Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Saturday, 18 March 2017

Mlevi aadhimisha siku ya kinamama kwa kumteua mkewe


    Image result for photos of salma kikwete    
Baada ya wana mama karibu dunia nzima kuendelea kunyonywa na mfumo dume, juzi kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake ulimwenguni, mlevi niliteua mke wangu bi mkubwa almaaruf Salama Chinga Domokubwa kuwa mjumbe wa kigwena cha walevi aka Bunge la walevi. Hii ni baada ya kugundua kuwa kumbe walevi wengine huwateua bi wakubwa wa marafiki zao kuwa wanene. Mie sikungoja nistaafu ili atakayechukua kiti changu ameteue bi nkubwa wangu. Kama mzee K M7 pale Ug, nimeamua kumpa bi nkubwa ulaji wakati nikiwa kwenye ulaji.
Tofauti na wale walioteuana na kuzusha gumzo, walevi waliridhika nauteuzi wa bi nkubwa wangu kwa vile wananiamini. Na isitoshe bi nkubwa wangu ni kapuku ambaye hana cha NGO wala kipato cha ustaafu. Tofauti nyingine ni kwamba bi nkubwa wangu amepiga shule hadi akaambiwa no more class go to your husband and cook and do other things for him. Yeye hategemei unene wangu kuteuliwa bali kisomo chake ambacho ni wanawake wachache wanacho kwenye kaya ya walevi. Hii sitafsiri ili wale walioghushi vyeti au kuogopa umande kama siyo kubashite waipate. Hapa lazima mtembee na kamusi. Mbali na hiyo, tokana na mfano uliowekwa hivi karibuni kule kwa Joji Kichaka na Trumpet, si vibaya nikaanza kupiga mahesabu ya nke wangu kugombea hata urais wa walevi.
Walevi ni viumbe poa sana kama ukiwaelewa. Wanachotaka ni wewe kuwaonyesha kuwa u mnyenyekevu na asiyejitia kujua kila jambo. Wao hata ukimteua mbwa wako kuwa mjumbe hawajali ilmradi uwape kanywaji na mapupu pale Uwanja wa hyena au vipi? Wala hawana visa na visasi kama wale wachunaji ninaowasikia wakihanikiza kupambana na wabaya wao wakimsingizia God utadhani wanamtumikia kweli. Hata hivyo, walevi si kama wadanganyika wala wabongolalalanders. Hakuna kitu wasichokubali kama kuwaburuza au kuwatisha. Kwa mfano, ukimweka lupango mwakilishi wao, hawangoji kipaza sauti anchomoe. Watakutokea wenyewe na utamwachia bila kungoja mapilato wenye adabu, heshima na udhu kumchomoa baada ya wewe kuchemsha kama nilivyoshuhudia hivi karibuni.  Ukitaka maulaji yao yakushinde jifanye imla. Ukitaka kukosana na walevi wadhulumu au kuwakingia kifua waliowadhulumu au kuvunja sheria zao. Watakutokea na michupa ima wakutie ngeu au utoke mkuku kama mbwa aliyefumwa akiiba nyama kama si paka aliyeiba maziwa. Kama ukifanikiwa kuwaburuza walevi ujue zako zesha. Kwani, watakulia pini hadi msimu mwingine wa uchakachuaji wakupige chini. Pamoja na ulevi wao, walevi wana sifa nyingine. Wana kumbukumbu kama tembo. Unaweza kuwaudhi ukajishaua na kujifanya wewe muungu mlevi kwa wakakushiti. Ila siku ya siku ikifika, utaona visasi vyao.
Turejee kwenye uteuzi wa bi nkubwa wangu. Guess what. Mwaka jana niliteua wajumbe wengine wa dezo. Kwa sheria za kilevi, lazima uteue angalau asilimia ya akina mama kwenye kila uteuzi. Kwenye uteuzi ule nilijitia ubabe na kuteua vidume wengi kuliko akina mama. Acha akina mama waanze kunung’unika. Si walikwenda kwa bi nkubwa ambaye wananchukulia kama shoga yao na kumpa onyo kuwa asipoteua mwanamama kutimiza matakwa ya sheria za walevi asahau ukuu mhula ujao. Kuona hivyo, si nikaamua kumteua bi nkubwa wangu ingawa yeye ni tofauti na hao mashoga zake hasa ikizingatiwa anatoka kwenye ukoo ule ule wa wanene wa walevi kama wale wa kule Idodomya.  Baada ya baadhi ya walevi na wavuta bangi kuanza kulalamika kwanini nimemteua bi nkubwa wangu, sikunyamaza zaidi ya kuwapa kanywaji na kesi kuishia hapo. Wengine walizidisha unywanywa. Kuwakata ngebe niliwaambia kuwa bi nkubwa wangu ni bonge ya supu yaani ni msupu au mzuri kwa wale wasiojua Kiswahili cha walevi.
Kimsingi, waliokuwa wakinitia taabu ni akina mama. Kwa vile wanaweza kudanganyana na kuwekana sawa, nilishangaa kuona walivyoridhika na mimi kumteua bi nkubwa wangu utadhani atawawakilisha makapuku waliokuwa wakinibana niteue ili kuleta uwiano wa kijinsia kwa mujibu wa katiba ya walevi. Sasa kwa vile nshamteua bi nkubwa. Next time, nanteua kitegemezi chetu kiitwacho Riziki ili kaya yangu yote iwemo njengoni. Isitoshe kama kitegemezi kitakuwa na mama yake njengoni, wale vishoka wanaosifika kunyemelea vya wenzao wataogopa kwa vile kipo. Hii nayo dili hasa usawa huu ambapo nasumbuliwa na malazi ambayo ni siri kuwaambia walevi hata kama wanayajua. Isitoshe mimi kwa cheo changu kama dingi wa kaya ya walevi si mjumbe wa kigwena chetu. Hivyo, sirahisi kuwapo kule kuhami mali zangu zisiliwe na vishoka, mafisi na vispring chickens vya kirume kama alivyofanyiwa nzee Madiba alipokuwa lupango. Hayo tuyaache. Kwanini tusiagane?
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 07:15

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (26)
    • ►  May (2)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ▼  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ▼  March (20)
      • Kumbe Tanzania imefika hapa!
      • Mgoshi Apendekeza Kijiwe Kihamie Koromije
      • Kwa Sasa Rais wa Tanzania ni Nani?
      • Kashfa ya Makonda: Inatakiwa busara si ubabe
      • Mlevi kuliambia na kulikolomije taifa
      • Bashite Kachape Kazi
      • Kwanini Magufuli anawadhalilisha mawaziri wake
      • Kijiwe champongeza Keinerugaba
      • Keinerugaba usisamehe fisadi wa elimu
      • Mlevi aadhimisha siku ya kinamama kwa kumteua mkewe
      • Mahakama isijirahisi hadi kuingiliwa na kunajisiwa
      • Kijiwe chawapa shavu CCM kuvuana magamba
      • Serikali isipoteze muda kuwafunga wakosoaji
      • Breaking News!!!! Kimenuka CCM washikana uchawi na...
      • Barua ya wazi kwa Makondakonda and Gwajimmy
      • Trump Giving Terrorists a Field Day
      • Waandishi wa habari hamjamtendea haki Janet Magufuli
      • Kijiwe chastukia matapeli wa maombi
      • First lady kuwa mbunge ni demotion au promotion?
      • Neema Muita Wa-mura: Wanene wote waige moyo wa Mugful
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ►  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.