 
        Yule kijana–––tokana na kutokuwa na uzoefu––––si jimama likamzidi ujanja likamshawishi kuanza mahusiano. Haukupita muda, jimama lilimtegeshea mimba. Kabla ya hata kujua la kufanya, jimama lilihamia nyumbani kwake kwa kisingizio cha mimba yake. Kwa vile hakutaka kuzaa bila kuoa, kijana alijikuta akiingia matatizo makubwa kwa kukubali kulioa lile jimama japo hakulipenda toka rohoni.
           Kwa upande wa jimama, lilishinda mambo matatu kwa mpigo. Lilipata mume tena msupu au mhandsome kama wasemavyo wakenya tena mwenye fedha na historia ya kutokuwa mhuni, na mtoto. Ni kama ilikuwa ndoa ya mwewe na njiwa. Alilitambulisha kwa wazazi wake, walistuka na kuhofia kulikuwa kuna namna lakini wasiingilie kwa kuogopa kumvunja moyo mtoto wao au kuingilia chaguo lake. Yule kijana aliamua kulioa hilo jimama.
                Maisha yalianza. Jimama lilokuwa pole kabla ya ndoa, ghafla, lilianza vituko kwa vile lilikuwa limeishaolewa na kumzalia mtoto. Mungu hamfichi mnafiki. Lijisahau. Lilianza kumchuna yule bwana kwa vile lilijua lilivyolazimisha ndoa. Hivyo, lilihofia huenda jamaa angeamka usingizini na kulipiga teke. Hivyo, zile tabia zake asili yaani RST zilianza. Kama tulivyogusia, jimama lilianza kuonyesha uhalisia wake. Lilianza kuwachukia ndugu za mumewe. Lilianza mahusiano na marafiki zake wa zamani wakiwamo hata ndugu wa karibu maana lilitoka kwenye  makabila ya wapenda fedha na ambao huchukuana ndugu kwa ndugu.
         Baada ya mume kustuka na kuanza kuwa mkali, jimama lilikosa kujiamini likaanza kusaka madawa ya mapenzi wa waganga wa kienyeji lisijue hakuna dawa ya mapenzi bali tabia njema, uaminifu, na mapenzi ya kweli. 
        Kufupisha kisa kizima, jimama liliishia kuachika tokana na RST. Hivyo, mnaopanga kuoa hata kuolewa, mjiepushe na RST iwe mke au mume. Tabia njema ni silaha tuliaswa. Kwa waoaji wasio na uzoefu, washirikisheni wazazi wenu yasiwakumbe yaliyomkuta kijana huyu asiye na hatia. Msikurupukie mahusiano bila kujiridhisha kuwa mnaingia kwa kuzingatia uchaguzi wenu. RST ni sawa kilema. Haitibiki. Iepuke. Ni vizuri wanandoa wakaendana kulhali japo wakati mwingine mapenzi hayachagui. Muhimu, tusilazimishe ndoa. Haitadumu. Tusitafute dawa ya mapenzi. Hakuna. Tusiingizane mkenge katika ndoa. Tuwaingizao watakengeuka na kulipiza kisasi.
Chanzo: Mwananchi jana.