The Chant of Savant

Saturday 25 August 2012

Mtu wa kwanza kwenda mwezini afariki


Neil Armstrong dies at 82. (Getty Images)


Jina Neil Amstrong likitajwa wengi hukumbuka 1969  mwaka ambao Amstrong alikanyaga kwenye uso wa mwezi na kuwa mtu wa kwanza kufanya hivyo. Tukio hili liliripotiwa dunia nzima na kuondoa hekaya nyingi za kweli na uongo juu ya mwezi. Tangu wakati ule sayansi ilikua na kuweza kufikia kuanza kwenda kwenye sayari nyingine za mbali kama Mars.
Amstrong rubani wa majaribio wa Kituo cha Utafiti wa Anga za Juu cha Marekani (NASA) amefariki akiwa na umri wa miaka 82. Baada ya kuwa mtu wa kwanza kwenda mwezini na kupata umaarufu dunia nzima, Amstrong hakulewa sifa. Mwaka 1971 alijiuzulu kazi katika Nasa na kuamua kwenda kufundisha unajimu chuo kikuu cha Cicinnati. Amstrong hakupenda makuu wala sifa zaidi ya kujiishia maisha yake binafsi kama mstaafu yeyote. Kwa habari zaidi kuhusiana na msiba huu BONYEZA hapa.



1 comment: