The Chant of Savant

Monday 28 May 2012

Maafa yanayoikabili Mombasa somo kwa Dar


Hali ya mji wa Mombasa nchini Kenya (pichani) si shwari hasa kutokana na hasira za mama dunia. Taarifa zilizopo ni kwamba mji wa Momba unaweza kuzama kutokana na baadhi ya visima vya maji ya kunywa kuanza kuzama. Wataalamu wa mazingira wanaonya kuwa hii imesababishwa na kuchimbwa visima vingi na kujengwa majengo marefu karibu na fukwe. Kinachoendelea Mombasa ingawa hakijajitokeza Dar es Salaam, ukweli ni kwamba muda si mrefu kitatokea. Hii ikiongozewa na serikali ya Tanzania kutotoa huduma za maji kiasi cha kuwekeza kwenye visima vya kuchimba hovyo hovyo, ukubwa wa jiji la Dar na majengo mengi yanayojengwa kihohela. Kwa habari zaidi kuhusu Mombasa BONYEZA hapa.

No comments: