The Chant of Savant

Thursday 26 April 2012

Wakubwa kutembea na dola ni fasheni?


Pichani ni Kikwembe (juu) na Malima (chini)
Baada ya waziri mdogo wa Nishati na Madini, Adam Malima kukiri kuibiwa vitu mbalimbali hotelini mjini Morogoro hivi karibuni, hakuna kilichovuta hisia kama kumilki bunduki mbili na pesa za kigeni dola 4,000. Wengi walijiuliza dola za nini ndani ya nchi? Jana mjini Dodoma kwa mara nyingine mbunge mmoja aitwaye Prudensiana Kikwembe aliibiwa kadi za benki na pesa taslimu dola 600 na shilingi 180,000. Je inakuwaje wakubwa wahusudu kutumia dola huku wakimomonyoa sarafu yetu? Je hiki ndicho chanzo cha kuendelea kushuhudia shilingi yetu ikiporomoka bila ya wakubwa kujali kwa vile wana uwezo wa kujipatia dola kwa njia wajuazo ziwe halali au haramu?

No comments: