The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Sunday, 11 October 2015

As we celebrate Mtikila






















            It is doubtlessly a great loss.  We grieve and weep for the the loss of the person –Rev Christopher Mtikila – an amiable man who kept political dialogue in the hunk always alive. Controversial as he was, Mtikila was the force to reckon with as far as Bongolalaland’s political landscape is concerned. Boozers were shocked and dismayed to learn about the untimely demise of their colleague.
             I personally knew Mtikila before becoming a megastar politician. I vividly recall. We used to meet at Mnazi Mmoja garden or Shule ya Uhuru Mchanganyiko grounds. It is at this time Mtikila was starting to build his political resume as he launched himself as a public intellectual. Mtikila was a good person to dialog with, so astute and charming that everybody would appreciate nattering with. He indeed, was a good chatterbox that seemed to know many things. Despite his low-slung edification, Mtikila was a self educated dude that died an icon as far as the second liberation of the hunk is concerned.
            Mtikila is the only person who lugged me into participating in the demos for the first and last time so to speak. It was at the time when he launched his “Operation Equality” when he wanted all Bongolalanders to treat each other equally. Despite not supporting his take on gabacholis, I still envy his courage of the mad that sent shock waves all over the world. One of his legacy is the fact that he is the one and and only one who brought sanity in the relationships between people of Asian descent and indigenous. Before Mtikila launched his campaigns of wanting the latter to pack and go back “home” the two communities lived a very segregated life. Before going towards the way of all the earth, Mtikila coined the world gabacholis or thieves or aliens. And indeed, the traditionally secluded community –slowly and dramatically –at least, started to mingle with the former.
            No doubt, Mtikila created many friends as well as enemies for the whole time he lived. His love for his hunk was second to none. A fearless and courageous person, Mtikila became the darling of the youth. He spoke their language. He, too, was a boozer whom boozers will always remember.
            However, Mtikila –as anybody else –knew he’d not become the president of the hunk, his chutzpah, rants and raves kept the embers burning even more. Though I personally don’t endorse all of his political stances, I still respect the man for his courage and steadfastness as far as taking on corrupt and skinny politicians is concerned.
            Like any mortal, Mtikila used to rise and fall as the time went by. Up till his demise, he seemed to have been launching himself after missing out of the show for sometimes. This year, sadly though, robbed us the man who had already launched himself almost close to the tune of the one he was before dwindling sometimes back.
            Indeed, like any boozer, Mtikila –the guy who feared nothing except fear –took on the high and the mighty. He rubbed some the wrong why while he dealt a blow to many so as to leave back many of his political casualties. Mtikila was the guy who was not afraid of death. And, indeed –for the love of his hunk –Mtikila died on the way from campaigns despite being denied to run for president. He still said clearly, loudly, and openly that some of corrupt politicians were not worth to become next president. He minced no words. Eddie Lowassa knows this too well. Sometimes, one would think that Mtikila was campaigning for accountability based on anarchy due to the fact that he attacked both Joni Kanywaji Makufuli and Eddie. This left many shocked and confused altogether.
            Although Mtikila is no more, no book of history of our hunk will be complete without accommodating his name. Mtikila’s sudden death speaks to the fact that no human is forever.  I know too well. His enemies are breathing a sigh of relief as if they won’t die. His friends are shocked and saddened. Again, this is the way for everybody.  Where is Horace Kolimba who openly and courageously told his party that it had lost direction? Where is Zakayo Chacha Wangwe?  They all went towards the way of all the earth just as all of us will –one day –do without any opportunity to abscond or adjourn.
            Although Mtikila lived in this world, he wasn’t a person of this world. He was like a big fish in small pond.  However, we need to thank the creator for allowing him to be with us for 65 years, RIP Christopher Mtikila. Boozers will dearly and badly miss you especially your commitment, veracity and ability in tackling things many fainted hearts feared to touch on.
Source: Guardian Oct., 11, 2015.

Tuesday, 6 October 2015

Kijiwe chatuma wajumbe Bondeni kupinga ufisadi












            Baada ya wachovu wa Bondeni kwa mzee Madiba kulianzisha, Kijiwe kimeamua kuwaunga mkono kwa kuwateua Msomi Mkatatamaa, Mgosi Machungi na Mijjinga kwenda kuwapa tafu.
Kabla ya kufikia uamuzi huu, Mgosi ndiye aliyelianzisha, “Wagosi mnaonaje tikatuma wajumbe Bondeni kushiiki kwenye maandamano ya kupinga ufisi na ufisadi kwenye kaya ie?”
            Mijjinga anakamua mic, “Naunga mkono wazo hili la kimapinduzi mia kwa mia. Kwa vile wenzetu wanaishi kwa kutapeliwa kama sisi, lazima tuonyesha mshikamano hata kama jamaa wakati mwingine huwa hawana maana kwa kufanya mauaji ya kibaguzi.”
            Kapende anakwanyua mic, “Mie naona kama wasauzi hawastahili kuungwa mkono. Utawasaidia watashukuru lakini wakishapata wanakutolea mapanga na kudai  urejee kwenu kama walivyowafanyia ndugu zetu hivi karibuni jambo ambalo nitalilaani maisha yangu yote.”
            Msomi anaamua kutia guu, “Nakubaliana nawe kwa namna moja na kupingana nawe kwa namna nyingine. Kimsingi, kwenda kule siyo kwa ajili ya wasauzi tu bali kuwaonyesha wezi na mafisadi wetu kuwa tunaweza kufanya kweli kama walivyofanya wasauzi. Pia tunakwenda kule kujifunza jinsi walivyoorganize move nzima au vipi?”
            “Hapo nimekupata msomi wetu. Kama ni hivyo, hata mimi naweza kutia guu kule na kuonyesha makeke ili nitie tizi tayari kuwakabili mafisadi na majambazi wetu ambao kwa sasa wamehanikiza kutuahidi vinono tusijue wakishapata ulaji watatugeuza sisi vinono,” anajibu Kapende huku akibusu kombe lake la kahawa.
            Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kutia guu kwa chati, “Naona mnapoteza muda, fedha na mawazo. Yenu yamewashinda mnashobokea ya wenzenu. Nani si fisadi hapa au hajawahi kula fedha ya ufisadi?”
            “Da Sofi hebu tuombe radhi. Wewe ni wa kutuita watu wazima na wasafi mafisadi? Hebu thibitisha kama ambavyo huwa unawataka wengine wafanye,” anajibu mheshimiwa Bwege akionyesha wazi kukereka.
“Unataka ushahidi upi wakati ufisadi umekuwapo na hakuna tulichofanya kupambana nao. Hii maana yake ni kwamba tunaridhika na kufaidika nao vinginevyo tusingengoja kwenda kujifunza toka Bondeni. Unaweza binafsi ukawa hujawahi kula fedha ya kifisadi. Ila kimfumo umeishafanya hivyo hasa ikizingatiwa kuwa kwa sasa hakuna anayeuliza fedha inayomwagwa kwenye kampeni inatoka wapi na imepatikana vipi. Nadhani kaka yangu tumeelewana.” Sofi anajitetea kiasi cha kuonyesha kumshawishi kidogo mheshimiwa Bwege ambaye anakatua kashata yake na kukuna kichwa.
Alhaji Mpemba anaamua kutia guu baada ya kurejea kutoka Makka baada ya kunusurika kukanyagwa na kunyotelewa roho, “Yakhe ulivosema waweza kuwa na ukweli japo si kwa yote ulosema. Mie wallahi sioni ubaya kujifunza na kufanya kweeli kama wenzetu wa Bondeni. Nadhani walofanya wenzetu ni kutukumbusha kuwa tukishikamana twaweza. Hivo tusikatishane tamaa wala kuogopa kwenda kule kujifunza ati.”
Kanji anakula mic, “Mimi penda sana dugu yangu ya Sauzi. Veve kama najua ile Juma naibia vao, taunga kono yeye. Juma nachukua juluku najenge jumbani yake. Hii baya sana dugu yangu.”
“Kanji ni Zhuma siyo Juma. Unashindwa hata kutofautisha jina jepesi kama hili! Ukisikia majina kama Sibusiso Sibulele si utatukana bure?”    anachomekea Mbwamwitu.
“Hiyo Silele Sisiso gumu sana dugu yangu,” anajitetea Kanji na kuacha kijiwe kikiangua kicheko kwa ubukanyaji wake.
Mipawa anakula mic, “Ni kweli usemayo Kanji.  Heri ya Zuma anajenga kwao kuliko wetu wanaotoroshea nje na kutuacha maskini huku njuluku yetu ikifaidiwa na waswizi na wakameruni na wengineo kule majuu. Natamani tuwachome moto badala ya kupoteza muda kuandamana wakatuma ndata uchwara watunyotoe roho wakati nao wanaibiwa. Sijui ndata wetu wameingiliwa na kitu gani maana huko nyuma hawakuwa hivyo?”
Mzee Maneno naye anaamua kula mic baada ya kumeza kashata yake, “Heri kufa umesimama kuliko kufa umepiga magoti. Kwanini kuogopa kujaribu mbinu hizi na zile wakati mafisadi wanafanya hivyo kama vile kuhama magenge yao na kujiunga na mengine na kutaka wapewe ulaji watugugune zaidi kama inavyoendelea? Acha twendeni Bondeni hata lau tutanue kama Njaa Kaya ambaye miaka yote kwenye ulaji amefanya kazi kubwa mbili yaani kutanua ughaibuni na kuchomoa njukulu zetu na wezi wenzake.”
“Hiyo isikukondeshe. Kwani punde atajiunga na Ben Tunituni Makapi aliyependa sana kuzurura. Kimsingi, kosa wanalofanya ni kusahau kuwa cheo ni dhamana. Tambo zote zitaisha mwishoni mwa mwezi huu,” Msomi anaronga huku akibofya kisimu chake.
Mzee Maneno anachomekea, “Wana shida gani wakati wameishahomola?”
“Unadhani haya Makufuli hayatawafuna hawa jamaa kwa kufanya kosa kumuamini kuwa atawahifadhi kama walivyohifadhiana? Wangejua wakamuunga mkono Eddie huenda angewaonea huruma. Yangu macho mtanikumbuka watakapogeukana kwenye ndoa hii ya mashaka,” anachonga Kapende.
Mijjinga anampinga Kapende, “Sitegemei nyani kumfunga ngedere. Inaonekana unalewesha na hizi ahadi za kisanii anazotoa jamaa ukidhani ni mwenzako. Huyu ni mwenzao na si mwenzako ohooo! Ngoja aingie au apigwe chini utaniambia. Huyu kumbuka ni mwanasiasa. Sina imani na wanasiasa mwenzenu kusema ule ukweli. Ingekuwa amri yangu ningewataka wachovu wawabidilishe kama nepi kama wanavyobadili vyama.”

Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita fisadi Jimmy Rugemalayer! Acha tumfukuze ili kumfanyia kitu mbaya.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 7, 2015.

Saturday, 3 October 2015

Nitakavyomkumbuka Kikwete







            Bila shaka –bbaada ya kumaliza kuaga ndani na nje –rais Jakaya Kikwete atakuwaanafunga virago kuondoka Magogoni; tayari kujiunga na wastaafu.  Hata hivyo, kwa muda aliokaa madarakani –pamoja na mapungufu yake –kuna mambo amefanikisha kwa kiwango cha juu. Nitayataja mafanikio ya Kikwete bila kupoteza muda.
            Mosi, amefanikiwa kutimiza ahadi yake ya Maisha Bora kwa Wote. Kwani, si haba. Japo si watanzania wote wamepata maisha bora zaidi ya bora maisha, walio karibu ya Kikwete wamepata maisha bora na hata zaidi.
            Pili, amefanikiwa kutengeneza ajira. Kama hapo juu, kazi hizi zilikwenda kwa watu wake wa karibu, marafiki, waramba viatu. Na nyingi ya nafasi husika ni za kisiasa. Rejea kuunda utitiri wa mikoa na wilaya na kuwateua watu wake kwenye nafasi hizo. Akina Mihigo Rweyemamu, Paulo Makonda, wabunge wa dezo wa kuteuliwa, Mwantumu Mahiza, Amos Makala, Wilson Mashilingi Abdulrahaman Simbo, Jack Zoka, Charles Makakala na wengine watamkumbuka bwana huyu bila kusahau waandishi habari nyemelezi aliowatumia kama nepi kuwachafua wapinzani wake na baadaye kuwazawadia vyeo. Rejea kutea mabalozi nje hata wenye kutia shaka bila kusahau majaji na maafisa wengine. Nadhani aliposema atatengeneza ajira na kuleta maisha bora kwa wote wengi hawakujua wote ni akina nani.
            Tatu, amefanikiwa kupata warithi wake kisiasa toka kwenye ukoo wake. Rejea mwanae kurithi nafasi yake ya ubunge wa jimbo la Chalinze huku mkewe akiibuka kuwa mjumbe wa vikao vikubwa vya chama. Pia usisahau alivyomwezesha mke wake kuanzisha NGO na kuweza kuongeza utajiri binafsi ukiachia mbali kujenga shule ya sekondari ya wasichana kwao. Sina shaka. Huyu mama niliyeambiwa ni mwalimu wa shule ya msingi tena mwenye elimu haba atakuwa ni tajri wa kutisha kama mke wa mtangulizi wa Kikwete, Anna Mkapa ambaye alianzisha utamaduni huu wa kujitajirisha kwa mgongo wa ikulu.
            Nne, Kikwete aliingia akisifika kuwa chaguo na kipenzi cha watu. Kweli amefanikiwa katika hili hasa ikizingatiwa kuwa chini ya utawala wake wengi waliokuwa waishie gerezani kama vile wezi wa EPA, Escrow, Kagoda, Richmond majambazi, wauza unga na wengine aliwapenda kiasi cha kuwaonea huruma asiwafunge.
Tano, Kikwete alifanikiwa kuitangaza nchi nje. Hadi juzi alikuwa ameishaizunguka dunia mara 410. Japo wabaya wake walimwita Vasco da Gama, kwa vile ni mtu wa watu hakujali na aliendelea na matanuzi yake.
            Sita, Kikwete amefanikiwa kujenga barabara nyingi hata kama ziko chini ya viwango na ni chanzo cha ajali ukiachia mbali kutolinga na kiwango cha fedha zilizotumika kuzijenga.
Saba, Kikwete amefanikiwa kukuza deni la taifa kiasi cha taifa letu kuwa miongoni mwa mataifa yanayokopesheka na yanayojua kutumia fedha.
Nane, Kikwete amefanikiwa kurahisisha elimu. Rejea jinsi wanafunzi wanavyosoma vitabu vichache ili wasiumize vichwa bure wakati elimu yenyewe haina soko hasa baada ya utajiri wa mkato kupitia jinai kama wizi na uuza mihadarati kugeuka deal. Rejea alivyoendelea kuwateua mawaziri waliotuhumiwa kughushi kama vile akina Mary Nagu, William Lukuvi, Deodorous Kamala, Makongoro Mahanga, Emanuel Nchimbi na wengine wengi tu bila kutaka wachunguzwe au kuadhibiwa kama manesi, polisi, walimu na mahakimu wanaofungwa na kufukuzwa kazi kwa kosa hilo  hilo.
Nane, amefanikiwa kuwaacha wanaotaka kumchimba na kujua utajiri wake wakibunia. Kwani , kwa miongo miwili amegoma kutangaza utajiri wake.
            Tisa, amefanikiwa kukiimarisha chama chake cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwezesha kuhamwa na mawaziri wakuu wastaafu wawili.
Kumi, amefanikiwa kuandika katiba mpya ya watawala na kuachana na ile ya kizamani ya wananchi iliyokuwa ikipigiwa upatu na akina Jaji Warioba.
Kumi na moja, chini ya utawala wa Kikwete wanyama wetu walipigwa jeki kwa kupandishwa ndege kwenda uarabuni ili kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia. Rejea Tanzania ilivyopata ugeni mkubwa wa machinga toka Uchina, India, Uturuki bila kusahau wafanyabiashara hodari wa pembe za faru na ndovu.
Kumi na mbili, Kikwete alifanikiwa kuweka uwazi na ukweli hasa kuwapasha watoto wa kike wa shule wanaopata mimba kuacha kiherehere chao ili wasidungwe mimba. Huu ni mfano mzuri wa kuigwa kwa kuwa na rais mwenye uchungu na mabinti zake hadi anawapa vidonge vyao japo kufanya hivyo si jibu iwapo wanaowadunga hawashughulikiwi kutokana na mfumo mbovu.
Kumi na tatu, Kikwete alifanikiwa kutoa uhuru kwa polisi kufanya watakavyo hasa kuwakomesha wapinzani na waandishi wa habari bila kusahau kuwachapa au kuwaua wananchi wanaojifanya kujuajua.
Kwa ufupi haya si mafanikio haba hata kama yanaweza kuwa na mshikeli. Mafanikio ni mafanikio yawe hasi au chanya. Cha mno atakachokumbukwa kwacho Kikwete ni kuacha nchi kujiendesha ikiwa kwenye autopilot kwa miaka nenda rudi huku yeye akiimarisha uhusiano wa kimataifa kwa kuizunguka dunia na kuitangaza duniani.
Hivyo ndiyo –binafsi –nitamkumbuka Kikwete. Je wewe msomaji utamkumbuka Kikwete kwa yapi? Tuonane jumapili ijayo.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 4, 2015.

Friday, 2 October 2015

Mlevi ampiga shule Fest Leidi


Baada ya Anna Tamaa Makapu na Salimia Kiquette kuugeuza ufesti leidi biashara, Mlevi ameamua kutoa nasaha kwa festi leidi ajaye. Kwanza ngoja nitoe utabiri wa kweli. Festi leidi ajaye atakuwa mwanamke.  Pili atakuwa na elimu ya wastani. Tatu, atakuwa anasikiliza ushauri wangu.
            Kwa vile nimeishazoea kuishi na festi leidi wangu wa walevi kwa zaidi ya miaka 20 ambavyo ni vipindi viwili vya urahis, nina uzoefu mkubwa na mafesti leidi. Mimi na gwiji Mchonga Kambarage wa Burito tuliwazuia mafesti leidi wetu kujiingiza kwenye uchuuzi na umachinga wa kwa mgongo wa ikulu. Hatukutaka ikulu iwe pango la wezi. Hatukuwaruhusu waanzishe kampuni almaarufu NGOs za uongo na ukweli. Mara Fursa za Ulaji kwa Wao mara MAWA. Wizi mtupu tena wa kichovu. Nani angekubali biashara hii kichaa yenye kutia aibu mamlaka? Kama ni kuhudumia akina mama si wizara ya wanawake na watoto ipo? Kwanini kuanzisha NGO mumeo anapoingia madarakani na si kabla kama si kutafuta utajiri wa haraka tena wa kifisadi? Piga buku kama Graca Machel uone.
            Basi, kwa vile ufisadi huu wa kichovu umeanza kukubalika, leo natoa waraka maalum kwa festi leidi ajaye.
            Kwanza, namtahadharisha na biashara ya NGO. Inachafua heshima yake, mumewe na utawala mzima. Mama anayejiamini hawezi kujificha nyuma ya mgongo wa mumewe.
            Pili, namshauri festi leidi ajaye asijiingize kwenye siasa za majitaka za kugombea vyeo uchwara kwenye chama cha mumewe simply because ni mke wa mwenyekiti. Wala asiruhusu watoto wake wala ndugu kutumia mgongo wa mzee kutafuta ulaji wa kisiasa au kibiashara kupitia NGO na upuuzi mwingine. Hata kama atakaidi akaenda kuomba kama jamaa yangu fulani ambaye mzee wake anaongoza kwa kwenda nje kubomu naye akifuatana naye kuomba misaada ya uongo na ukweli, ni aibu. Hata ukijengewa kijishule kimoja au viwili vya sekondari kama miradi binafsi bado hutaacha kuonekana mroho na mbinafsi na anayetumia madaraka vibaya.
            Tatu, namshauri festi leidi ajaye aende shule ajipigie kitabu badala ya kukimbizana na vijesenti vya aibu. Mfano wa kuigwa ni festi leidi wangu wa walevi. Hana NGO wala si mwanachama wa chama changu cha Ugali Nyama na Maharagwe (UNM). Nilipochaguliwa na walevi kula vyao kirahisi yeye aliamua kupiga book. Tena mwenzenu kasoma ughaibuni na hata akiongea ung’eng’e hapaniki, kubukanya wala kumiminikwa na jasho utadhani anakimbizwa.  Kisomi mchezo wa kutumia madaraka ya mzee kwa mhusika kujineemesha na jamaa zake huitwa Bedroom politics ambapo mhusika hutumia kitanda kama mtaji.
            Nne, asimsumbue mzee kwa kutaka ateue ndugu au mashoga zake kwenye ulaji hata kama hawana sifa. Aache kila mtu apige msele apate cheo kwa jasho na sifa zake.
            Pia festi leidi ajaye aepuke kupenda matanuzi kiasi cha kutaka kila safari anayofanya mzee ughaibuni naye awepo na mashoga zake kwenda kutoa tongo tongo. Si mmemuona rafiki yangu na mwanafunzi wangu Braaka Obamiza alivyokuja juzi Afrika. Hakuja na Michele wala Unga wala watoto wao. Siyo lazima kila anapokuwa baba na mama awepo hata kama anaruhusiwa kufanya hivyo.
            Tano, festi leidi aepuke kupenda makuu kama vile kupokelewa kama mzee aendapo kwenye shughuli zake binafsi. Walevi watachagua na kumuapisha mzee tu. Hivyo, lazima rahis awe mmoja. Ufujaji tulioshuhudia usirudiwe. Maana ni aibu na ni kishawishi cha kufanya Ukiwila kama aliofanya Anna Tamaa na mzee wake ambao sasa wanaishi kwa kutegemea kulindwa na wenye ulaji kwa sasa ambao nao watategemea kulindwa na mzee ajaye.
Sita, ngoja niishie hapa niende kukamata ulabu na bangi kidogo ili kuchemsha bongo.
Muhimu, festi leidi ajaye azingatie ushauri na uzoefu wangu kama rais wa Walevi watakatifu.
Tukutane ikulu!
Chanzo: Nipashe Oct., 3, 2015.

Wednesday, 30 September 2015

Kamanda Nkuzi alivyosherehekea Birthday yake




Kamanda wetu Nkuzi alitimiza miaka mitano sambamba na kuanza vidudu huku mdogo wake kama Nkwazi Jr akitimiza miaka mitatu wakati dada yao Mkubwa Nthethe alianza chuo kikuu mwezi huo huo. Tulisheherekea tulivyoweza kwa kutoka nje kidogo. 

Tuesday, 29 September 2015

Kipindupindu na wagombea urahis

   Baada ya kuona kampeni zikiendelea huku kila mgombea akija na sanaa zake za kuwaahidi wachovu neema wakati mwisho wa siku ni maafa, Kijiwe kimejitoa kimasomaso kuwataka waongelee gonjwa hili la uchafu liitwalo kipindupindu.
            Mijjinga ameingia akiwa na laptop yake leo kuonyesha kuwa mambo anayaweza. Anaiweka mezani, kuamkua na kutoa mpya, “Wazee mna habari kuwa mgombea mmojawapo amekumbwa na kipindupindu kiasi cha kuwa anakatiza hotuba kwenda msalani?”
            Kila mmoja anastuka. Mgosi anasema, “Una maana kipindupindu cha ubongo au? Maana tinaona wagombea wakisema vitu visivyoiinga akiini kiasi cha kuhisi wanakabiiwa na kipindupindu cha ubongo?”
            “Haswa. Kumbe nawe ni mwanafalsa Mgosi,” Anajibu Mijjinga huku akifuta fumbi laptop yake.
            “Hii mpya na kali! Yaani kipindupindu kimekuwa tishio hadi kukabili ubongo!” Mbwamwitu anachomekea.
            Mipawa anakwanyua mic, “Nadhani kuna ukweli usiopingika. Kuna kipindupindu cha ubongo kimekumba kampeni hizi. Maana sisikii wahusika wakiongelea katiba mpya iliyouawa na mafisadi, kupambana na ufisadi na kuondoa uoza unaoachwa na huyu anayeondoka kiasi cha kugeuka kipindupindu.”
            Msomi Mkatatamaa anatia guu, “Nakubaliana nanyi mia kwa mia. Hata kipindupindu chenyewe ambacho ni alama ya uchafu na umaskini hakiongelewi. Badala yake utasikia wasanii wakiongopa kuwa watatoa elimu bure. Kwanini msitoe elimu ya kipindupindu kwanza? Kwanini hawaongelei uchafu uliokithiri tena kwenye lisirikali ambapo wezi wanajiibia watakavyo kana kwamba kaya hii ni shamba la bibi? Nilitegemea majina kama Jimmy Rugemalayer, Singasinga, Ni zero Kadamage, Kisehna, Idd Lion na mengine yakitajwa na jinsi watakavyoyashughulikia.”
             Kapende anampoka Mgosi mic, “Mkuu hapa umewashika pabaya. Ulitegemea CcM waongelee escrow wakati waliianzisha wao na kupunyua uchache kwa ajili ya kampani ya kampeni? Ulitegemea Mr. Richmonduli aongelee uchafu wakati yeye ndiye bingwa wa kuutenda? Sidhani kama kuna mwenye ubavu wa kuongelea masuala nyeti kama vile katiba mpya au kupambana na ufisadi wakati wahusika wanaogelea kwenye uchafu huo. Ziko wapi nyumba za kaya zilizouzwa na Ben Tunituni Makapu wakati Dk Kanywaji alipokuwa waziri mhusika?”
            “Du mzee unapiga huku na kule bila kupindisha!” anachomekea Mchunguliaji.
            Kanji naye anaamua kukamata mic, “Dugu zangu hii pindupindu natisha sana. Sasa kama siasa kuba naharisha hadi nakimbia hotuba sisi vatu dogo takufa.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kutia guu, “Ni kweli Kanji. Sisi wadogo tutaangamia hasa ikizingatiwa kuwa tunakunywa maji ya visima vilivyojaa kinyesi. Hivi unategemea nini wakati visima vyenyewe vimechimbwa jirani na vyoo?  Huko chini maji yanaingiliana na hii ndiyo sababu kubwa ya wengi kuugua kipindupindu. Pia hatuna uwezo wa kwenye Ugabacholini kutibiwa kama wao.”
            Mpemba anashika mic, “Yakhe mie nshangaa hii roho mbaya ya hawa wasanii wetu wallahi. Waongelea vitu vya ndotoni wakati matatizo ya wazi wayaona na kujifanya hawayaoni. Heri hicho kipindupindu kingewakamata si ubongoni pekee hadi kwenye matumbo yao ili waonje joto ya jiwe wallahi.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakamua mic, “Dua la kuku halimpati mwehe kaka yangu Mpemba. Nadhani tatizo la kipindupindu ni la wachovu wenyewe. Wanapaswa kuanza kuchukua hatua za usafi ambazo si lazima wafundishwe. Hapa lazima tujilaumu wenyewe kwa kuingiliwa na gonjwa hili.”
            Mgosi Machungi anarejea, “Da Sofia nakuheshimu sana. Kama kuingiiwa si sote bali nyinyi mnaokii kuingiiwa. Nadhani wangeiingiwa wao kwanza ili kuonyesha kuwa viongozi wako mstai wa mbee ingekuwa poa.”
            Mzee Maneno anakula mic, “Waingiliwe mara ngapi wakati wameishaanza kuonyesha jinsi wanavyoharisha majukwaani? Hukumsikia aliyedai ataondoa umaskini kwa njia ya kutenda ufisadi kama ule wa Richmonduli? Hukumsikia mwingine aliyesimamia wizara ya ardhi akisema kuwa lisirikali liligawa ardhi vibaya utadhani yeye hakuwa kwenye lisirikali hilo? Hawa sidhani kama wana jipya zaidi ya kueneza kipindupindu cha kisiasa.”
            “Mzee Maneno una maneno kweli kweli. Umekumbusha habithi anayetembelea mashangingi kusema eti ataondoa mashangingi na kutumia hiyo njuluku kwenye kutoa elimu. Angekuwa serious si angepanda bajaj kam alivyofanya papa Francis kwa Joji Kichaka alikopanda bajaj na kukataa Beast la Obamiza? Wasanii, wanafiki na waongo watupu. Huwezi kuwa ndani ya Nambari Wani au UKAUA ukawa na jipya zaidi ya kipindupindu cha ubongo.” Anachombeza Kapende huku akibofya ki-Sumsung Galaxy 6 chake.
            Mpemba anarejea, “Mie naona walougua kipindupindu cha tumbo na ubongo ni wale waniodanganywa kwa ahadi hewa huku wengi wao wakiwaomba rushua wagombea ulaji. Kwani hatuoni mitaani ambapo nshiko watembezwa? Kama hawa waniodanganywa hawana kipindupindu sehemu zote inakuwaje wakubali hadaa na urongo wa nchana kana kwamba hawana akili?”
            Kanji anakatua mic, “Dugu yangu Pemba mimi penda veve sana. Nasema kweli tupu dugu yangu.”
            “Angalia Kanji. Eti umisema unampenda sana ii iweje dugu yangu? Veve napenda yeye vipi na kwanini. Hebu tieeze tieewe.” Anachomekea Mgosi huku akiangua kicheko.
            Mijjinga anyakua mic, “Tuache utani. Bila kuuondoa huu mfumo wa kifisadi hata aje malaika atatuambukiza kipindupindu cha ubongo kama hawa wanavyofanya. Sioni mstakabali wa kaya kwenye kampeni hizi zinazolenga kuamuliwa kwa kuangalia watu na siyo sera. Wengine wakiongea utadhani wamemeza chura.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si kunguru aliyeugua kipindupindu akatuharishia!
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 30, 2015.

Kumbe Rugemalira ameiweka serikali ya Kikwete mfukoni!


Makama wa rais Dk Gharib Bilal akimpa tuzo mkurugenzi wa Mabibo Spirits James Rugemalira mtuhumiw amkuu wa ufisadi wa escrow. Huu ni ushahidi kuwa kumbe jamaa bado anao ubavu wa kupewa tuzo kwa biashara chafu iliyotokana na fedha za wizi wa mabilioni ya shilingi ya umma. Ndoa hii ya serikali na fisadi ni hatari na ya kukatisha tamaa ukiachia mbali kupaswa kulaaniwa. Badala ya mhalifu huyu kuwa gerezani sasa yuko majukwaani akichangia hata miradi ya serikali hiyo hiyo aliyoifilisi! Ni ujinga au upumbavukuendelea kuwa na serikali inayolala kitanda kimoja na mafisadi?

Monday, 28 September 2015

When parties became diapers

          I recently was following what unfold in Australia where former premier Tony Abbot was unseated by Malcom Turnbull after being in power for just two years. Guess what, we attended the same university with this fella. Abbot’s predecessor spent only six months in power while Julia Gillard spent three years like Abbot. To cut a long story short, since Jake Kiquette came to power, Aussie has already seen six PM coming and going minus the incumbent. This informs us that PM (presidents for Tanzania) are changed like diapers. Why?  It is because there’s no longolongo there. You don’t deliver you hit the road whether you like it or not. No zengwes or what. And you can’t turn Aussies into dumbos like in Bongo.
          When it comes to kicking out governments, Greeks are second to none. They have had five elections in 2015. Since, 2012, Greeks have gone to polls ten times. They give no hoot to governments that don’t deliver. I wish Bongolalalanders were like Greeks.
          In a word, in Bongo politicians are changing parties like diapers. They’re fluky. They aren’t changed like diapers as indicated above in Aussie.  After some were ditched in their parties, they moved to others to seek ulaji. I don’t want to list down the bigwigs we saw decamping to the opposition. What I’m concerned with is this new tendency that the opposing side bared recently. It used to make us believe that it was fighting graft and archaic system to end up embracing emissaries from the same anathema they purported to fight!
          Like Aussies, we need to change them like diapers even if they change parties like diapers. You wonder a person like Makorongo Muhanga would decamp from the party that shielded him even when he faced forging allegations. I didn’t wonder to hear that even Mr Kagoda is supporting the opposing side while he got the dosh he’s burning from the laxity of those he is throwing mud at. Again, If Luwasa and Sumuye can attempt to cut the hand that used to feed them, anybody can cut the tree he is on.
          Another thing that begs us to change politicos like diapers is the fact that they monkey with everything and get away with murder. You’ll hear them promise to solve almost every problem while they actually are more a problem than the problems they purportedly want to take on.
          They monkey around on rostra and spread such false information such as bringing changes that was arrested or betrayed by the outfits sponsoring them. They promise a lot of goodies to end up crucifying the same boozers they duped. For those who remember what we are getting out of will agree with me that politicos are selling boozers down the river while they promised goodies. Despite spewing a lot of promises, politicos don’t get it done. What they’re good at is nothing but self-services as we evidenced on the all past regimes except Mchonga’s. When it comes to taking boozers for a ride, politicos and con men are but ying-yang-like, if not, identical-twin cohabitants. How on earth–for example–promise say jobs, factories, increasing pensions without showing how you’re going to do it and fall short of conning those you’re blatantly duping? How can you promise development without showing how you’re going to tackle obstacles to development such as corruption, mega theft, drug trafficking, tax evasion, capital flights and all the like? How can you do that without having a legal mechanism that empowers you to take on criminals that are always pampered simply because they know how to share the loots? As a boozer–though this can be seen as pushing the limits–methinks, nobody will do anything without having the New Constitution that corrupt bigwigs feared it would send to jail due to the crimes they committed in power. This is why I espouse changing politicos like diapers as we’ve seen in Aussie.
          Guess what. When it comes to addressing corruption, there are some politicos –especially those implicated–who don’t want to touch it. Why should they add fuel to the frame? Again, boozers seem not to get it. Instead of tasking those who want to rule them to address graft; they’re talking about personalities instead of issues! Mtaliwa sana!  Agitate for the system that will enable you to change politicos like diapers the way the politicos have shown in changing parties like diapers. Without tweaking the system all promises are but hogwash and hoo-has.
Source: Guardian Spet., 27, 2015.

Saturday, 26 September 2015

Matokeo ya uchaguzi yalete mabadiliko


          Hakuna ubishi. Kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba zimetawaliwa na watu na si masuala. Wagombea wanajinadi kwa sifa binafsi na si sera wanazotegemea kutekeleza. Masuala muhimu kwa watanzania yamewekwa kando. Ni bahati mbaya kuwa –kutokana na mfumo mbovu tuliorithi toka chama kimoja –wapiga kura hawana uwezo kisheria kuhoji.
          Si chama tawala wala upinzani, hakuna anayejikita kwenye sera zitakazoondoa matatizo ya watanzania ambayo yamekuwa yakiterekezwa na kila serikali inayoingia. Kwa mfano, watu wanajadili wagombea wenye ushawishi yaani mgombea wa Chama Tawala (CCM) Dk John Pombe Magufuli na mgombea wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Edward Lowassa. Hata ukiangalia hiki kinachoitwa UKAWA kimeondoka kwenye misingi iliyokiunda, yaani kutetea katiba ya wananchi. Wakati mwingine unashangaa kuona wale waliopinga na kuua katiba husika kuwa vinara wa kambi iliyokuwa ikikumbushia na kupigania katiba mpya.
          Kuna mambo mawili ambayo wapiga kura na wanaotaka kuchaguliwa wameyatelekeza au tuseme kuyaua. Mosi, ni katiba mpya. Na pili, ni namna ya kubadili mfumo wa kikale na mgando uliowaweka mateka watanzania kiasi cha mgombea, kwa mfano, wa chama tawala kutaka kubadili hali ukiwa ni ushahidi kuwa serikali ya chama anachowakilisha ilivuruga. Je serikali inayoondoka haikuvuruga? Jibu wanalo wasomaji na wapiga kura kwa ujumla. Kama ingekuwa ilifanya vizuri, basi mgombea wake asingeikosoa.
          Swali linalosumbua wajuzi na wachambuzi wa mambo ni: Je rais ajaye ataweza ku-deliver wakati mfumo wa kutomwajibisha haujaondolewa? Kwa mfano, rais ajaye hawezi kupambana na ufisadi au kutoushiriki wakati mfumo unamlazimisha kufanya hivyo. Kuweka suala hili kwenye picha rahisi, hebu angalia baadhi ya wagombea wanavyotoa ahadi za kuwapa watu vyeo kana kwamba vyeo hivyo ni mali yao binafsi. Wapo wanoona kama hii ni rushwa ya kitaasisi.
          Japo Dk Magufuli amekuwa akisema kuwa atapambana na ufisadi, je sheria au nyenzo inayompa mamlaka yaliyojitenga na utashi wa mtu binafsi viko wapi?  Magufuli amekuwa akiahidi kupambana na ufisadi huku akijua wazi hakuna mfumo sahihi wa kumwajibisha kama hatafanya hivyo kama alivyofanya rais anayeondoka. Kimsingi, ni hatari kutegemea utashi binafsi wa rais badala ya utashi wa kisheria na kimfumo. Jakaya Kikwete alipoingia madarakani, hata hakusumbuka kujiapiza kuwa angepambana na ufisadi. Na kweli hakupambana nao zaidi ya kuupamba kiasi cha mafisadi papa wengi kuwa washirika na marafiki zake. Rejea madai kuwa Kagoda kampuni iliyohusishwa na mshirika wake Rostam Aziz ilikwapua mabilioni ya fedha kwenye fuko la madeni ya nje EPA. Je mtuhumiwa alichukuliwa hatua gani zaidi ya kuamriwa –yeye na wenzake –warejeshe baadhi ya fedha hata bila kuhojiwa na polisi? Je wezi wa wizi wa kutisha wa hivi karibuni –hata kudaiwa walimshinikiza rais kwa njia ya email asiwachukulie hatua bila yeye kunanusha –wamechukuliwa hatua gani? Je rais ajaye ataweza kuwachukulia wahalifu hawa ambao ni serikali ndani ya serikali bila kuwa na nguvu ya kisheria? Hapa ndipo mantiki ya kuwashauri wananchi washinikize wagombea wajadili sera hasa suala zima la katiba mpya ya wananchi unapokuwa muhimu. Wananchi wakiendelea na usingizi huu wa kupumbazwa na ahadi hewa wataishia kulia sana hata baada ya kuwa na serikali mpya ambayo haitakuwa na jipya lolote zaidi ya business as usual.
          Hakuna awezaye kuleta mabadiliko –hata angekuwa malaika –bila kuwa na nyenzo ya kufanya hivyo kama vile sheria na mfumo unaolenga kuleta mabadiliko. Hivyo, kwanza, tuseme kuwa wagombea wanafanya usanii ili kupata madaraka. Na si kwamba hawajui umuhimu wa kujadili masuala badala ya personalities. Wanajua fika sema wanataka wapate madaraka yatakayowawezesha kuwa miungu watu kama hawa wanaotaka kuwarithi. Sidhani kama mtuhumiwa wa ufisadi au mgombea ambaye chama chake kimelea ufisadi anaweza kuongelea ufisadi. Akifanya hivyo, atakuwa anajitia kitanzi kisiasa. Laiti wapiga kura wangeliona hili na kulishupalia. Kama wapiga kura na watanzania kwa ujumla wataendelea kupumbazwa na ahadi lukuki na maneno matupu, wataishia kujilaumu watakapogundua kuwa kumbe walitapeliwa. Wakati muafaka wa kudai mageuzi ya kweli kwa kushinikiza kubadili mfumo ilikuwa sasa. Kama watanzania wangekuwa makini wangegomea hata uchaguzi au kutaka uchaguzi uendane sambamba na mkakati wa kufufua mchakato wa kupatikana katiba mpya iliyouawa kwa hofu ya waliotenda ufisadi wakiwa madarakani kufikishwa mahakamani. Je mtu binafsi tena aliyeteuliwa au kupitishwa au kuenguliwa na watuhumiwa wakuu ataweza kuwachukulia hatua waliomuumba? Kinachofanyika ni kituko kama kitachukuliwa kama harakati za kuleta ukombozi, mapinduzi na mabadiliko ya kweli katika maisha ya mwananchi wa kawaida wa Tanzania.
          Tumalizie kwa kuwaonya watanzania kuwa –kama wataendelea na mfumo huu –wasitegemee mabadiliko yoyote bila kujali nani watamchagua. Kimsingi, ni kama wanachagua baina ya pombe na mvinyo. Vyote ni vilevi na tofauti yake ni majina tu.
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 27, 2015.

Usalama mitaani: Fungeni tunguli si kamera

          Nilimsikia rahis Njaa Kaya akisema ana mpango wa kuhakikisha miji yote mikubwa kayani inafungwa kamera kudhibiti wizi na maafa mengine. Japo napiga mibangi na ulabu, naunga mkono wazo la kuhakikisha walevi wanatanua bila kusumbuliwa na mijambazi, mipaka hata mifisadi.
           Hata hivyo, nina ushauri tofauti. Badala ya kufunga kamera mitaani, kwanza, funga hizo kamera kwenye vituo vya kupigia na kuhesabia kura ili kuepusha uchakachuaji. Kwani, vidokozi si tatizo zaidi ya mfumo.  Wengi wanaamini kuwa tatizo la vibaka si kubwa kama lile la mafwisadi tena wanaolindwa na wazito walioahidi wangewalinda walevi ukiachia mbali kuwapunyua kodi za kutanulia kuiba kama vile ni shamba la bibi.
          Tunadhani tatizo ni wazito hasa mzito na wateule, marafiki na washirika zao kama vile akina Kagoda, escrow, EPA na wengine wengi.  Wakati tuliposikia hii kitu mlevi mmoja alisema eti hiki nacho ni kituko cha jamaa kuondokea. Kwani muda wote alikuwa wapi ukiachia mitaa yetu mingi kujengwa na kupangwa hovyo .  Walevi wanadhani fweza ambayo ingetumiwa kwenye usanii ingeelekezwa kubomoa mijengo iliyojengwa kinyume cha sheria na chini ya viwango kama ule wa uhindini. Au mijengo ya wanene iliyojengwa sehemu zilizokatazwa kama ule mhekalu wa Mchunaji Rwakatarehe na mingine mingi huko Ukwasini.
            Hata hivyo, jamaa pamoja na ulevi na mibangi yake, alikuwa na pwenti. Umeme wenyewe wa kuendeshea hizo kamera uko wapi?  Hivi kweli umeme wa mgao unaweza kuwaahidi ulevi usalama tokana na mikamera hii hewa au ni sanaa kama kawa? Kama kamera hizo ni dili basi fungeni Masaki na kote wanapoishi binadamu na siyo Uswazi wanakoishi wanyamawatu. Mitaa haina hata taa za barabarani wala za pembezoni mwake. Mijumba yenyewe imejengwa kama magugu na haina namba. Hizo Kamera zitafungwa wapi? Heri mfunge tunguli na si kamera wataziiba kama siyo kuzihujumu.
          Walevi tunapinga kwa nguvu zetu kufungiwa kamera mitaani kwetu. Zinaweza kutuchungulia hasa kwenye vyoo vyetu vya uswazi zitatuchungulia tunaoga na kunonihino. Pili, mnaweza kutupandishia kodi jambo ambalo litawanufaisha wezi wazito kwenye lisirikali.
          Tatu zinaweza kusababisha mabalaa mengine hasa wale wanaopenda kusimama mitaani na washikaji zao wa pembeni. Nasikia hata ndata wanalalamika kuwa zikufungwa kamera zinaweza kuwaacha bila nguo hasa wale wanaosindikiza mizigo ya wizi nyakati za usiku.
           Hata wenye gesti bubu nao wanalalamika kuwa kufunga kamera mitaani kunaweza kuharibu biashara yao ya chapchap. Na kama kweli mko serious basi mtavunja ndoa kibao. Mie mwenzenu nshafunga ndoa na ulabu na bangi. Sina wasi wasi wala kizuizi. Ila msinilaumu kama mtapuuza ushauri wangu.
          Kama kuna haja ya kufunga kamera basi zifunge kwenye vituo vya kupigia kura kwenye uwanja wa ndege, mipakani ili kuzuia mibwimbwi, madini na nyara zetu kutoroshwa nje. Tena kama ingewezekana kwenye maeneo nyeti kama haya tungeshauri zifungwe darubini ili tuwabaini wanaotugeuza mabwege. Pia tungeshauri zana hizi zifungwe kwenye ofisi zote za TRA, Bandari, Uhamiaji, Tanesco, TIC, hospitalini ili kuona wanaopunyua rushwa na kufanya kaya yetu iwe ombaomba wakati uchumi inao lakini inaukalia.  Hata Mjengoni kungefaa kufungwa zana hizi ili kubaini waishiwa vilaza na wanaoupiga usingizi ukiachia mbali wengine kuchangamkia posho bila kufanya lolote.
          Kama kweli jamaa ana maanisha basi ningemshauri afanye kitu moja ya nguvu. Yaani, afunge tunguli. Najua vidokozi na majambazi wengi walivyozoea ushirikina na upuuzi mwingine kama huo basi watazigwaya kuliko hata ukoma. Taarifa; Maswihiba zetu Saleh, Omari,na Hussein Assagaf wa Gerezani wamefiwa na dada yao mwezi uliopita. Salamu ziwafikie washikaji wote wa Gerezani, Kidongo Chekundu, Msimbazi na Lumumba. Nasikia mnakamata Nipashe ili kumsoma mshikaji wenu mlevi kama hamna akili nzuri. Msichunguliane. Kila mmoja anunue nakala yake na kufunua.
Chanzo: Nipashe Sept., 26, 2015.