The Chant of Savant

Thursday 16 August 2012

Wakati Kenya wameamka Tanzania waendelea kuuchapa!


Jiji la Nairobi jana lilishuhudia maandamano ya wafanyabiashara wazawa kupinga wamachinga wa kichina kuendesha biashara za viosk. Wakati wachina wakiendelea kutawala biashara ndogo ndogo ya kimachinga maeneo ya Kariakoo jijini Dar, jijini Nairobi hawakaribishwi wala hawataachwa kufanya biashara hiyo ambayo ni ya wazawa wenye mitaji midogo. Machinga wa Kenya wanasema wazi kuwa wachina wamepewa tenda za kutosha za kujenga madaraja, barabara na urari wa biashara baina ya nchi mbili haulingani ambapo China huzoa pesa nyingi toka Kenya ikilinganishwa na Kenya inayopata kutokana na biashara baina ya nchi hizi mbili. Je tatizo hapa ni wakenya kutetea haki zao au watanzania kutojua na kutokuwa tayari kutetea haki zao? Je hapa nyenzo ni mwamko wa wakenya au usingizi wa watanzania?

No comments: