The Chant of Savant

Tuesday 30 December 2014

Huu wimbo ni zawadi ya mwaka kwa viongozi feki wa dini

Tokana na kutamalaki kwa utapeli kwa kutumia jina la Mungu, blog hii imeamua kutoa wimbo huu kama dedication kwa wote wanaoibiwa na matapeli wa kidini kwa kutumia mbinu mbali mbali kuanzia kutenda miujiza, kutabiri, mihadhara,kupanda mbegu, kufukuza majini, kuombea taifa na nyingine nyingi. Ni vizuri watu wakaacha imani za kibubusa ambapo wanageuzwa mashamba ya bibi na matapeli wanaojificha nyuma ya neno la Mungu. Taifa letu linaanza kugeuka la kishirikina kiasi cha kuhitaji magwiji wa fikra na falsafa kuingilia kati. Haya ndiyo matokeo ya viongozi wenye uoni mfupi na watokanao na jamii za kishirikina.

No comments: