The Chant of Savant

Monday 30 July 2012

Hongera Sipho 'Hotstix' Mabuse kumaliza fomu six

South African musician Sipho Mabuse performs during the Joy of Jazz festival in Johannesburg on August 2010. Photo/FILE
Kwa wale wapenzi wa zilipendwa wanamkumbuka gwiji la muziki toka Afrika Kusini Sipho 'Hotstix' Mabuse (Pichani). Gwiji huyu alitoroka umande katika miaka ya 60 kuendeleza kipaji chake cha muziki. Pamoja na mafanikio yake kimuziki, hakuridhika kuwa kihiyo au kughushi shahada au vyeti wa usomi. Alijipinda na kurejea shule ambako hivi karibuni alihitimu elimu ya kidato cha sita akiwa na umri wa miaka 60. Kwa wale wanaodhani wamechelewa au kughushi kuna somo kubwa hapa. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

1 comment:

Anonymous said...

GAZETI la Mwanahalisi limefungiwa kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa linachapisha habari na makala zisizo na tija kwa jamii.