The Chant of Savant

Wednesday 26 November 2014

Kijiwe chalaani majanki yaitwayo majaji

Baada ya mhishimiwa mmoja ambaye ametokea kuwa mpenzi na shabiki wa kijiwe kututonya kuwa matwahuti ya lisirikali na Chama Cha Mafisi na Mafisadi (CCMM) wanasuka mbinu ya kutumia mapilato kuzuia kijiwe cha Idodomya kisijadili na kufumua kashfa ya ujambazi wa kijinga wa Esrew, kimeamua kuwalaani na kutoa onyo.
          Msomi Mkatatamaa ndiye anayeanzisha mdaharo wa leo. Anakunywa kahawa yake na kutafuna mic, “Waheshimiwa maprofesa madaktari na maguru wa elimu wa kijiwe hiki mna taarifa kuwa kuna matwahuti wanataka kuua mjadala wa kashfa ya esrew kule Idodomya?”
          Mpemba anajibu, “Yakhe mie hayo nimesikia magazetini. Hivi kweli hawa waheshimiwa wetu waweza kubali fanyiwa ushenzi kama huu watumika kama mihuri ya kuhalalisha haramu hii?”
          Msomi hangoji mwingine ale mic. Anakwanyua mic, “Basi wasomi, taarifa nilizopewa na mhishimiwa Davie Kafulia ambaye ametokea kuwa shabiki na mpenzi wa kijiwe hiki kitukufu ni kwamba kuna mpango wa kutumia baadhi ya majanki yaitwayo majaji kuzuia mjadala ili kuepuka walioko nyuma ya jinai hii wasijulike wala kusulubiwa.”
          Mgosi Machungi anadandia mic na kusema, “Msomi huu ni upuuzi. Mbona tinawajua wote walioiba hii njuuku kwa sura na majina?”
          Msomi anajibu, “Nadhani hamuwajui wote.”
          Kapende anadandia mic, “Msomi hapa umeniacha hoi. Eti hawa majambazi wa esrew hatuwajui? Unamaanisha nini Msomi?”
          Msomi analazimika kurejea , “Najua mnawajua baadhi yaani wale watano yaani prof Sossie Muongo, prof Benny Ndururu, Saidia Mkuyati, Mura Freddie We-rema, Aliar Kim Maaswi na Filisinchi Muramba. Je ni hao tu?” anamalizia kwa swali.
          Wanakijiwe wanatoa mimacho bila kujua waseme nini. Ndiposa Mijjinga anaamua kutia guu, “Kweli usemayo profesa emeritus Msomi mwenyewe. Nadhani kama tutafanya uchambuzi yakinifu na wa kina synthesis na analysis, tutagundua kuwa wanaopaswa kubanwa na kupewa kichapo kwenye kashfa ya escrew siyo hao uliowataja wala mzee Mizengwe Pinder. Wapo akina Jimmy Rugemalayer na ponjoro Singa Herbinger of lot.”
          Msomi anachomekea, “Hata wewe bado huwajui. Maana unaotaja ni makuwadi na dagaa wanaotumiwa na papa na nyangumi mwenyewe.”
          “Yakhe wamaanishani hapa uniposema papa na nyangumi?” Mpemba anauliza kwa kuudhika kidogo.
Msomi anajibu, “Kwani esrew ni kashfa ya nani kama siyo IpTL ambayo ililetwa makusudi kayani kuibia wachovu? Unajua walioingiza hili balaa hadi wafadhili wakachetuka?”
Baada ya kuona hakuna anayejibu, Msomi anaendelea, “Someni au tafuteni historia ya usaliti huu mtagundua kuwa uliingia chini ya utawala holela wa ruksia huku mzito Njaa Kaya akiwa waziri Nishati, Midini na Mimaji. Kwa taarifa yenu waliosuka dili zima ni mkulu, Milima ya Kigoma, Horasi Kolimbae, Endelea Chenga, Joni Mhavi-le, Bill Shija aliyerejesha namba hivi karibuni , Abdi Kigodae,Dan son of Jonah, Meri Ndosssi, Raph Moreli na Jimmy Rugemalayer. Hata hawa si wote.”
Kapende hangoji, anakamua mic, “Kweli hatuwajui. Duh! Kweli kaya hii inabunguliwa na hawa mchwa bila huruma. Ukiwaona utadhani wanadamu kumbe mafisi na mchwa wa kutisha!”
Sofi Lion aka Kanungaembe anaonekana kuudhika wazi wazi. Anatia guu, “Watu wengine kwa kutoa madai mazito bila ushahidi wanakera. Hivi unaweza kutupa ushahidi wa haya yote unayozusha?”
Msomi anamchomekea Sofi, “Da Sofi kwanza futa kauli yako kusema eti nazusha. Tatizo la wachovu ni kutojisomea. Mbona taarifa za huu uchafu ziko kila mahali. They are all over the place.”
Sofi anaonekana kushikwa pabaya. Hajibu. Kanji kuona hivyo anajitahidi kuingilia kati kumuokoa mshikaji wake. Anasema, “Sasa kama shahidi iko all owa the place kwanini bunge hapana shughulikia vote nafanya hii mbaya?”
Mheshimwa Bwege anaamua kutia daruga, “Si kwamba wahishimiwa wameshindwa kushughulikia hawa manyang’au wala si kwamba hawawajui. Wanajua kila kitu. Wapeni muda muone kama hatawafanya zaidi ya walichofanya walipoingizwa mkenge na akina Sam Sixx na kumtoa kafara Eddie Luwasha. Taarifa nilizo nazo toka ndani ni kwamba haponi mtu hata huyu mkulu anayejificha kwa Joji Kichaka akidai anauguza busha.”
Kijiwe hakina mbavu jinsi anavyokandia.
Mijjinga aliyekuwa akibofya kisimu chake anaamua kuuma mic, “Kwanza nakupongeza Prof Emeritus Msomi mwenyewe kwa kuweka mambo hadharani. Ni kweli. Hiki kinachoitwa screw ni zaidi ya hapo. Hapa lazima CCMM, lisirikali na Njaa Kaya mwenyewe wapigwe chini ili tujikomboe na kuanza upya vinginevyo wahishimiwa wakubali kugeuzwa waishiwa kwa kupania vidagaa wakati mapapa na nyangumi yakiendelea kukata maji na kusababisha madhara zaidi hasa kwenye ngwe hii ya lala salama.”
Anakunywa kahawa yake na kuendelea, “Kwa tunaojua chesi zima ni kwamba njuluku hii imeibwa ili kuelekezwa kwenye uchakachuaji mwakani. Hata huyu Luwasha mnayesema alitolea kafara yumo mzima mzima. Maana wanataka kumjengea mazingira kuwa alionewa na pia anakubalika kwa kutumia utafutaji mlo unaoitwa utafiti. Kwani hamjui!”
Mzee Maneno anaamua kula mic, “Yote tisa. Nilicheka pale niliposikia kuwa kuna baadhi ya majanki yanataka kutumiwa kuzima moto huu yasijue yanaongeza mafuta. Nadhani sasa mnaweza kuona ukweli na mantiki ya kupinga kwetu uteuzi wa kishikaji na kulipana fadhila. Maana tuna majanki mengi yaitwayo majaji yaliyoteuliwa si kwa sifa wala kufaa bali uchafu na ushikaji wao.”
Kijiwe kikiwa kinanoga si lakipita shangingi la janki moja! Wacha tulitimue ili tulivue ujaji!
 Chanzo: Tanzania Daima leo.
 
 

No comments: