The Chant of Savant

Saturday 28 April 2012

Je wakuu wa EAC wataridhia upuuzi wa wabunge wao?




Hakuna kitu kilichotustua kama wabunge wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EALA) kujiingiza kwenye mjadala wa kijinga kuhusiana na watuhumiwa wa mauaji na vurugu za baada ya uchaguzi wa Kenya wa 2007. Bunge la Afrika Mashariki lilipitisha hoja ya kutaka eti Kenya iunde mahakama yake ya kuwashughulikia watuhumiwa wa nne wajulikanao kama Moreno Four. 
Kimsingi, wabunge wenye busara hawawezi kuanza kupingana na sheria za kimataifa tena kwa faida ya kikundi kidogo cha watu. Heri wabunge hao wangetumia fursa hiyo kupitisha sheria bora za uchaguzi ili kuondokana na uchakachuaji ambao ni chanzo cha upuuzi na mauaji ya Kenya. Je marais wote wa EAC wataingia mkenge wa Kenya na kujitia kwenye aibu ya kuanza kupambana na ICC jambo ambalo ni sawa na kutwanga maji?

No comments: