The Chant of Savant

Thursday 25 December 2014

Zawadi yangu bora ya Krsimas

 Huwa napokea zawadi nyingi na mbalimbali wakati wa Krsimas. Mwaka huu nimepokea zawadi ambayo imenifurahisha kuliko nyingi nilizowahi kupewa. Nimefurahi kiasi cha kushindwa kujizuia kuiweka hapa ugani. Hebu andamana nami uone zawadi niliyopewa ambayo bila shaka yaweza kukufaa hata wewe. Karibu.

Kwanza Samahani Mhango, sisi tunamfumo wetu wa utawala unaitwa sirikali siyo hiyo unayofikiri wewe serikali. Wewe haufahamu hatua za maendeleo ya sirikali yetu

Pili kimsingi sisi hatulazimishwi na taasisi au serikali yoyote duniani kufanya maamuzi kwa maslahi yetu.

Tatu utafiti tunaofanya sasa tutatumia watalaamu wetu kutoka peponi na kalumanzira ili kuwaletea majibu shetani wetu atakapojalia.

Nne katika kundi ketu la sirikali mtu ambaye siyo Kundi letu tumekwisha muondoa kwa kumfukuza madarakni tena bila shukurani.

Tano Jamaa zetu wa kundi letu tumekubaliana umma nchi za magharibi waikutishika kooni basi tunawashauri kujiuuzulu au kuwasimamisha tunawapatia mafao yao yote na kuwateua vyeo vingine pia, tunatoa shukurani kwa utendaji wao mzuri uliyotukuka kudumisha sirikali yetu.

Nategemea Mhango utakuwa umetuleewa na pia hii ni zawadi yako krismasi na heri ya mwaka mpya. Shetani wetu akubariki kwa mwaka ujayo.

Maana tutawekeza juhudi zetu katika kupata viungo vingi kutoka Zaruzaru kama mahitaji yetu kutoka kamati zetu karumanzira inavyosema ili tushinde uchaguzi katika sirikali yetu.

No comments: