Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Thursday 8 August 2024

FYATU MFYATUZI: Ukweli nchungu kuhusu uchaguzi wa mwaka 2025


Nikiwa kwa akina Nshomile, wapo wachionjiua wala lengo langu. Nilipochema ukweli walidhani namwaga ntama kwenye kuku wengi baada ya kuchoshwa na dhuluma wanaona kama ulijifanya nshomile. Kuna mmbea mmoja kanitonya eti nilikuwa nimepewa ka-nshomile nilikolala nako kakanizingua nikafyatuka na kufyatua niliyofyatua nikasahau kuwa ningewaudhi wengi hacha wanene wa chata wanaotaka chacha nifyatuliwe wachijue chi vizuri.                                     Kilichowakosha mafyatu ni kufyatuka na kufyatua ukweli, sorry, upupu ulioacha Chama cha Mafyatu (CcM) hoi japo hai. Wapo wanaozusha eti nilikuwa amefyatua lubichi, kimpumu, gongo, na waragi toka UG. Wapo waliochema eti nilivuta chigara kubwa chiku hiyo ikanifyatua nifyatuka hadi kufyatuliwa. Wangejua kuwa hata juichi huwa chinywi kwa kuogopa inaweza ku-ferment ikanifyatua, wachingefyatua wanayofyatua. Hata kama nilipata kanywaji wao yawahuchu nini? 
Hata kama nimefyatuliwa, najivunia nilivyopayuka, chorry, kufyatuka wachijue mie ni Fyatu Mfyatuzi aka Mpayukaji Mchemahovyo zamani kabla sijabadili dini na kuwa na dini ya Mwananchi hadi nikapewa chafu hii. Nimechemaje? 
            Chiogopi wala kuchononeka. Hii kwa kimakonde huitwa collateral demage. Chijali. Ukifyatuka ukafyatua lazima ufyatuliwe. Kamuulize mhariri wangu. Chamtaim, hutaka kunifyatua. Huwa tunayamaliza kichikaji. Hivo, pliji, don’t take me chiriyachili. Hayo tuyaache njomba.
             Eti wanashangaa Nilivyochema eti kwenye uchakachauaji ujao, kama kawa, kutakuwa na upigaji halafu wahuchika watatubu na kuomba Chir God awachamehe. Kwani chili? Hawajali mafyatu watafanya nini? Wanadai eti ninawaona mafyatu kama hamnazo kama mie wanayedhani eti china akili na ujachiri mkubwa chana wakati nimeonyesha wazi nilivyosheheni kwangu. Nilimchikia mmoja akiniita mkumbaff achijue ukumbaff mwingine unalipa njomba. Kama unafanya ukumbaff unachinda, shida iko wapi? Kwanini nao wachifanye ukumbaff huo huo kuwazuia na wakachinda?
Nawachangaa wanaonichangaa na kunitukana. Mbona yupo waziri aliyechema eti chichi tunakopa kwa vile tu matajiri wakati raichi anachema anadhalilishwa kwa kukopa na hakuchukuliwa hatua? Mbona yupo aliyetengeneza uhaba wa chukari na bado anatecha? Mbona hata aliyetuhumiwa upigaji Mirerani amepandishwa cheo?
Zifuatazo ni chababu kuntu za kujipongeza:
        Fechiti, najua wengi hawanijui. Hii ni chiri uchiwambie hawajui nimerithi ujachiri wa dingi wangu? Mara nyingi wengi wakiniona humwaga chozi. Maana ni kama huwa wanamuona njomba kanali Mucha mwenyewe baba yangu mzazi.
        Chekandi, napenda ukweli na uwazi kama njomba Ben Nkapa. Hii ni achili yetu. Kuchema ukweli njomba. Nadhani huko Njomba Nkapa alipo atakuwa anafurahia kaburini mwake.
        Three, japo mimi chiyo chehe, nimetabiri vizuri kuwa Chichiemu itashinda hata kama ni kwa goli la mkono kama ilivyotokea 2015 nilivyotabiri bila kukochea au kupitia nje ya chanduku la kula kama ambavyo itatokea mwakani. Nani hajui hili japo wengi tena wanene wanaficha? Hawajui kuwa mie chiyo ntu wa utani utani!
        Nne, nimethibitisha kuwa ni gwiji la hichitoria. Rejea zilivyokuwa zikifyatuliwa kula za kura kama nilivyowahi kuchema kuwa ni goli la nkono. Naamini hii itarudiwa uchawa huu ambapo mnachema mitano tena kwa maza. Kwa wachio kujua nawachauri warejee hichitoria. Nakumbuka kicha cha kule Ntama ambako mshindani alipotea kabla ya kurejesha fomu nawe tukapeta? Nani hakumbuki kuwa hata aliponyatuka Mwendaze nilichema eti Mungu kaamua ugomvi? Hawa nazani wamechahau au wanijui au wanajifanya kutonijua. Wanachahau kuwa niliwahi kuchema kuwa huwezi kuchonga kinyago halafu kikakutisha. Chijui kinyago ni nani hapa.
        Tano, kama ushauri wangu utazingatiwa, tunaweza kuokoa njuluku ambazo zimekuwa zikipotezwa kwenye uchakachauaji ambao matokeo yake hujulikana hata kabla ya kufanyika kama ilivyo kwa majirani zetu wa Rwanda na Uganda. Kwanini kupoteza njuluku wakati tunacholipia ni kujitia hachara na kinachotakiwa kinaweza kupatikana bila kutumia njuluku. Bahati mbaya, wanaokulaumu hawalioni, kulijua, wala kulikubali.
        Kabla ya kumaliza, ngoja nimguchie pia rafiki na mshirika wetu Mgoshi wa Bumbui. Naye alifyatua maulaji hadi yakamfyatua akafyatuka kabla ya kufyatuliwa. Chijui mzee wake anajichikiaje chacha. Maana, aliwahi kututambia kuwa vitegemezi vyake vina akili chana na lazima kuteuliwa uwaziri achijue kuna na kutumbua aka kufyatua. 
Chijui huyu naye chiku hiyo alikunywa kanywaji gani hadi kuchema eti hawampendi mtukufu raichi doktari mpendeka. Tate nane tate nane.                         Niliwaonya kuwa kuchifia kupita kiachi chaa nyingi hupitiliza na kuchababisha kukufuru kama huyu aliyemponda maza wakati alikuwa akijionyesha kuwa anampenda. Nadhani mlichahau mlilvyotumbuliwa na Mwendazake akawachamehe na akafyatuka mkaendelea kumchengenya. Hayo tuyaacha. Nangoja kuona wengine kama wale wa walitengeneza uhaba wa chuga, wenye kachifa za mirerani japo naona wengine wamepandishwa, na wale wote wachiomchaidia mtukufu raichi daktari. Hivi leo ni chiku gani?
    Chanzo: Mwananchi jana.

No comments: