![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh5dZwI9i76iGBwqkk2DkqyOQ3VfgKzXnP0LEUfcKd5aayV_5PlVHf7uYEyYg7LOlPJpkk4sd4Hrb-j6DVEUVXVTPF_ZY0AnVcMb12hiFBVZAKJGf42-p_pyw7EO_dF5pXYLxXNUp4O/s640/IMG_7830.jpg)
Elimu ya mke wa rais wetu inatia shaka. Wengi wangependa ajiendeleze angalau aendane na wakati na majukumu na changamoto za kuwa mke wa rais. Kwa hali ilivyo hana muda wa kujiendeleza zaidi ya kuendeleza ziara hata bila umuhimu. Wengi wanashangaa huwa anaongea lugha gani huko au anaandamana na mkarimani anayelipwa kwa pesa ya walipa kodi. Je umefika wakati wa kuanza kuangalia na sifa za first lady ili kuepuka kuwa na first lady kihiyo anayeweza kutumiwa vibaya na wasaka ngawira? Tuzidi kumshauri first lady wetu kwenda shule ili aende na wakati. Madaraka yana mwisho lakini elimu haina. Ni ushauri wa bure tu.
1 comment:
Anasoma digrii Open University
Post a Comment