The Chant of Savant

Tuesday 26 June 2012

Majambazi waheshimiwa wenye pesa Uswisi changamkeni basi


A virtul image of the new man-made, "island". An Austrian firm has come up what it hopes is the next big thing for the mega-rich: a man-made, floating "island" with a list price of 5.2 million euros ($6.5 million), the company's founder told AFP Monday. (AFP Photo/Ho)

Ingawa kuiba mali ya umma hata ya binafsi ni kosa la jinai, huwa kosa zaidi mwizi anapokuwa na tabia ya panya-yaani kuiba na kuficha ile pesa isitumike. Ukienda nchi ya jirani ya Kenya utaona utajiri wa watawala wao wezi. Ukija Tanzania kila mwizi anajifanya mjamaa wakati ukweli unajulikana kuwa ni mwizi wa mali ya umma kuanzia rais hadi mjumbe wa nyumba kumi. Misiseme nimesema rais mwizi. Hasha. Ila kwa jinsi rais Jakaya Kikwete na familia yake walivyokataa kutaja mali zao ukiachia mbali tuhuma za kila siku dhidi yao na dili zao, unaweza kumweka rais wetu kwenye kundi tajwa. Anyway, leo naandika kuwapa changamoto wezi wetu waheshimiwa wapenda uroda wa kila aina kuwa kuna mali hapo juu inapigwa seli. Hapa akina Lionchamwene hawana haja ya kwenda Guest House Unyampaani. Wanajitoma baharini na kufaidi ufuska wao. Malima A upo bwa mdogo? Na Njaa Kaya je?  Basi jiwahini. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: