The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Tuesday, 13 November 2012

Waishiwa tajaneni haraka vinginevyo tutatia guu



BAADA ya msimu wa sanaa na abracadabra kuanza kule Idodomya, juzi tulishuhudia vituko ambapo wahishimiwa waliendelea na mchezo wa kuvuana na kuvalishana nguo.
Kituko cha kwanza ilikuwa ni kufichwa na baadaye kuachiwa ripoti ya uchunguzi dhidi yaaibu za wahishimiwa kudai rushua toka kwa katibu mkuu aitwaye Maaswi.
Kwa vile wahishimiwa walikuwa ndiyo watuhumiwa, wapelelezi na waendesha mashtaka, kila mlevi alijua ambacho kingetokea kama kilivyotokea.
Pamoja na Takokuru kusema jamaa ni wala rushua, kamati yao haikuwakuta wao wakiwa na hatia ya kudai rushua toka kwa bwana Maasi au Maaswi kwa kiarabu.
Kituko kingine au sema scene ni pale Mzito Kabwela alipokuja na hoja ya kutaka walioficha njuluku kule Uswisi washughulikiwe.
Hata kabla ya kutulia si Mzito alibanwa ataje majina akaishia kujikanyaga huku mwenzie Mtundu Lissu akiwataja Endelea Chenga, Grey Mgonjwa na “marehemu” Dadi Balaahili.
Mwenzenu nilingoja kwa makini kusikia majina hasa yale yaliyotajwa kwenye the so-called List of Shame ya Dk. Silaha. Kwanza, tujiulize. Hata hao wezi na majambazi wakubwa walioficha njuluku zetu nje wakitajwa unategemea nani awachukulie hatua wakati wote wameoza? Hivi unategemea kambale amnyoe mwenzie sharubu? Thubutu yako!
Ziko wapi tambo za Takokuru kuwa ingewasiliana na mamlaka za Uswisi? Mgosi Machungi niliyemtuma kufanya upelelezi kwenye ofisi ya Eddie Washea aliripoti kuwa hata barua ya kuonyesha nia ya kudai njuluku zirejeshwe haijaandikwa! Hiyo ndiyo Bongolalaland inayoweza kuliwa na kila jizi jambazi na tapeli.
Hiyo ndiyo Bongolalaland ambayo imegeuka shamba la bibi chizi. Ndiyo hiyo Bongolalaland ambayo mzee Mchonga aliipiga laana baada ya kugundua kuwa patakatifu pa patakatifu paligeuka kuwa pango la wezi mchana kweupe huku walevi makondoo wakichekelea kama si kulalamika lalamika.
Hawa wanaodai watu watajane majina wanaonekana kuwa watu wabaya kuliko hata shetani mwenyewe. Hivi kama watatajana majina ukakuta hata majina ya watakatifu na watoto na wake zao tutafanyaje? Sisi kijiweni tunasema tajeni hata kama kuna jina la Mungu mwenyewe.
Tajaneni tuwaone wajanja vinginevyo tutaendelea kuwaona wanafiki waongo na wababaishaji wa kawaida. Tuchukue fursa hii kumshukuru na kumchakatiza Mzito Kabwela aende hatua nyingine kwa kutaja majina. Maana ashataja majina ya wizara walimotoka walioficha njuluku nje.
Kwa kumbukumbu ni kwamba Mzito alitaja mawaziri wote wakubwa walioshika madaraka kuanzia 2003 hadi 2010. Hii maana yake ni kwamba watajwa hapa ni Freddie Tuwahi Sumae.. we koma! Wengine ni Eddie Ngonyani Lowasir, na mzee Mizengwe iliyoPinda. Kitaalamu huita ushahidi kama huu circumstancial evidence yaani ushahidi uliojikunja kunja kimazingira.
Wengine waliotajwa ni waliowahi kuwa madingi wa shirika la Wese yaani (TIPIDICI). Hapa namkumbuka rafiki yangu Jona Kilaganane nawe msomaji ongezea mwingine ili tuwavue nguo. Wengine waliotajwa ni wale walioshika wadhifa wa waziri wa madini 2003 hadi 2010. Hapa rafiki yangu Niziro Ka-damage, Willy Ngeeja na Dan son of Jonah, hamuwezi kuponyoka. Rejesheni njuluku zetu haraka kabla hatujawapiga na albadiri.
Nasikia pia kuwa Mzito Kabwela alikuwa anataka kuwataja wengine wakubwa zaidi akatishwa na kuibiwa karatasi yake alipokuwa ameorodhesha majina yao. Hata hivyo rafiki yetu Profesa Msomimkatatamaa alifanikiwa kuyanyaka majina ya majizi hawa wazito.
Waliopaswa kutajwa walikuwa ni wote waliowahi kukaa patakatifu pa patakatifu baada ya kuondoka mzee Mchonga bin Musa. Hapa rafiki yangu Alie Hossein…nyi, Bendangerman Mkapu na Njaa Kaya hamuwezi kuchomoka. Najua leo hamuwezi kufanywa lolote. Ila huenda kuna siku ya siku mtajikuta mkinyea debe kule lupango kwa wakati wenu na madhambi yenu.
Kabla ya jamaa kuanza kuwashiana taa za kutaka kutajana, nani angeamini kuwa kaya hii ni ya mibaka ingawa siyo siri? Wahishimiwa wanakamua kwenye ujumbe wa kamati huku mawaziri wakiiba wanapomwagwa wino kwenye mikataba kama alivyofanya Ni Ziro Ka-damage alipokwenda London kusaini mkataba wa Uzwaagi hotelini na akapewa njuluku zake alizokimbizia Uswisi.
Kwa vile sasa habari zinakuja mdomdo, kijiwe kina mpango wa kukaa kama kamati na kutoa shinikizo kwa wahishimiwa kutajana kabla hatujaandamana hadi mjengoni na kuwafanyia kitu mbaya. Leo sitasema ni kitu gani mbaya tutawafanyia. Tutawafanyia kitu mbaya kuliko hata hicho wanachofanyiwa na huyo mama Microphone bint Speaker.
Yeye anawadhalilisha ili kuwaridhisha mabwana waliomsimika hapo halipo. Sisi hatutawadhalilisha. Badala yake tutawaadhibu kama watoto wadogo ili kila mtu hata kunguru wawacheke kila watakapopita. Hivi fikiria tukiingia mjengoni wanakijiwe wote halafu tujinyotoa roho akitakuwa kitu mbaya kwa waishiwa sorry wahishimiwa?
Lakini hatutafanya hivyo kutokana na kuwa hii mijitu haina huruma hata mkijinyonga itaendelea kuiba. Heri kuinyonga yenyewe badala ya sisi. Tunaweza kuingia mjengoni na kukaa kwenye viti vya kabla hawajaingia na wakiingia tunatangaza rasmi kuwa mjengo ni wetu na sio wao.
Tunaiambia dunia kuwa tangu siku hiyo tumeamua kujiwakilisha baada ya kugundua kuwa kumbe wenzetu wanawakilisha matumbo yao na vyama vyao badala ya sisi waliotuingiza mkenge. Unadhani hii ni kitu ya mchezo? Tutakuwa wa kwanza duniani kuwatimua waishiwa kwa kuingia mjengoni na kuchukua nafasi zetu. Maana vile vigoda wanavyokalia ni mali ya majimbo siyo matumbo yao.
Tukishaingia mjengoni tunatangaza kuwa hata mashangingi na mashumbwengu ya waishiwa ni mali yetu. Hivyo, tutawaamuru waondoke pale kwa miguu wakapande dala dala na baadaye treni kuelekea kwao kwa aibu yao. Pia tuwaamrisha warejeshe mshiko wote uliopo hapa kayani na Uswisi haraka sana kabla hatujachukua hatua nyingine kama vile kuwa-Gaddafi kama siyo kuwa-Mubaraka tena haraka.
Utani kando, hivi walevi tukiamua kuvamia ule mjengo na kuchukua nafasi yetu kuna mtu anaweza kutuzuia? Hii meseji ni ya mshirika wa Bedroom. Acha niende tukapange jinsi ya kuitana waheshimiwa baada ya kuwatimua wale wezi wanaoshindwa kutajana. Sisi tutawataja piga ua tukishafika huko.
Chanzo: Tanzania Daima Novemba 13, 2012.

Well, well, Freddie, don’t break my ribs again!


Politicians are funny creatures just like magicians. Sometimes, they tell lies and promise heavens as they deliver hell. In a phrase, they perform acrobatics. Again, what transpired recently made me change my take on politicians. One Freddie Tuwahi Sumaye left me in stitches after accusing his party of corruption.
You know what; after being defeated in the game of eating and cheating, Freddie rushed against his party saying that it was dogged with corruption. True, Freddie left me with many more questions than answers.
Firstly, does it mean Freddie did gravely suffer from the mess he created? Again, didn't Freddie realize that once power slips from hands you become the opposite of what you used to be? A pretentious veneer of respectability does away and you become a commoner, if not, a “nobody.” In power, you are but an angel that can demonize anybody telling you the right things to do. History is a good witness. Once you’re out of office, you just cascade back to “demonhood” as it happened to Freddie.
Essentially, when Freddie expounded that whoever that wanted his business to shrive should join CCM, didn't he know who own CCM—those in power? Anyway, Freddie has nobody to blame except himself for nurturing that vice. So too, Freddie has no moral authority whatsoever to point a finger at CCM if at all his son is still enjoying goodies at Bank of Titans otherwise known as Bank of Tzed (BoT).
Maybe, just maybe, Freddie is becoming old so as to easily forget what he uttered yesterday. Ageing is a bad process. It makes you forget even simple stuff. Maybe, this is happening out of devastation. So too, ageing makes you blames others even if they’re the ones you produced such as corrupt guys and hyenas not to forget economic sharks that shrive under CCM. For instance, it’s alleged that Marry Nyago forged her PhD. When allegations surfaced, she threatened to sue to no avail. Circumstantially, this suffices to convince me that there was, and still is; something fishy on how she obtained her PhD. Did Sumaye see it the same was as me before being beaten by the suspect? Of course nope! Kulindana and now kuangushana!
When it comes to allegations that Nyago used money to suffocate and later defeat you, understand Freddie. This is the product of joining CCM--- her biz is now booming thanks to protectionism and opportunism CCM created for such gawks. thanks to her heeding your call to join CCM.
True, Freddie, don’t break my ribs. Seriously, don’t my friend. You know what? When some kamikaze guys told you and your boss that our hunk was stinking with corruption, you called them names. Your friend-cum- boss Benny Makapu used to say that those telling you the right things were as jealous as women. Now look Freddie. Marry Nyago used the same “female jealousness’ to turn tables against you! Had she used ‘male jealousness’, she’d have invited Protection and Condoning Corruption Bureau (PCCB) to dig into your past and book you. You know what? The other day I was reading one newspaper to find that some smart guys documented many things about you. They documented that Tshs. 50,000,000 you scooped from one public firm, farms and parcels of land you obtained in Moro and 500,000,000 you spent in the country of Obama before September 11.
Freddie, when you invited the media to set the records straight many goofed thinking that you’d address all the basics instead of politicking and flinching as you did. They wrongly thought: you’d blast your establishment. Poor them! Didn't they know that nobody cuts the hand that feeds him? They needed to know that you are a politician who can say anything. Essentially, when cornered the vulture cries wolf.
Freddie, now that  you've been slapped in face, what are you going to do? Importantly, remember. When good Samaritans were telling you of fighting corruption, they meant to help you to avoid such a shame of being bought out of power as it recently happened. There was no fitting way to set records straight like this. Sadly though, you lost it. Even those who booted you out will one day face the same. For he who lives by the sword, dies by the sword. It is unfortunate that power intoxicates so as to cause myopia. Hegel once said that history is always there because people learn nothing out of it. It becomes even evidently sad if those in question are so myopic that their ability to see is the length of their noses. How many do you think we currently have Freddie? I’m not peppering you with a barrage of questions today. Again, I can hedge my bet and you can take this to the bank. The defeat rendered you politically impotent. If you jump the ship do it not for seeking presidency. The timing is wrong and the stars align in a wrong way. Had you sensed the wind of humiliation prior you’d have become diamond not liability. Whatever you do now, will be judged as vengeance and devastation. Fait accompli. People will argue, “If he failed to win just a district position how he can win presidency? Whoever that tells you that you can reclaim your fame, tell him to tell it to the birds. No how Freddie, you’re caught between the rock and the hard place. Again, well, well, Freddie, don’t break my ribs anymore.
“In the country of the blind, the one-eyed man is king,” Desiderius Erasmus Roterodamus.
Source: ThisDay Nov., 12, 2012

Monday, 12 November 2012

Kenya yapoteza polisi 42!

Injured police officer in hospital
Ingawa sakata la wizi wa mfigo nchini Kenya linaonekana kama la kawaida, mwaka huu limechukua sura mpya baada ya wezi wa mifugo kuvamia askari na kuua 42 na kujeruhi wengine wengi. Sakata hili lilitokea kwenye eneo la Samburu ambapo wafugaji humilki bunduki ili kujihami dhidi ya wavamizi toka nchi jirani. Serikali imepata somo kwa njia ngumu baada ya kupoteza idadi kubwa namna hii. Je huku kuzagaa kwa silaha si kitisho kwenye eneo zima? Je dawa ni nini zaidi ya kuhakikisha kuwa Somalia inakuwa na serikali imara? Kuna haja ya kuliangalia janga hili kwa macho mapana. Majirani wanapaswa kuanza kujiandaa kupambana na madhara yatokanayo na kuzagaa kwa silaha. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

Kikwete anaposhutumu kile alichoanzisha!



“Vitendo vya kuchambuana mwishowe ili mharibiane mwishowe mnakuwa dhaifu.. vita ya panzi sherehe ya kunguru,” Rais Jakaya Kikwete akihutubia mkutano wa chama chake . Alitoa maneno haya wakati akikemea wanaoutafuta urais baada yake. Kwa wanaofahamu jinsi Kikwete alivyoasisi mchezo wa kuchafuana akiwatumia hired guns kama Salva Rweyemamu na waandishi wengine wa habari nyemelezi na wachumia tumbo, wanashangaa Kikwete anapata wapi jeuri ya kuwananga wenzake. Je ni yale yale ya nyani haoni kundule au  unafiki wa kawaida? Je Kikwete ana udhu wa kuwananga wenzake wakati yeye ndiye mwanzilishi na mnufaika wa jinai na kadhia hii?
Hebu angalia nukuu nyingine ya Kikwete, “Niacheni…. nitakuwa mwenyekiti wa ajabu sana, eti wanataka niwe kwenye kambi zao hivi nikiwa kwenye kambi zao nitatenda haki?”
Kweli Kikwete haishi maajabu na sanaa. Haki gani anaweza kutenda iwapo ameshindwa kutenda haki ya kutimiza ahadi zake? haki gani anayoijua Kikwete iwapo utawala wake umeghubikwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu? ni haki gani anayoongelea Kikwete iwapo ameshindwa kutenda haki ndogo tu ya kukemea mafisadi achilia mbali kuwakamata?
Kikwete ataondoka madarakani na kuacha historia ya kuwa rais asiyeeleweka wala kuelewa. Ataacha legacy ya kukuza na kudumisha ufisadi na ugeugeu hata mahali pasipostahiki.
Je maneno ya Kikwete ni ya kuamini na kuaminika iwapo anajulikana yupo kwenye mtandao upi? Je kwanini Kikwete anadanganya na kujidanganya mwenyewe? Hakika time will tell.

Saturday, 10 November 2012

Kwa hili nampongeza rais Bozize

Rais Francois Bozize wa Afrika ya Kati alifanya kitu ambacho kimewashinda marais wengi wa kiafrika. Hivi karibuni aliamrisha mwanae, Kelvin awekwe ndani baada ya kukataa kulipa deni kwenye hoteli moja ya kifahari mjini  Bangui. Sakata hili lilisababisha meneja wa hoteli husika kuwekwa ndani kabla ya baba mtu kuingilia na kumwachia huru meneja huyo.
Viongozi wengi wa kiafrika wamewaachia watoto hata wake zao kutumia madaraka yao bila hata kuwakaripia achia mbali kuwazuia. Kwa hili rais Bozize ameona mbali kiasi cha kujenga picha ya mtu asiyetaka madaraka yake kuwa mali ya familia marafiki au ukoo. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

Wednesday, 7 November 2012

TAKUKURU na wabunge walipovuana nguo!

JAMAA wa taarabu walipoimba “Mtu Mzima Hovyo” sikujua kuwa kumbe walimaanisha! Mwenzenu juzi nilipata burdani na kutoa burdani kijiweni.
Baada ya kushuhudia wahishimiwa wa Mjengoni na njemba za Takokuru wakivuana nguo tena hadharani, niliamua kuchukua kigoma changu na kujimwaga mitaani kucheza ndundiko.
Wakati sherehe zangu za kuvuana nguo hazijatua si nikasikia kuwa vijana wa Takokuru wamemnyaka mhishimiwa Zungu ambaye hata hivyo siyo zungu kitu bali uvumishi wa waswahili. Wapi na wapi chotara wakimakonde na kiarabu akawa zungu? Hata hivyo, wanaojua mchezo wa kulindana na kugeuzana majuha walijua hawa vijana wangekemewa na mambo kuisha! Unacheza na Chama Cha Mafisi siyo? Mgosi Machungi haachi kusema tiishasema kuwa mbwa hamng’ata aiyemfuga. Hayo tuyaache.
You know what? Baada ya ile Taasisi ya Kupamba na Kupokea Rushua (Takokuru) kusema wahishimiwa ni wala rushwa si nao walikuja juu na kuigeuzia kibao ikaishia kuwa kama jibwa jizi! Kamwene Pita Msigwa ndiye aliongoza mashambulizi kwa Takokuru aliosema ni wala rushua Kaya nzima hakuna. Wanakula rushua kuliko hata Endelea Chenga na Dokita Iddiliisha Rashid.
Msigwa alisema kuwa mijamaa ya Takokuru ina utajiri kama Bill Gate. Nasikia dingi wao Eddie Washea ana njuluku kuliko hata mzee Warren G Buffet yule mshikaji wa kwenye kijiwe chetu cha Nebraska kule kwa Joji Kichaka. Huyu jamaa tulisoma wote chuo ingawa yeye hakumaliza. Hayo tuyaache.
Baada ya wahisimiwa wala rushua kuwavaa wala rushua wenzao wa kampuni ya kutetea na kukusanya rushwa Takokuru, mwenzenu nilifarijika nikijisemea kuwa sasa nimewapata. Nilicheka sana kuona huu wendawazimu na ujuha wa kitaasisi ambapo madingi waliamua kutoana nguo na kubaki watupu.
Kumbe ndiyo maana jamaa wanapigania uheshimiwa kwa kila namna ili wapate njuluku za rushua! Sasa nimeelewa. Kama sikosei, kama Bunch of Thieves (BoT) itakuwa imesheheni watoto au ndugu wa vigogo. Kwani hamkusikia kuwa hata mahospitali yote ya Dar yanasimamiwa na watoto wa vigogo waliotajwa kuwa Amani Milima ya Kighoma, Janati Joji Alihama, Asha Omare Mahitaa, Hawa Rashidu Kawa na Gwa nini Ikate ile Kamba? Hapa bado daktari Salama Kikwekwe ingawa ni mtaalamu wa njino.
Turejee kwenye uhuni wa Takokuru na wahishimiwa. Mie zamani nilidhani kuwa Takokuru hawali rushua.
Lakini baada ya kupata data kuwa jamaa hawa ni matajiri wa kutupwa nilistuka na kubadili imani yangu juu yao.
Hata hivyo, tujiulize. Hata wakiamua kama walivyokwishaamua kula rushua nani atawakamata wakati wakamataji ni wenyewe?
Hii mzee mzima ilinikumbusha kisa cha wazee wa mabao wanaomilkin ngwara ngwara bin dala dala. Magari yao hayapigwi bao. Nani atayapiga bao wakati wapigaji mabao ni wao? yaani baada ya kufichuka ufisadi huu wa wakubwa na mbwa wao nilitamani mwalimu Mchonga afufuke na kuwa rais wa kaya ili awakamate hawa jamaa na kutaifisha mali zao na kuwapeleka lupango.
Lakini kwa sasa nani atampeleka lupango nani wakati wote ni mijizi yarabi? Nakumbuka mgosi Machungi na Mipawa waliwahi kudai kuwa wahishimiwa wetu wanawakilisha matumbo yao na nyumba zao ndogo. Mimi nilibisha. Sasa nimeamini walichomaanisha magwiji hawa wa uzamizi wenye PhD za kijiwe tena bila kughushi.
Hakuna kitu kilinishtua kama Takokuru kunyamazia tuhuma nzito kama hizi. Nilidhani angalau wangejibu hata kwa majibu mepesi. Badala yake waliuchuna wakijua kuwa walevi ni wepesi wa kusahau. Na kweli wamesahau. Laiti nguvu na akili inayotumiwa kwenye upuuzi kama upinzani na chuki za kiimani vingeelekezwa kwa majambazi hawa, basi kaya yetu ingekomboka vilivyo tena haraka.
Ajabu hata mkuu wao aliyesema ana orodha ya wala rushua wote, majambazi na wauza unga aliminya wakati jamaa wa Takokuru wako chini ya afisi yake!
Hata hivyo simshangai kutokana na jinsi yeye na watu wake wanavyohomola sawa na Takokuru yake na wahishimiwa. Muulize ili ahadi ya kurekebisha ile mikataba ya kichukuaji ya uwekezaji imefia wapi?
Si amehomola na kuacha jamaa waendelee kutugeuza shamba la bibi.
Naanza kujenga hitimisho kuwa haki kwenye kijiwe chetu iko sokoni ikiuzwa na kila kibaka kwa amtakaye na bei atakayo.
Je, namna hii tusipochenjiana tusiokuwa kwenye gemu si tutaisha jamani?
Walevi mko wapi au bado mnaendelea kushikilia matumaini?
Shauri yenu mtaendelea kuliwa na wawekezaji na makuadi wao waliotamalaki kila kona. Mie simo! Haliwi mtu.
Nani atamla mvuta bangi na mlevi ambaye yuko tayari kujinyotoa roho hata bila kuudhiwa? kwa walevi walio laini wakiimbiwa nyimbo ngojera na sanaa za amani, hakika mtaliwa sana.
Hata hivyo, siyo mbaya. Mmezoea kuliwa endeleeni kuliwa tu. Kweli kaya yetu sasa imegeuka ya kulana. Walimu wanakula wanafunzi wao. Wachungaji wanakula waumini; madaktari wagonjwa; wanasiasa wapiga Kura.
Nasikia kuna makabila hata wababa wanakula vibinti vyao! Ni kulana mtindo mmoja.
Polisi wanawala wahalifu, wenye nyumba wapangaji wao bila kusahau madalali. Ama kweli kaya ya kuliwa ni ya kuliwa. Mnaipeleka wapi kaya yetu?
Kwa vile jogoo aliwafundisha vifaranga kunya ndani, je, ni wangapi watatumia udhaifu huu kuendelea kuwala wenzao? Upuuzi ni pale jogoo wanapokunya ndani wasiguswe lakini vifaranga wakithubutu wanatishiwa kifo?
Kwani hatuyaoni ambapo wakubwa wanakula kila aina ya rushwa na kuachiwa ilhali wale wadogo wakipatilizwa? Je walevi mtaliwa hadi lini? Siachi kujiuliza.
Kama wahishimiwa tena watunga sharia wanakula rushua kweli watatunga sharia za kuzuia na kupambana na rushua au kuilinda na kuipamba kama yalivyo matendo ya Takokuru? Hakika hii ni kaya ya mafisi na mafisadi!
Naona Zungu anakuja ngoja nikamuulize alivyoua hii soo.
Chanzo: Tanzania Daima Novemba 6, 2012.

Tuesday, 6 November 2012

Natabiri ushindi wa rais Obama kesho



Ingawa mimi si mtabiri, sina wasi wasi rais Barack Obama ataendelea kuongoza Marekani kwa miaka minne mingine ijayo. Jinsi alivyoendesha kampeni zake na kutetea utendaji wake na jinsi mpinzani wake Mitt Romney alivyoshindwa kuwashawishi wamarekani, lazima Obama ashinde.

Kikwete pambana na ugaidi badala ya kutoa pole


Hakuna ubishi kuwa vitendo vya kigaidi vinavyoendelea nchini ni matokeo ya ulegelege na uzembe wa serikali. Ingawa rais Jakaya Kikwete amekuwa mwepesi kuwahi kwenye matukio ya waathirika wa vitendo vya kigaidi, hii ni sawa na machozi ya mamba. Je lipi muhimu, kutoa pole au kupambana na vitendo vya kigaidi. Serikali imeonywa mara nyingi kupiga marufuku vikundi vinavyoeneza chuki baina ya watanzania. Imeonywa juu ya mihadhara ya kidini inayoendeshwa na wachumia tumbo wasio na hata elimu ya dini imedharau. Sasa tazama madhara ya ujinga huu ambapo watu wanaanza kuathiriwa kama ilivyotokea kule Zanzibar ambapo katibu wa Mufti wa Zanzibar Fadhil Soraga ( Pichani)amemwagiwa tindikali.
Tunadhani waathirika hawahitaji "machozi na pole" vya rais bali kushughulikia chanzo cha kadhia hii. Ingawa waliofanya kitendo hiki cha kinyama hawajajulikana, kuna haja ya vyombo vya dola kuwasaka na kuujulisha umma ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Hali ikiendelea hivi bila kudhibitiwa, kunaweza kuibuka hatari ya kulipiziana visasi hata kwa watu wasiohusika. Je amani anayoimba Kikwete na wenzake siku zote bado ipo? Tafakarini umma umechoka kutapeliwa kwa usanii wa kisiasa.

Monday, 5 November 2012

Thanks PCB and MPs for entertaining us with your “nudity”




If you hear my keening, wonder not. I wish I’d pick my timbrel up and enjoy the madness of the nudity of the titans. I read the story that Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) --that has nary prevented or combated any corruption-- is itself corrupt. Such allegations were made by Members of Parliament (MPs) after PCCB alleged they were corrupt as well. This is why I’m singing and cachinnating. When grasshoppers fight who benefits? What else can I do to witness such megalomania?
The deplorable, sorry, honourable MPs said loudly that PCCB was vile with corruption. During their muscle-flexing bout about who’s who in corruption, much was said and learned. Big dent was incurred in this half-nelson. It’s spooky and doozy to note that those who bore us with their clangor and mantra of fighting corruption are themselves corrupts to the bone. Technically, we call institutional madness or nudity.  Who’d think that the waheshimiwa and anti-corruption watchdog officials were such hopeless and useless? Is PCCB anti-corruption watchdog or a mere thievish dog that can eat its own puppies? We now know that PCCB receives kickbacks. We egg it to come clean.  Astonishingly, when such damning allegations were tossed PCCB didn't rebut by telling MPs to recant them. It was claim and counterclaim, accusations and counteraccusations pell moll. In the end, we all saw how dirtier their underclothes were especially when they’re left on the agora. Again, given that this hunk is grossly immoral nobody cares.
For us who grew up under ethics-minded regime of Mwalimu Nyerere, our first shock was the way the general public treated these revelations. The power that-be, so too, kept mum as if this wasn’t a crime. For a reasonable power that-be such revelations were but a hunch to begin with. Many thought it was the time to bring the big gorilla in. If it were Mwalimu, I believe, he’d never coy to send these guys to Ukonga ASAP in the first place. Again, after our hunk suffered psychopathic megalomania, who’ll take on them if at all they all are the same? Under Mwalimu such revelations guaranteed property seizure and punishment right away. Under mwalimu such poltroons would regret their tongue wagging.
It started with PCCB firing its allegations that honourable MPs were corrupt. MPs did not sit on the allegations. Peter Msigwa (Iringa Town) CHADEMA had this to say, “TAKUKURU are the ones leading in corruption. For instance, during the campaigns of the past elections they (PCCB) were the first to alert the suspects to vacate the particular place when they were phoned. Later they would pretend to go to the place and would tell you that there was no corruption,” Msigwa admonished PCB to put their house in order first.
Serious and denting as the allegations were, one would think that PCCB would not silently own everything up. Instead, PCCB would have done the right thing namely to come clean on the allegations. Hell no. This was a passing cloud. There was no need for PCCB to spill more beans knowingly that Wabongo are good at forgetting easily. Who cares if at all such vices have been legitimized hunk wide? Who bothers if at all those charged with delivering justice are foolishly vending it? Who care if at all everything is well and peace and tranquility are plenty in the hunk?
The other day little bird told me that PCCB officials are super rich thanks to having nobody to arrest them when they fleece suspects. They’re above the law. They can target whomever they deem fit but not one of theirs.  And this has been the wishy washy tradition of the hunk. If you’re among the high and mighty nobody should disturb you. This is why MPs were wronged so as to spill the beans. PCCB must apologize for embarrassing the waheshimiwa. Ask Andy Chenge. The high and might can break all laws in the books.  Nothing sinister can happen given that the law is an ass. It is enacted to protect the “good” and punish the “bad” especially paupers. This is why PCCB deals with small fish but not sharks.  It is sad though that those nitwits are getting away with it due to the fact that the sin of corruption is a down- top and top-down affair in our hunk. If politicians can buy power, as it was alleged, then who’ll reprimand whom?  If some politicos can rig election in the broad daylight and call it free and fair, who then will see what we see? You know what?  Swahili sage has it that the cockerel taught the chicks to shit in the house. Instead of white washing PCCB needs to be helped by disbanding it with immediate effects. If I were president, I would not allow such a dirty beast to be under my office. For people will wrongly think that they are there to protect me with my people. Again, who wants to commit suicide at this very time at which corruption has been legalized especially for the high and mighty? PCCB bury not your head in the sand. Let me calmly tell you. This is hypocrisy.  Courage lost, all lost.
Source: ThisDay Nov., 5th, 2012

Sunday, 4 November 2012

Hakuna utajiri na neema kama hivi!


Katari (left) and Karam Chand have become the world's longest married couple. (somethinamazing.blogspot.ca)

Je kuna kitu binadamu uhitaji kama kuishi maisha marefu? Ongeza kitu kingine muhimu- kuwa na ndoa yenye furaha. Ongeza tena si ndoa tu bali ndoa ya muda mrefu. Vikonge hivyo hapo juu Katari (100) na Karam Chand (107),  kwanza vimekula chumvi nyingi. Pia vimeishi kwenye ndoa kwa miaka 87. Vimevunja hata rekodi ya kitabu cha maajabu cha Guiness. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

Thursday, 1 November 2012

Taaswira ya hali ya Tanzania


Imenikumbusha kauli ya waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye akiwaambia wafanyabiashara kuwa wakitaka mambo yao yawanyokee wajiunge na chama (hospitali) yake. Mambo ni hivyo hivyo karibu kila mahali. Mwanafunzi anaambiwa na mwalimu kuwa angehudhuria tuisheni yake angefanya vizuri. Askari wa usalama barabarani wanawaambia madereva kwenda kwenye 'hospitali" zao ili wasipigwe mabao. Sijui mkulima mdogo mdogo na mfanyakazi wa kima cha chini watamwambia nani kwenda kwenye "hospitali" zao?
Kweli Kipanya ana mambo.

Rais wetu kijina anazidi kuwa kijana


Rais Jakaya Kikwete akiangalia kopo la tangawizi  huko Mambakati Same alikozindua kiwanda cha Tangawizi. Kumbe uzee ushamnyemelea! Inaonekana hapa watu wake wa saluni walisahau kumpamba vilivyo kama siyo wapiga picha kukosea angel ya kuchukua picha.

Wednesday, 31 October 2012

Je CCM watamkumbatia Nagu au kumwangukia Sumaye?



 Chama Cha Mapinduzi (CCM) hujitahidi kuficha aibu zake kwa kuwabana wanaodhaniwa kutaka kukiaibisha, kashfa ya rushwa kwenye uchaguzi wa ndani wa chama uliopita haifutikwi chini ya busati. Hakuna mwiba unaoikabili CCM kama madai ya waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye kuwa uchaguzi ulitawaliwa na rushwa.

Sumaye alipotoa madai yake CCM ilitumia busara ya kuepusha malumbano. Lakini taratibu zilianza kuibuka tuhuma nyingine za dhambi hiyo hiyo ya rushwa hasa baada ya kufanyika uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa (UVCCM). Kuna madai kuwa rushwa ilitembea nje nje. Ingawa rushwa ni jadi ya CCM, kuzudi kwake kulimfanya mwenyekiti wake rais Jakaya Kikwete kusema, “Nawaambieni, mkifanya mchezo ipo siku mtakuja kujuta maana mkishamchagua kiongozi asiyefaa, mtalazimika kuwa naye huyohuyo hadi mwaka 2017 na kama waswahili wanavyosema majuto ni mjukuu,” 
Wengi walimuona Kikwete kama mnafiki na mwenye kutapatapa kutokana na ukweli kuwa ndiye aliyefunga rushwa ndani ya chama na serikali. Rejea kuendelea kuwakingia vifua watuhumiwa wa rushwa kama vile Andrew Chenge na Dk Idris Rashid waliobainika na mamlaka za Uingereza kupokea rushwa ili kununua rada mbovu kwa bei mbaya toka kwenye kampuni la BAE.
Rejea kuendelea kumlipa marupurupu na stahiki za kustaafu waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa hata baada ya kubainika kushiriki ufisadi wa Richmond. Rejea kuwarejesha kwenye baraza la mawaziri watu walioshiriki kwenye kuuza nchi kama vile Dk Abdallah Kigoda.

Yote tisa, baada ya Sumaye kushupaa na kutamka hadharani kinyume na taratibu za chama kuwa aliyemshinda kwenye uchaguzi Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Mary Nagu kutokana na rushwa, CCM imejikuta msambweni. Sumaye bado ana ushawishi chamani. Je CCM itamkumbatia Nagu na kumtosa Sumaye au kumwangukia na kumtosa Nagu. Yetu macho.

Mpayukaji ajiteka ili kuwapakazia ndata

BAADA ya kuona kundi la Uangusho kule Zaainzibaa likimwaga cheche na kupata maujiko huku SZM ikiwafumbia macho ikidhani wataufumuua muunganiko, mzee mzima Alhaji, Dk., Professa, Lt Col. Father, mtaalamu wa kuongea na majini, Mpayukaji Msemahovyo Waambie niliamua kujiteka ili kuanzisha vurugu ambazo nilidhani ni ukombozi wa walevi.
Nilipoona wabangaizaji kama Ismi Juha, Shehena Fuad na Tapeli Pondwa wakipata ujiko hata ulaji nami nikaona nitie guu. Ningeachaje kufanya hivyo wakati nina usongo na nambari kwani ukiachia mbali kuweza kupata wachukuaji waitwao wawekezaji wanaoweza kudhamini fujo zangu ili walevi wapigane nao wavune mali zao? Kwa wasiojua gemu zima wajiulize kwanini DRC imo msambweni? Madini wanangu. Kwanini Mashariki ya Kati imo motoni? Wese wanangu.
Kwa vile na kaya yetu ina madini na imegundua miwese mingi, lazima tulianzishe ili tupate washitili wa kula nao kwa ulaini. Unadhani ulaji mchezo?
Pia kufeli na uroho wa wanasiasia kula peke yao kumetufanya nasi kuona tunaweza kutumia nyenzo yoyote kuanzia bangi, kahawa, dini, hata jinsia kupata ulaji.
Hivyo kesho mkiona bi mkubwa wangu akiingia na chama chake cha Wanawake na Maulaji (WEMA) au Equal Oportunities for First Ladies (EOFL) msishangae, ni mambo ya ulaji.
Twende kwenye dili. Baada ya kuona napiga mikelele kwenye kijiwe na walevi hawapati somo, niliamua kujiteka na kutangaza kuwa nimetekwa na ndata ili walevi waamke na kupambana na ndata hata kuwanyotoa roho kama yule wa kule Zenj alivyofanyiwa na wahuni wa Shehena Fuadi.
Ili kuwapata walevi waliochoshwa na kutolewa chochote na ndata, niliwaambia kuwa badala ya kupigana na ufisadi huu wa ndata, tuanzishe vurugu kudai kuwa mfumo wa maisha wa walevi ndiyo unaopaswa kuendesha kaya. Kama Shehena wa Kupondwa Pondwa nilikuja na mkakati wa kudai kuwa walevi tunaonewa. Badala ya kulaumu ulevi na bangi zetu, nilitupia kila lawama kwa ndata na lisirikali.
Na walevi nao kutokana na ulevi na bangi zao si walikubaliana na mahubiri yangu ya ngoa na usongo. Ila kwa vile walevi ni walevi na hawawezi kuwavaa ndata, niliona nibuni njia nyingine ya kuwaamsha wapambane na ndata. Siku ya siku niliondoka zangu home na mshirika wangu wa bedroom tukiwa tunaendesha baiskeli yetu.
Nikiwa naendesha tulijadili mpango mzima na bi mkubwa wangu. Tulikubaliana kuwa baada ya kujiteka na kwenda kujificha kwenye kijiwe cha Uswekeni, baada ya siku tatu nijitokeze kama aliyeachiwa. Uongo tuliotunga ulisema hivi: Tulipofika mitaa ya Usiniulize, nikamwambia bibi mkubwa aondoke zake. Kwani nilikuwa na miadi na Mgoshi Machungi na maongezi yetu yangechukua muda mrefu.
Hivyo, bi mkubwa alipaswa kuondoka ili awahi naye kwenye miadi yake na shoga yake Salmi Kikwekwe ili ampe mbinu ya jinsi ya kutumia NGO yake kutengeneza ulaji hapo baadaye. Baada ya bi mkubwa kuondoa baiskeli niliingia zangu kichakani kuchimba na kupanda dawa. Wakati narudi si ndata wakaniteka kwa siku tatu!
Ilibidi nifanye haraka kujiteka na kujitokeza hasa baada ya kugundua kuwa kumbe na Shehena Pondwa naye alikuwa amelianzisha ili apate ujiko. Hivyo sikutaka amalize ujiko peke yake. Ilibidi nijiteke ili ukombozi upatikane ingawa niliishia kukumbwa na kesi ya jinai.
Baada ya kujiteka si mambo yalitibuka baada ya walevi kuingia mitaani na kuzidiwa nguvu na ndata. Isitoshe kuna walevi wenzetu waliostukia mpango mzima na hivyo kuupinga wazi wazi jambo ambalo lilinimaliza nguvu nikaamua kutoka nilikokuwa nimejificha kwa aibu.
Pamoja na dili langu kubuma nimejifunza mambo mawili matatu. Ukitaka kujulikana kwenye kaya yetu fanya fujo ukamatwe na ndata. Amini usiamini utapata majuha wengi wa kukuunga mkono kwenye kila bangi utakayokuwa ukiipigia debe.
Pia nimegundua kuwa walevi wengi wana hasira hasa baada ya kunyonywa sana na mafisadi. Ingawa wameshindwa kupambana na mafisadi mmoja mmoja au wote kwa pamoja kutokana na woga, wakipata mtu wa kuwachochea kumbe wanaweza kuwa vifaa huko tuendako!
Pamoja na kuwa na hasira, walevi pia wana kisasi na mafisadi, sema hawajui kupambanua nani wa kushughulika nao kwanza. Mfano mzuri ni juzi tu walipoamua kutaka kupambana na ndata wakati adui wao mkubwa ni mafisadi. Mara hii mmesahau mafisi kama Eddie Ewassa wanavyogawa mifweza ya wizi kwa vijiwe mbalimbali! Hawa ndio wa kufa nao badala ya ndata wasio na tofauti na mbwa na amfugaye.
Pia nimejifunza kuwa hata mafisadi nao hawana mikakati ya kuona mbali. Wakibanwa mbavu wanahaha na kuparaganyikiwa kama jamaa zangu waliofungulia masoja kwenda kufanya kazi ya ndata. Kwanini nasema hivi? Hebu angalia jinsi ambavyo akina Shehena Fuadi na Pondwa Pondwa walivyowajambisha ndipo wakakumbuka kufunga eti vyombo vya umbea vilivyokuwa vikitumika kuhubiri chuki na ngoa.
Kwani hawakujua kuwa vyombo hivi vya udaku havikuanzishwa kuelimisha na kuiburudisha jamii zaidi ya kuichafua, kuijaza ujinga na kuihuzunisha. Hawa jamaa nao wamezidi kwa ujuha na kujisahau.
Unakumbuka wakati wa Ben Tunituni bin Makapu alisemaje vyombo vya umbea vilipombana kuwa alikuwa fisi na fisadi? Aliviambia kuwa kama navyo si fisadi vieleze vilipokuwa vimepata mitaji ya kuanzishwa.
Sasa hawa jamaa walipoona vyombo hivi vya umbea vinahubiri maangamizi, wao wakatumia vyao kuhubiri chuki dhidi ya vyama vya upingaji.
Ngoja nirejee kwenye kisa changu cha kujiteka na kudai nimetekwa. Kwa ufupi ni kwamba nimejilaumu baada ya kugundua kuwa kumbe mambo si rahisi kama nilivyodhania. Pia niligundua kuwa kumbe si walevi wote wanaoniunga mkono. Hata hivyo, sitachoka.
Kama watafanya mchezo kama walivyofanya kwa kufanya mambo kwa nguvu ya soda, nitakuja na mikakati mikubwa ya kuchukua kaya kwa njia yoyote bila kujali kama ni halali, haramu, salama ama hatari. Walevi kaeni mkao wa kuliwa kama hamtajifunza kutokana na haya yaliyopita.
Naona gari la Jei Wii. Acha niishie wasije kunikamata kwa uzushi wangu! Hivi kunguru na mwewe nani kiboko ati? Acha nijikate kabla ya kunikamata na kuninyoa madevu yangu kama yule jamaa!
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 31, 2012.

Sunday, 28 October 2012

The bad the ugly and the good and miracle performers of Bongo



Looking at EddieWhitehair Lo- Wash doling money out for whoever that approaches him, one’d see love of the rich to the poor. Again, is this love true or has something else? Since he’s forced out of power thanks to Richman Scam, Eddie’s become a very generous politician Bongo has ever had. He does not budge when it comes to dishing out millions. He loves churches even mosques. Ironically, such places are called the places of God! Which God between god money and God Almighty? Aren’t those dens manned by jackals and hyenas Jesus admonished us to be aware of? Mwl Mchonga added that we’d fear such crass putas like leprosy if we want to be safe. Again, who bothers? 
If you want to get Eddie’s dosh just come with the media guys and invite him to anything you deem fit. He surely will come and make you rich. More often than not, those who don’t know how the media operate have always been quick to accuse the media as part of this sellout. Nay guys; ours as media, is to cover events regardless the one making news is a devil or an angel. This is the bottom line. Again, this does not mean that Kanjanjas are not out there abusing and breaking all rules in the books.  Verily, they’re there selling themselves like twilight girls of Ohio and Kinondoni. Technically, we call this professional prostitution just like political prostitution the money has created recently.  
Back to Mr. Plutonic Eddie, when he rakes money out in his spin nobody bothers to ask if his money is legally or illegally gotten. The power that-be has always mollycoddled him and people have taken it seminally! Aren’t, this way, people blessing thuggery and corruption? Who care if at all money talks?  Baniani mbaya (literary bad banyan’s shoe is a cure). A dead donkey does not fear hyenas. You know who is a dead donkey and who hyenas are. What a systemic malady of corruption so to speak? Why don’t we have such courageous people especially men to take on the guy and tell him to his face that we need our Richmond money back? Are we such gullible and greedy in the first place? Miraculously, even Mr. Prezzo who has always made us believe he is there to fight corruption is silent!   
By and large, people know that this ‘generosity’ is temporal by nature. In a simple parlance, this game is known as kutumiana namely to fool each other. Again, blessed is the hand that giveth than the one that taketh. In future, someone will suffer such a humungous blow.  The equation is so simple.  Recipients will be made to pay dearly. What is evil is the fact that at this moment of truth, major victims will be our children.
Given that people have consented to being bribed and fooled with their own money, whose fallacy is this? Again, dudes, if you’ve blindly and pointlessly accepted this hanky panky generosity, don’t take it for granted. For, from now on to October 2015 it’ll exist. Thereafter, tell it to the birds. If he gives you any coin come jeer at me and call me a liar.  Ironically, since some smart guys invented Uhujumaa na Kujimegea (kleptocracy and Selfishness) to replace Socialism and Self-reliance under Zenj Declaration, all opportunists decided to seek power. Those who still remember and adore Arusha Declaration must commit suttee or hara-kiri.  
Things have changed tremendously. We used to get good leaders based on principles, ethics, vision, handwork and what it takes. Currently, money, dirty money, has taken over all those good virtues. Yeah. Show me just one leader who did not buy his way to power today. Not in this deadly venal hunk of ours. Anybody can become president, bishop even sheikh. For those who aspire to become president just like Eddie, it is simple. Grab money from anybody and spend that money on buying political loyalty. This way anybody can become president. Thus, never wonder when you hear guys like Andy Chenge or mzee wa vijidosh wants to become one. Everybody likes to become president especially at this punkish and thieving era. The zinger is under such rotten atmosphere after becoming president you can steal as much as you deem fit to reimburse yourself the money you spent on getting votes. Nobody will put you to task given that all you are manning are conspirators thus thieves by consent. This is where the root of zilch accountability and performance for many afro-president lie. You can become as Mobutu as you like and nothing will happen to you. You know what? Whoever that will try to lay you bare will be hated and persecuted. Have you forgotten how Jesus was treated while a thief Barabbas was adored?    And don’t buy a pig in the poke. Who’ll douse this fire?
Source: ThisDay Oct,. 29, 2012

Wednesday, 24 October 2012

Corruption in Africa: The Dilemma

Almost every African country is currently facing corruption and has an “anti-corruption” body. These bodies are known by various good and serious names such as Takukuru (Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa) Tanzania, Kenya Anti-Corruption Commission (KACC) and Anti-Corruption Coalition Uganda (ACCU). Even DRC despite being tainted with corruption, hopefully had an anti-corruption corps.
Although impunity involving those manning anti-corruption bodies is quite known for many Africans, the recent conviction of Nigeria’s anticorruption agency EFCC’s officials is a slap in the face to the government. Douglas Williams and Abba Ishaku were recently convicted for asking a bribe of $ 630 from a politician in order to stop investigating him. The amount of money is so small. This suggests that even the officials in question are junior. What transpired in Nigeria is but a typical replica of what has been going in Africa. African anti-corruption agents are antithetic to what they say they are fighting. They can deal with “everybody.”
Under every rule, there is an exception - they cannot deal with politicos and sacred cows in the country. Most of the anti-corruption agencies intimidate and dupe the general public and donors that their respective governments are fighting corruption. Most of these carbuncular creatures of corrupt regimes are under the office of president like Takukuru. Their modus operandi towards their masters goes with a proverb: asking me no questions; I’ll tell you no lies. How can a corrupt regime fight corruption? How can a government that came to power by rigging fight corruption?
Anti - corruption agencies are being used by corrupt rulers as diapers to clean and conceal their messes. For example, Africa's minerals are stolen every day but nobody is brought to book. How can anti-corruption agencies tackle corruption while there is no ethical grounding in African governing systems? How can anti-corruption agencies take on corruption while they are doing so in Nigeria style of “give me what’s mine otherwise you face it.” In Africa, any thief can plunder and become super rich for no ethical rules are in place for individuals to declare how they acquire their wealth. 
Power in Africa is a family business. The President’s power is used by family members and friends to solicit loans from the banks and other preferential treatment. Anti-corruption agents neither see them nor take on them. To show how smarter anti-corruption agents are, they make their own killings and this is why many of the officials of anti-corruption agencies are rich due to sound salaries and kickbacks they receive in order to “fight” corruption. 
We need independent bodies that can take on whomever no matter what. This must be stipulated in the law. One can’t fight corruption without pertinent ethics in place. Africa needs the same code western countries use. Everybody must give an account of how he or she made her wealth. By having such accountable and responsible codes, Africa will be able to forge ahead. Are African strategies to fight corruption monkey business or another display of hypocrisy and megalomania?
Source: The African Executive Magazine Oct., 24, 2012.

Tuesday, 23 October 2012

Serikali ijilaumu kwa kuufuga udini


HIVI karibuni taifa letu limekuwa gumzo kwenye vyombo vya habari vya kimataifa. Hata hivyo, si kwa sababu nzuri bali uchomaji wa makanisa uliotokea baada ya watoto kufanya utoto kutokana na kufundishwa imani potofu na za kishirikina.
Chanzo cha yote ni ubishi baina ya watoto wawili mmoja mkristo na mwingine Muislam kuwa akojoleaye au kuharibu, kutemea mate Korani aweza kugeuka mjusi hata kufa.
Hakuna anayeunga mkono kitendo hiki hata kama ni cha kitoto. Kadhalika, hakuna mtu mwenye akili na nia nzuri anayeweza kuunga mkono matokeo ya kadhia hii.
Katika utoto huu mmoja wa watoto aliamua kufanya majaribio kujua kama alichoambiwa ni ukweli au la. Baada ya kufanya hivyo bila kufa wala kugeuka mjusi, tunaambiwa mwenzie alichukia na kwenda kuripoti kwa wazazi.
Kimsingi, watoto wamefanya utoto kiasi cha kuwaingiza mtegoni watu wazima kushabikia na kufanya utoto zaidi. Wanaojiita waislam wenye ajenda zao za siri walipata fursa ya kuhubiri kiama huku wakishinikiza makanisa yachomwe!
Je, hii ni busara, elimu au dini aina gani isiyotumia hata chembe ya akili? Akikosa mkristo au mkwere mmoja basi unaadhibu wakristo au wakwere wote!
Ili kuona kama kweli kulikuwa na haja ya kujichukulia sheria mkononi ngoja tuhoji. Je, Korani ni nini? Korani ni kitabu sawa na vitabu vingine ukiondoa kuwa husemekana kuwa kimetoka kwa Allah. Ukiondoa hiki kitabu tunachoona, Korani si vile vitabu tunavyomilki bali ujumbe ambao mtume Mohammad (SAW) alikuwa akipokea na kuwakaririsha wafuasi wake.
Ni ajabu: Mohammad alipokufa, aliacha kila kitu kwenye uislam ambao alisema aliukamilisha isipokuwa kitabu kinachotugombanisha.
Je kwa msingi huu, hii Korani (kitabu) ambayo hata mtume hakuiacha inakuwaje inapewa umuhimu kuliko hata ubinadamu?
Binadamu ameumbwa na Mungu. Korani imetengenezwa na binadamu. Huu ni ushahidi ima wa ushirikina au kutojua mambo.
Nasema hivyo kutokana na ukweli kuwa anapochomwa moto kibaka kwa mfano ambaye ni kazi ya mikono ya Mungu, watu hawaandamani wala kuchoma makanisa.
Ajabu kikichomwa kitabu kazi ya mikono ya binadamu watu wanakamiana na kutaka kuuana! Je hapa kweli tatizo ni kuchomwa kitabu au kuna jingine?
Si uzushi wala upendeleo kusema kuwa serikali yetu imefuga hisia za udini nchini mwetu. Maana kumekuwa na watu wanaoota ndoto za mchana kuwa kuna siku Tanzania itatawaliwa Kiislam au Kikristo.
Ila wanasahau kuwa uislam haujawahi kutawala popote ukiachia mbali baadhi ya watawala kuutumia kufikia malengo yao. Mfalme Constantine aliutumia Ukristo kutawala Rumi, Ezana (Kush) huku watawala wa Ottoman, Mughal na Safavid nao wakiutumia uislam kujiimarisha kwenye madaraka.
Je, chanzo cha manabii wa vita na machukizo kama vile Uamsho na wana mihadhara ni nini? Ni ulegelege wa serikali bila shaka.
Tunao wahubiri wengi wa kiislam wanaotumia Biblia kushawishi watu kuwa waislam pasina kutumia Korani kutokana na kutoijua wala kusoma dini.
Hili ndilo kundi kubwa lenye mashehe wa kuzuka kama huyu anayehubiri machafuko aitwaye Issa Ponda Issa ambaye shehe mkuu Shabaan Simba alisema si shehe wala msomi, bali mhuni wa kawaida anayetafuta riziki kwa kujificha nyuma ya joho la uislam.
Leo tuna makundi yenye kila alama za ugaidi kama Uamsho yakijidai kupigania haki za waislam hata watanzania. Ukiwauliza aliyewachagua na kuwatuma hupati jibu zaidi ya kuvunja sheria ya nchi.
Hawa na wale wa kikristo wamekuwa wakiwapigia watu kelele bila hata kujali kuwa wanahitaji utulivu. Leo, kwa mfano, ni hatari kulelea mtoto kwenye baadhi ya maeneo jijini Dar kutokana na kelele zinazotoka misikitini na kwenye makanisa hasa ya mikesha.
Kinachofanya serikali ilaumiwe ni ile hali ya kuruhusu kila mtu kujifanyia atakavyo bila kufuata serikali. Madhehebu ya dini yalipaswa kusajili kwa sharti kuwa yakienda kinyume na matarajio ya serikali yanafutiliwa mbali.
Leo tuna maaskofu wengi feki wanaotumia dini kuwaibia maskini na kuwadanganya wanamchi kila uchao.
Tuna mashehe wengi wanaoibuka na kutangaza vitu vya ajabu kama hawa wanaotaka kuangusha Bakwata au kutaka kueneza uislam wa kihafidhina ambao hata Mtume hakuuacha.
Hata hivyo, inapaswa watu wa namna hii kuambiwa kuwa tulipopigania uhuru tulipigania uhuru kama watanzania na si waislam wala wakristo. Mtu yeyeto aweza kuingia dini yoyote na kutoka lakini hawezi kufanya hivyo kwa uraia wake kirahisi hivyo.
Kwenye kujiunga na dini hakuna maombi wala masharti sawa na uraia. Mbona wakati tukiingizwa kwenye mfumo wa kikoloni au kupelekwa utumwani hizi dini zinazotaka mamlaka leo hazikutusaidia zaidi ya kuwa wakala wa mateso yetu?
Kuna haja ya kusoma historia kuepuka aibu ya kiakili kama hii. Hivyo, hawa al muthnaka wanaoota mchana kudhani Tanzania inaweza kutawaliwa kidini, washikishwe adabu mara moja.
Ni upuuzi na utaahira ukiachia mbali uchizi kwa watanzania maskini kujificha nyuma ya imani za kimapokezi na kimamboleo hadi kuchelea kumalizana. Ni ajabu leo watu wanahamanika hata kufikia kutaka kutoana roho kwa mambo mepesi wakati mambo mazito kama kupambana na ufisadi wanayafumbia macho!
Kimsingi, Tanzania hakuna udini bali uchovu wa kifikra na umaskini wa kunuka.
Sioni tatizo baina ya wakristo na waislam ukiachia mbali wahuni na matapeli wanaotumia dini hizi kuleta vurugu.Hatuwezi kuwahukumu waislam wote kwa ujuha na ajenda fichi za makundi madogo ya kitapeli yenye kufadhiliwa na maadui wetu.
Tumekuwa mafisadi hata wa kiakili kirahisi hivi? Mbona hatuongelei viongozi mafisadi wa kiislamu wanaowaibia na kuwatumia waislamu maskini sawa na wale wa kikristo wanavyowaibia wakristo?
ACHENI UVIVU WA KUFIKIRI na kulialika janga ambalo hamuwezi kuli-contain. Tukianza vurugu wengi wa watu wetu hawatakufa kwa matundu ya risasi bali, njaa baada ya kushindwa kwenda kuhangaika maana ni maskini mno; hawana hata ujanja wa kutorokea nje-hawana pasi za kusafiria wala pesa.
Tuwaacheni waishi maisha yao ya mahangaiko yanatosha, Tatizo la nchi yetu siyo udini bali ufisadi wa kimfumo hata wa kidini.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 24, 2014.

Tatizo letu si udini, bali uduni


BAADA ya kunuka au kuumana hivi karibuni kwenye kaya yetu ya amani, mzee mzima nimeona nitoe busara na elimu bure ili kuepuka kujitia kitanzi kijinga na kipofu.
Laiti ndata wasingekuja Kijiweni na kutulipulia mibomu yao ya michozi wadhani ningenena?
Ningewaacha wamalizane kwa vile wamefugana na kufuga ujinga na ujanja ujanja wao wenyewe huku wakitudharau sisi ambao hatuhusiki na ligi yao ya kuaminisha walevi imani zao.
Ni juzi tu watoto wawili wameonesha utoto wao na ushirikina unaoashiria mafunzo mabaya kutoka kwa wavyele wao.
Si mitoto mitukutu ilibishana kuwa mmojawapo akikojolea msahafu atageuka mjusi au kufa. Kutokana na ukosefu wa busara si mitoto ikaamua kufanya kweli. Wallahi naapa angekuwa kijogoo wangu siku hiyo ningemfungia kwenye gunia kwa muda ili ajifunze kufikiri.
Nisingekurupuka na kuanza kuchoma ma-church wala kudhani kuwa Manaswara ndiyo maadui zangu. Nisingefanya hivyo kwa vile adui alikuwa nyumbani mwangu saa nyingine mimi mwenyewe kumfundisha mwanangu mambo yasiyoingia akilini.
Haya ya watoto tuyaache. Huo ndiyo utoto wenyewe. Leo nalonga na wakubwa wenzangu hasa wale walioshika maulaji na madaraka kulea ujinga umaskini na ufisadi kiasi cha watu wetu kuanza kuwa na imani mfu na hatari.
Laiti watu wetu wangelikuwa wamepiga shule wangejua kuwa kwa mfano misahafu ni makaratasi yaliyotengenezwa na binadamu ili kuwawezesha kujitawala vizuri.
Wangejua kuwa miili yao ina thamani kuliko makaratasi. Wangeoogopa hata kuchoma vibaka kuliko kuogopa hata kuwa tayari kutoana roho kwa ajili ya makaratasi.
Kijiweni tulishangaa kusikia eti watu wanafia misahafu. Hawakusoma hawa? Huwezi kunajisi misahafu. Ukijitahidi kufanya hivyo utanajisi kitabu lakini si ujumbe wa Mwenyezi Mungu Subhana Wa, taala. Misahafu siyo tabu bali ujumbe wenyewe.
Kwani mnadhani kipenzi chake Allah Sayyidna Muhammad (SAW) alikuwa juha kama nyinyi siyo? Mnajua ni kwanini hadi anafariki hakuwa ametoa idhini ujumbe wake uandikwe kwenye makaratasi zaidi ya mioyo?
Alichelea uvivu wa kusoma kusababisha watu waache kuhifadhi na badala yake wategemee matabu ambayo sasa yanawagombanisha.
Mnadhani Mtume alikuwa zoba kama nyinyi siyo? Kwanini hakuacha amejenga misikiti ya bei mbaya ilhali alijua hekalu la mfalme Suleiman? Niwasaidie, alitaka dini isiwe mzigo bali nyenzo ya kuwafanya watu kuishi kwa furaha na si karaha na kuchukiana. Ukimchukia mwenzio elewa huna dini tena.
Kweli aliyewaita Bongolaland hakuwaonea. Mnagombea nadharia huku mkiogopa hata kugombea mambo yanayowahusu kila uchao? Mbona hatuoni jazba kwenye kupambana na ufisadi na dhuluma?
Ni walevi wangapi wanalanguliwa na wenye mbavu za mbwa mnazoita nyumba ambao wengi wao tena huapa kila mara bila kujali kuwa wana dini? Je, wezi wa namna hii wana dini au mauza uza? Nikimuona mama mwenye ubavu wa mbwa wangu anavyoapa hovyo hovyo na matendo yake nachukia hizi imani kusema ukweli.
Leo mmeruhusu wahuni wahuburi maangamizi na matusi hata bila kuwaonya! Hao mashehena wanaojifanya walimu na magwiji wa dini hasa Ugalatia walisomea wapi kama siyo kuendeshwa na njaa? Wengi hawana hata kazi achia mbali elimu zaidi ya kupiga mikelele.
Mbona hakuna mahali mtume alihubiri ubovu wa Baibulo la moyo wa chuluka jamani? Si aliikuta na kuiacha? Msitupigie kelele na uongo na ujinga wenu.
Mnadhani tunapenda hiyo mikelele na mikesha yenu? Tafuteni kazi au njooni Kijiweni tuwape misheni ya jinsi ya kupambana na ukwe.. na ukapa huu tulio nao.
Tukikwambia kuwa tunapata bangi ili kuondoa mawazo mnatuona makafiri wakati nyinyi ni wabaya kuliko sisi.
Maana bangi zetu tunavuta wenyewe wala hatulazimishi na wengine kuvuta bangi zetu kama nyinyi.
Hivi kama mwili wote ungekuwa sikio jicho lingekuwa wapi? Kila mtu anatuhubiria uzuri wa dini yake wakati tunaona matendo yao ya kutisha.
Kama mmeshindwa kutatua tatizo la kitoto kama hilo mtatatua matatizo yetu au mnataka kutuingiza kwenye matatizo yenu.
Nyinyi mnapata wapi? Kwanini mnatuletea bidaa mchana kweupe halafu mnataka kutumia bidaa zenu kutugawana. Mshindwe na mlegee nasema.
Wabongolalalanders wana matatizo yao mengi. Wanakabiliwa na ukapa na ukwe.. We stop! Wanasumbuliwa na ufisi na ufisiahadi na siasa za Uhujumaa na Kujimegea.
Kwanza, wengi wa wabongolalalander hawana dini na kama wanayo basi si nyingine bali kutafuta utajiri.
Hamuwaoni wale wachunaji wanaojiita wachungaji au mashehena wanaojiita mashehe. Shehe aweza kuhubiri vita na upuuzi au mchungaji miujiza na kuwadai watu sadaka? Acheni njaa zenu na wazimu wenu tujenge kaya.
Juzi nilisikia wajinga fulani wakisema eti Bongolalaland inatawaliwa kwa mfumo Christ! Toba! Mfumo Christ chini ya shehe! Mnamdanganya nani jamani? Mijitu iliyolewa chuki eti inasema lazima tutangaziane vita! Hivi vita mnaijua au mnaisikia?
Tukianza vita wajua tutakufa si kwa matundu ya risasi bali njaa? Mijitu yenyewe makapuku ya kunuka?
Hamna tofauti na mipumbavu inayokula nyama kila siku halafu ikaanza kulalamika eti haipati maharage.
Wenye nazo wakianza kupanda mipipa kwenda kuishi ng’ambo nyie mtanukia kwenye mbavu zenu za mbwa.
Hivi umaskini au maradhi na ujinga vinajua dini? Mbona kwenye mbavu za mbwa za kupanga hambaguani isipokuwa kwenye vichwa vyenu wana hizaya nyie?
Jamani tupeni fursa tupambane na matatizo ya kweli badala ya haya ya kuumba.
Tuondolee mbu na uvivu wenu wa kufikiri jamani tupambane na umaskini tuliotengenezewa na mafisadi ambao dini yao ni utajiri. Tena kabla ya kusahau.
Mbona mafisadi wote wana dini moja ingawa majina yao ni ya Kizungu na Kiarabu?
Waijua dini ya mafisadi? Inaitwa Almight Money bin Senti bin Fwedhaa. Wamjua Mungu wao?
Matumbo na tamaa zao. Leo mnajitia kiranga halafu ndata wakiamua kuwatia adabu mnaanza kulalamika. Acheni mauza uza tufanye mambo ya maana.
Acha niwape vipande vyenu. Tatizo la Kaya yenu si dini bali uduni na ujinga. Nasikia mibomu. Sijui nani kakojolea nani tena?
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 24, 2012.

Monday, 22 October 2012

I love our chummy laws and their enforcement


This is the song of peace
It aims at all S.O.B's and D.O.B's
You guys in fatigues
With your totting guns
Trigger happy as you always are
You the killing machines,
You who violate peace
You who are used by morons
Guys,
When you kill, just kill peacefully
When you rape just do it peacefully
You venal and thievish nobles
When you steal just do it peacefully
Do even your corruption peacefully
For this is the hunk of peace
Peace in everything you do
Cops, officials and all courtiers
When you act, please act peacefully
I am talking to everybody
All sheep and hyenas
Noble and disgraced
Please observe peace
Again I should insist
That those suffering should not accept this
Stand up for your rights
Avoid and hate this elusive peace
Do your pacifism and passivism work hither?
Peace that leave in pieces
Just fight straight on and head on
Fight this Criminal Cabal of Murderers (CCM)
Fight all Coveted Oppressive Parloiners (COPS)
Fight all noble thieves and their majordomos
Fight fight everywhere
The poem above reminds me of the poem I wrote for myself when I found that I can’t do anything to prevent the dooms our people were being driven to.
In our good country and under our gentle laws, if you happen to be smart you can get away with it.
You can rob the public, indulge in capital flight, sabotage, receive kickbacks especially when signing such fat investment contracts and stash your money to offshore banks and nothing sinister can happen to you.
If you happen to use gun especially if you are a cop, you can shoot anybody you dislike under any pretext and nothing sinister can happen to you. You can sleep on the wheel if you are CEO of public business such as government and whatnot and nothing can happen to you. You can rig elections under the science of uchakachuaji and the heavens won’t fall on you. No law can reign on you even if what you are committing is pure impunity. This is why I like our gentle and humble laws. Again, don’t take our laws for a ride. They will not only ride on you but run over you especially if you contemplate stealing chickens or valueless things like receiving small kickbacks or indulging yourself in political ambitions under opposing parties; on this our law will nary treat you gently.
The other day I heard people shouting at the top of their voices that they’re not going to be counted during the national census. No law dealt with them. Others went a mile ahead as saying that they’d like their religion to be included in the census as if we were looking for priests and sheikhs. Again, our generous laws did not bite such people who were trying to use religious wisdom to gain political mileage. Under our generous laws, if you are smart or connected, you can do as you like without fearing anything.
I recently heard that some illegal immigrants came to the country and grabbed land and no law bit them. So too, I heard that some coveted illegals were even able to proselytize and nothing happen especially when they started preaching violence. Motorists enjoy our laws. Break them. The traffic officer calls you aside and you just valorize the law and that is that. Drug dealers know it well. Pay an officer at the airport handsomely and your cargo just passes sleekly.
True, our laws are almost generous to everybody except the wretched of the country. If you are an honourable MP you can sleep in the house, tell lies, do nothing to your constituency and the laws hug you instead of biting.
Sometimes back I heard some ballyhoos that the power that-be would take on thugs and drug dealers. Again, when it came to light that those guys were the funders of a certain powerful party this project was abandoned indefinitely. Who would like to cut the hand that feeds him? You can take this to the bank. Ask chaps like “the old man of vijesenti” Endelea Chenga and his pal Dr Idd Rashid. They’ll tell you how gentle, civilized and generous our laws are. You know what? It came to light that those guys stashed billions of dough abroad. Our laws, instead of biting them, they hugged them so as to be given even more ulaji in the house. Do you think I am making this up? Don’t sweat it. Ask Eddie Luwasha who was openly implicated in the Richman scam. He patriotically relinquished his PMship and went on becoming a chair of a powerful house committee plus being availed with all emoluments, pochopochos and whatnot all former PMs get.
To cut a long story short let me surmise saying long live our civilized and generous laws and the soft way they are enforced to see to it that we remain the hunk of peace.
Source: ThisDay Oct.,22 ,2012.

Saturday, 20 October 2012

Serikali inamdanganya nani kuhusu mihadhara

    
   Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Saidi Meck Sadiki alikaririwa akisema kuwa serikali imepiga marufuku mihadhara ya kidini inayokashfu dini nyingine hadi hali itakapotulia. Mihadhara hii imekuwa ikiendeshwa na kushabikiwa na waislam hasa wa kada ya chini hasa wasio na elimu ukiachia mbali kudhaminiwa na wafanya biashara wengi wenye asili ya kiarabu. Huu ni upuuzi. Kwanini kuipigia mihadhara marufuku hadi hali itakapokuwa shwari wakati wameishakiri kuwa inakashfu dini za wengine? Kinachokera ni kwamba hawa wanaojifanya wahubiri hawana elimu si ya Ukristo wala Uislam bali njaa na kutafuta sifa. Kuna haja ya kufanya mihadhara kuwa kosa la jinai hasa wahusika wanaposhambulia dini nyingine au kutokuwa na elimu juu ya kile wanachohubiri.
        Hii imekuwa staili ya serikali yetu ya nguvu ya soda katika kupambana na matatizo. Leo tunaambiwa hata Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar (SMZ) nayo imepiga marufuku mihadhara ya wana Uamsho. Too late. Mwanzoni chini ya kihoro cha kutaka muungano SMZ iliridhia na hata kushirikiana na Uamsho kuhubiri chuki na dhihaka dhidi ya muungano ikidhani ingeweza kuwatumia kufikia ajenda zake bila kujua kuwa nao walikuwa na ajenda zao fichi. Maalim Seif Shariff Hamad alipigia upatu hili . Kwani hii imekuwa ajenda yake tangu akiwa CCM hata baada ya kufukuzwa CCM na kurejea kwa mlango wa nyuma chini ya kisingizio cha serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) ambayo hata hivyo inamhusu yeye na si chama chake. Leo wamegundua janja ya kutumiana wanaamka na kuanza kupiga mihadhara marufuku. Yote hii ni matokeo ya kuwa na watawala wasioona mbali.
           Hakuna anayehitaji mihadhara katika maisha. Mbona mihadhara imeanza juzi juzi miaka ya 90? Mbona kabla ya hapo tulikuwa tunaheshimiana na kupendana. Kesho wataibuka wahubiri wa mihadhara wa Kikristo waanze kuonyesha udhaifu wa Uislamu na waislamu wataanza kuja juu na kuchoma makanisa kutokana na kutokuwa na subira. Je namna hii tutafika? Maana kila dini ina udhaifu wake. Ndiyo maana dini zote hupenda kuwaaminisha watu badala ya kuwaelimisha. Hivi kwa mfano mtu leo akija anaongelea maisha ya Khadija mke wa kwanza wa Mtume aliyemwamuru Mtume amuoe si watu mtakatana shingo bure?
            Wengi wa waendesha mihadhara ni watu wasio na kazi ambao kimsingi ni wanyonyaji. Hata Uislam kama utatafsiriwa vizuri unazuia ujinga huu. Sayydina Omar ibn Al- Khatab Khalifa wa pili alipiga marufuku watu kumaliza salat na kuendelea kupiga mdomo wakiswali taraweh badala ya kwenda kufanya kazi.
Ila baada ya Tanzania kuruhusu utapeli wa kutumia majoho ya dini, tumeshuhudia kuibuka utitiri wa mihadhara na madhehebu ya kikristo mengi yakiendeshwa na matapeli wanaotaka utajiri wa haraka.
Je serikali inamdanganya nani zaidi ya kujidanganya na kulea huu uhuni usio na faida kwa watanzania?

Friday, 19 October 2012

Vurugu za kidini je ni akili kumfia Mungu asiyekufa na mwenye nguvu?

Kinachoendelea nchini Tanzania ambapo vurugu zimeishatokea kinaelezewa kama vurugu za kidini. Je ni kweli ni chuki za kidini au kukata tamaa kwa watu wetu? Nimejaribu kujihoji na kuhoji mantiki ya mtu ambaye ni kiumbe dhaifu kuliko vyote kuwa tayari kuua hata kuuawa eti kwa ajili ya ima dini au Mwenyezi Mungu. Nashindwa kuelewa kutokana na ukweli kuwa Mungu hafi ila binadamu anakufa. Je hapa wahusika hawasemi ukweli kuwa wanapambana kupata maisha bora kwa wote kwa kutumia mgongo wa dini? Kama tutamfia Mungu asiyekufa yeye Mungu atafanya kazi gani? Kwanini tufie dini zake wakati mwenyewe yupo anaangalia? Je sisi ni vichaa na mataahira au ni wajanja wenye hoja fichi? Wanangu nataka maoni yenu lau tujadili jinsi ya kulielekea hili. Maana tukilinyamazia litalimaliza taifa letu.

Kikwete toa tamko na msimamo wako





Ingawa wengi ambao tumekuwa tukikosoa staili ya utawala wa rais Jakaya Kikwete, tumeonekana wabaya. Ingawa lengo letu ni kumsaidia kufanya anachopaswa kufanya badala ya kugeuka kiguu na njia kila siku angani akizurura ughaibuni, tunaonekana wabaya. Hakuna ubishi kuwa nchi yetu sasa iko msambweni ikitishiwa kusambaratishwa na udini utokanao na ujinga, ukosefu wa ajira, usongo na husda kwa baadhi ya watu wetu tulioshindwa kuwaendeleza. Hapa ndipo unatakiwa uongozi wenye visheni na mipango madhubuti ili kupangua  janga hili la kujitakia. Kumekuwa na malalamiko kuwa serikali inatumia nguvu nyingi kupambana na upinzani badala ya kutimiza wajibu wake. Jeshi la polisi limekuwa jepesi kuwahi kusitisha mikutano ya upinzani. Bila kujua kuwa kuna upande mwingine ambao umekuwa ukiutumia udhaifu huu, sasa serikali inajikuta uso kwa uso na wahafidhina wenye hoja zao fichi. Je ni wakati wa utawala wa Kikwete kuwekwa kwenye mizani au kuumizwa na wale uliowadharau na kuwafumbia macho. Ingawa tunaona machafuko yanayoendelea kama matokeo ya udini, ukweli ni kwamba ni matokeo ya ufisadi, umaskini, ujinga, ufisi, uroho na kasumba.
Watu wetu wengi hawana ajira na hawajui kesho yao itakuwaje. Wamekata tamaa na wanaweza kutumiwa na yeyote awezaye hata kuwaahidi jibu achilia mbali kutoa hilo jibu. Hii ndiyo maana hot spots za vurugu ni kwenye makazi ya watu maskini kama vile Mbagala na siyo Oyester Bay wala Masaki. Walioko kule wana uhakika wa maisha wagombee au kuandamana kwa kitu gani?
Sasa Kikwete amerejea. Tumshinikize atoe mwelekeo wa taifa. Kwa mazoea yake ya kutojali unaweza kuambiwa kuwa kesho ana safari ya kikazi kwenda nje. Amekuwa akituchezea akili hivyo. Kila kukitokea matatizo Kikwete na genge lake wako nje wakitanua huku umma wetu ukiendelea kuteseka. Amekuwa akitumia jeshi la polisi kuzuia rabsha. Sasa ameishiwa hadi anaanza kutumia jeshi ambalo kikatiba kazi yake ni kupambana na maadui wa nje na si wa ndani.
Tumalizie kwa kumuasa Kikwete kuwa kama hatabadili staili yake ya kutawala ataiweka nchi pabaya. Ameacha mambo yajiendee ambapo kila tapeli anaweza kuanzisha dhehebu au kundi la dini kama walivyofanya Uamsho na Ponda Issa Ponda. Tunao wachumia tumbo wengi waliojificha nyuma ya majoho ya dini kutokana na kuujua udhaifu wa Kikwete. Rais Kikwete toa tamko na msimamo kuhusiana na mwelekeo wa taifa letu.
Mungu ibariki Tanzania.