The Chant of Savant

Wednesday 30 May 2012

Kwa hili nampongeza Sitta hata wakenya wamponde



Kenya na nchi nyingine za Jumuia ya Afrika Masharika hawana raha na Samuel Sitta na Tanzania kwa ujumla. Hii ni baada ya kuwawekea ngumu kuingiza suala la ardhi kwenye jumuia. Taarifa toka kwenye vyombo vya habari zimeonyesha chuki kiasi cha kuanza kutafuta pa kushika kuiadhiri Tanzania ionekane kama mnafiki. Maana kichwa cha habari kinasema kuwa Tanzania inahubiri maji na kunywa mvinyo. Tulishaonya kuwa hakuna mantiki ya kuwa na muungno wa Afrika Mashariki wakati nchi zote isipokuwa Tanzania hazina ardhi na zina idadi kubwa ya watu. Chukulia mfano Kenya ambayo ni chini ya nusu ya Tanzania ina idadi ya watu sawa na Tanzania. Kama ni kuungana heri tuungane na Msumbuji na Zambia lakini si nchi zisizo na raslimali wala ardhi. Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: