Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Friday, 18 December 2015

Rais Magufuli tunusuru na akina Makonda tafadhali

            Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda si mgeni katika vituko. Baada ya kumshambulia mzee Joseph Warioba, hapo tarehe  2 Novemba 2014 rais mstaafu Jakaya Kikwete aliishangaza dunia kwa kumteua Makonda kuwa mkuu wa wilaya. Hatua hii ilifafsiriwa kama onyo kwa Warioba na wale wote waliokuwa wakipigania Katiba Mpya kuwa wangekomeshwa na mgenge ya wahuni. Wapo waliotafsiri uteuzi wa Makonda kama kulipa fadhila kwa kazi aliyokuwa ametumwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ikiongozwa na Kikwete. Wengi walihoji busara ya uteuzi huu ambao ulikuwa ni udhalilishaji wa moja kwa moja kwa mzee Warioba.
            Wahenga walisema: Mchovya asali hachovyi mara moja; na ukimtukana mzee mmoja utawatukana na wengine. Baada ya Makonda kujihisi kuwa hawezi kuguswa, aliendelea kutembeza ubabe hasa ikizingatiwa kuwa ndiyo zana na nyenzo iliyomfikisha hapo alipo kama tulivyoeleza kwenye sakata la kumshambulia, kumtisha na kumdhalilisha mzee Warioba. Kama vile ilikuwa imepangwa, Makonda aliteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni anamoishi mzee Warioba.
Kimsingi, Makonda alizoea siasa za kibabe na kihuni kiasi cha kuzigeuza kuwa ndiyo kanuni ya mchezo wenyewe asijue mambo yamebadilika. Gazeti moja liliandika “Ikumbukwe DC ndiye Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na DSO akiwa katibu wake, sasa mtu kama Makonda ambaye yupo tayari kufanya vurugu yoyote kutetea maslahi ya CCM leo kupewa u-DC wa Kinondoni tutegemee nini uchaguzi mkuu wa Oct 2015?” Kwa vile rais John Pombe Magufuli amepania kurejesha heshima ya taifa na uwajibikaji vya kweli, ni wakati muafaka kumtaka aondoe watu kama Makonda toka kwenye ofisi za umma. Maana, kuwapo kwao madarakani –licha ya kupingana na dhana nzima ya kuwakomboa watanzania –kunazidhalilisha ofisi za umma na kunapingana na hali halisi hasa ikizingatiwa kuwa wengi wa aina hii waliteuliwa kama njia ya kulipana fadhila bila kuzingatia uwezo na sifa za kushika nafasi hizo.
            Kuendelea kuwa na watu kama Makonda kutaanzisha vurugu. Chukulia mfano wa hivi karibuni ambapo Makonda aliamuru mbunge wa Ubungo, mheshimiwa Said Kubenea (CHADEMA) kukamatwa kwa vile walipishana lugha na kurushiana matusi. Huu ni ushahidi kuwa Makonda hajui thamani na mipaka ya madaraka yake. Kimsingi, ukuu wa wilaya siyo cheo cha majaribio wala kujaza wahuni na kusababisha kuvunjika kwa Amani. Makonda alikaririwa akimwambia Kubenea, “Unajua mimi ni nani?” Naye Kubenea alikiri kumjibu, “Wewe ni kibaka tu.”  Inakuwaje mkuu wa wilaya mzima anakosa adamu na uvumilivu ili kufuata njia zinazohusika kisheria anapovunjiwa heshima? Kama tunakuwa wakweli, nani ni nani kati ya mbunge ambaye ni mwakilishi wa kuchaguliwa na wananchi na mkuu wa wilaya ambaye anateuliwa na mtu mmoja kumwakilisha na si umma? Je wananchi wa Kinondoni wakiamua kusimama na mbunge wao –kama serikali itaendelea kumkingia kifua –je Kinondoni kutakalika? Kwanini Makonda hakuyapima yote haya? Sijui sifa za kitaaluma za Makonda. Hata hivyo , matendo yake yanamuonyesha kama mtu mbumbumbu asiyejua thamani na uzito wa mamlaka yake. Kimsingi, nukuu ya hapo juu kuwa unapompa Makonda ukuu wa wilaya tutegemee nini zaidi ya fujo ina mashiko. Kimsingi, alipopewa ukuu wa wilaya baada ya kumdhalilisha mzee Warioba, Makonda imekuwa ni sawa na chizi kupewa rungu jambo ambalo matokeo yake yanajulikana hata kwa kuku mwenye ubongo mdogo.
            Tunafahamu kuwa kuna wakuu wengi wa wilaya na mikoa walioteuliwa ‘kinamna’ wakati hawana sifa wala uwezo wa kushikilia madaraka haya makubwa. Hivyo, rais Magufuli atuondolee aibu na vurugu kwa kuwawajibisha mara moja watu wa namna hii ambao wanajulikana licha ya wao kujijua. Tulizoea kushangaa rais alipokuwa akitangaza uteuzi wa wakuu wa mikoa, wilaya, mabalozi hata baadhi ya majaji wasiofaa. Tulizoea kusikia wananchi wakisema, “Hata na fulani naye kateuliwa!” Ama kweli, ukishangaa ya Warioba utaona ya Kubenea kuhusiana na ubabe wa Makonda ulivyo!
             Hatupendi tuonekane tunamsakama Makonda. Ndani ya miezi miwili ameishaonyesha udhaifu usiokifani kuhusiana na nafasi na utendaji wa mkuu wa wilaya.  Ni vizuri Makonda akafahamishwa kuwa siasa za kutukana na kutishana au kufanyiana uhuni zimeishapitwa na wakati hasa wakati huu ambapo uchaguzi mkuu umekwisha. Makonda na wenzake walizoea kutumia matusi kuwatukana wapinzani kama mtaji wao bila kujua wananchi wanataka nini. Kubenea amechaguliwa na wananchi. Hivyo –kama mbunge wao halali –anapaswa kuheshimiwa na kulindwa. Inashangaza hata kitendo cha polisi kumkamata na kumweka ndani kwa amri ya mkuu wa wilaya bila kuangalia haki zake kama mwakilishi wa wananchi. Je Kubenea angekuwa mbunge wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) angekamatwa na kuvunjiwa heshima yake kwa amri ya mkuu wa wilaya anayejulikana kwa sifa na tabia zake za vurugu kama tulivyooneysha hapo juu? Kama Makonda amefikia kuwadhalilisha nguli waliochangia ustawi wa taifa hili kama mzee Warioba, atashindwa kuwadhalilisha wabunge wa upinzani? Je Magufuli anaridhika na siasa za majitaka kama hizi wakati kauli mbiu yake ni kazi tu na kutumbua majipu? Basi tunamuomba rais Magufuli chonde chonde, tumbua jipu hili Makonda.
Chanzo: Mawio Desemba 18, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 17:41

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


I Love My Country Tanzania

I Love My Country Tanzania

The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (42)
    • ►  July (6)
    • ►  June (7)
    • ►  May (5)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ►  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ▼  2015 (399)
    • ▼  December (34)
      • Kijiwe chastukia wanaojitia kuombea kaya
      • Magufuli amefika wakati muafaka ila anahitaji nguv...
      • Dr. Magufuli, relieve us of Makondas
      • Wachungaji wachunaji wamulikwe
      • Mlevi kushitaki sirikali The Hague
      • Burundi: Cry Beloved Country
      • Wanakijiwe walaani kubomolewa mijengo yao
      • If you believe Africa is the poorest continent thi...
      • I propose the magufulification of the new constitu...
      • Mkurugenzi wa Tanesco naye aachie ngazi
      • Mlevi aunda baraza lake la mawaziri mbadala
      • Rais Magufuli tunusuru na akina Makonda tafadhali
      • Are Mayardit and Machar waiting for indictment?
      • Kijiwe chajadili uteuzi wa Muongo
      • Do they look good really?
      • New Cabinet: Escrew will screw us even more
      • Motisha na kuzawadia wafichua uovu
      • Mlevi kuomba kukutana na rais
      • Kiquete kuingia na EPA kutoka na Escrow
      • Nimeipenda hii japo Kikwete, Muhongo na Escrow hawamo
      • Mwl Nyerere na mke wa Kaisari
      • AFRICA REUNITE or PERISH is out!
      • Unifying Africa: Lesson from the 2015 Sino-Africa ...
      • Kijiwe chaunda BEEP na kukosoa uamuzi wa Dk Kanywaji
      • Akina Makonda waache uhuni na kuvunja sheria
      • My poem appears in Poetry Nation!
      • How do you find this?
      • Mother Africa deserves this very song
      • Hello John Pombe Magufuli
      • Born With Voice
      • Africa should brace for Eco-imperialism
      • Kijiwe chajivunia uanachama wa Majaaliwa
      • Fighting Corruption pragmatically
      • Mlevi kuomba kukutana na rais
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.